Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE aliuliza:- Kumekuwa na changamoto kwa baadhi ya vituo vya Afya Mkoani Mwanza kukosa vyumba vya upasuaji:- Je, ni nini mpango wa Serikali wa kupunguza vifo vinavyotokana na uzazi kwa kucheleweshwa kufanyiwa upasuaji?

Supplementary Question 1

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu hayo kutoka Serikalini, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Ilemela ilifanikisha kuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Kata ya Buswero na walifanikisha kukamilisha majengo ya OPD na vilevile jengo la magonjwa ya dharura. Hata hiyo, kutokana na changamoto zilizokuwa pale, wakaona hapafai kuwa na Hospitali ya Wilaya maeneo yale wakaanzisha ujenzi katika Kata ya Bugogwa:-

Je, Serikali haioni kwamba kuna umuhimu wa majengo yale kuanza kutumika sasa kama Kituo cha Afya, kwa sababu yanakidhi haja hiyo ya kuwa kituo cha afya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, swali langu la pili nianze kwa kuishukuru Serikali kwa kutujengea Kituo cha Afya cha Malya Wilayani Kwimba. Kwa kweli ni kituo kizuri kinatoa huduma kwa wananchi wengi Wilayani humo, lakini kimekuwa na changamoto zifuatazo: hakina Mganga Mkuu na mhusika mkuu pale ni Clinical Officer; vile vile hakina mtaalam wa Maabara, hakina chumba cha upasuaji, hakina Daktari wa Akina Mama na Watoto; na bahati nzuri Naibu Waziri, Mheshimiwa Waitara ameshafika katika hiki kituo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, swali langu ni moja: Je, ni lini Serikali itahakikisha kwamba changamoto hizi zinapungua ili tuweze kupunguza vifo vya akina mama na watoto?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza Mheshimiwa Maria anauliza juu ya umuhimu wa eneo ambalo lilikuwa limeshaanza kujengwa Hospitali ya Wilaya lakini ikaonekana kwamba hapafai ni bora kikajengwa kituo cha afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze kwa dhati. Hata pia Mheshimiwa Angelina Mabula amekuwa akiliongelea suala hili kwa muda mrefu. Ni adhima ya Serikali kuhakiksha kwamba tunaondoa congestion katika maeno yote. Kwa hiyo, eneo lile na majengo ambayo yameshajengwa, hakika naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, inafaa kabisa kuwa Kituo cha Afya baada ya maboresho machache ambayo yataenda kukamilishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, Mheshimiwa Mbunge pamoja na kwamba amesifia tunashukuru kwa hizo pongenzi kwamba Kituo cha Afya kimeshaanza kufanya kazi nzuri, lakini kinakosa baadhi ya wataalam. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni azma ya Serikali kwamba yale majengo kwa maana ya vituo vya afya hatujengi ikawa kama picha. Tunataka wataalam wanaohusika ili upasuaji na shughuli zote zinazotakiwa kwenye kituo cha afya ziweze kufanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira. Wakati mwingine kuna watalam ambao ni lazima wawe trained. Kwa mfano, katika upasuaji lazima tuwe na wale watu ambao wanatoa dawa za usingizi na ndiyo maana tumewapeleka kuwa-train. Naamini na kituo hicho ambacho anakiongelea kitapata wataalam hao.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE aliuliza:- Kumekuwa na changamoto kwa baadhi ya vituo vya Afya Mkoani Mwanza kukosa vyumba vya upasuaji:- Je, ni nini mpango wa Serikali wa kupunguza vifo vinavyotokana na uzazi kwa kucheleweshwa kufanyiwa upasuaji?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Halmashauri ya Mji wa Tarime, kata zote zilikuwa haina kituo cha afya bali walikuwa wanategemea Hospitali ya Mji. Tunashukuru tumepata Kituo cha Nkende ambacho kinaendelea kujengwa; lakini kuna kata nne za pembezoni ambazo zina zahanati tu, kwa maana ya Kata ya Kitale, Kata ya Kanyamanyori na Nanyandoto. Wananchi wa katia ya Kanyamanyori wameamua kuchangishana ili kuendeleza kile kituo cha afya kwa maana kujenga maternity ward na maabara:-

Ni lini sasa Serikali itawatia moyo wananchi wale kwa kutoa fedha kuweza kujenga kituo afya cha ili kupunguza vifo vya mama na watoto?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepata fursa ya kutembelea Jimbo la Mheshimiwa Mbunge na nikatembelea Hospitali ya Wilaya ambayo mwanzo ilikuwa inahudumia maeneo mengi sana kiasi kwamba kukawa kuna congestion kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge mwenyewe anakiri na anashukuru kwamba kimeanza kujengwa kituo cha afya na imebaki hizo kata ambazo yeye amezitaja. Naomba aendelee kuiamini Serikali kwamba kama ambavyo tumeanza kujenga katika hiyo kata kwa kadri bajeti itakavyoruhusu, tumeahidi tutatekeza na katika kata nyingine kwa jinsi bajeti itakavyokuwa inaruhusu.

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE aliuliza:- Kumekuwa na changamoto kwa baadhi ya vituo vya Afya Mkoani Mwanza kukosa vyumba vya upasuaji:- Je, ni nini mpango wa Serikali wa kupunguza vifo vinavyotokana na uzazi kwa kucheleweshwa kufanyiwa upasuaji?

Supplementary Question 3

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Katika ziara ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI mwaka 2018 katika Jimbo la Monduli aliahidi kumalizia ujenzi wa Vituo vya Afya vya Nararami na Lemooti.

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake kwa wananchi wa Monduli?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kama ambavyo katika swali lake ameuliza kwamba Mheshimiwa Waziri wa Nchi TAMISEMI aliahidi juu ya ujenzi kumalizia vituo vya afya viwili katika Jimbo lake, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, hakuna hata siku moja ambayo Mheshimiwa Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI alishawahi kuahidi akakosa kutekeleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuvute subira. Kwa muungwana ahadi ni deni, nami nitamkumbusha kwamba kwa Mheshimiwa Kalanga uliahidi kumalizia vituo vya afya hivyo viwili. Kwa kadri fedha itakavyopatikana, hakika naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, hivyo vituo viwili vya afya vitaweza kumaliziwa.