Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:- Hivi karibuni Mheshimiwa Rais alitoa agizo la kutatua migogoro ya vijiji na hifadhi mbalimbali na orodha ya vijiji vyenye migogoro toka Jimbo la Nkasi imefikishwa na kupokelewa na Wizara:- Je, ni lini migogoro ya vijiji vya Kasapa, King’ombe, Mlambo, China, Nkomanchindo na vinginevyo vilivyoondoshwa vitapatiwa ufumbuzi?

Supplementary Question 1

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa majibu haya yaliyotolewa na Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Mnamo mwezi wa pili mwaka huu wahifadhi wa Rwafi Game Reserve, walifyeka mazao ya wananchi wa kijiji cha King’ombe zaidi ya hekari 359 za mazao mbalimbali. Wakati wanafyeka agizo la Mheshimiwa Rais lilikuwa limekwishatolewa na sasa wananchi hawa hawana chakula. Je, Wizara ipo tayari kufidia chakula hicho walichofyeka?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili chakula ni uhai na moja kati ya hitaji la msingi la maisha kwanini Wizara inafikiria kwamba kufyeka ni kusuluhisha migogoro inayojitokeza badala ya kutafuta suluhisho lingine?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze kwa sababu amekuwa akitoa ushirikiano mkubwa sana katika kutetea wananchi wanaoishi kando kando na maeneo ya hifadhi. Lakini taarifa kwamba mwezi wa pili mwaka 2019 askari wa Rwafi Game Reserve walifyeka mazao kwenye hekari 359, ndiyo nazisikia leo na iwapo ni kweli kwamba taarifa hizi zipo na zimefika katika Wizara yangu, basi Wizara itachukuwa hatua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili Mheshimiwa Mbunge anataka kufahamu kwamba kufyeka mazao ndiyo suluhu ya migogoro hii lakini pia athari zake kubwa kwa wananchi ambao watakosa chakula. Mheshimiwa Rais alikwisha toa maelekezo na askari wetu wote wanajua katika hifadhi zetu zote za Taifa ni marufuku kufyeka mazao ya wakulima kwa sababu mazao mengi ni ya muda mfupi na iwapo hili linaendelea kutokea naomba Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane ili tuweze kuchukuwa hatua.

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:- Hivi karibuni Mheshimiwa Rais alitoa agizo la kutatua migogoro ya vijiji na hifadhi mbalimbali na orodha ya vijiji vyenye migogoro toka Jimbo la Nkasi imefikishwa na kupokelewa na Wizara:- Je, ni lini migogoro ya vijiji vya Kasapa, King’ombe, Mlambo, China, Nkomanchindo na vinginevyo vilivyoondoshwa vitapatiwa ufumbuzi?

Supplementary Question 2

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Migogoro kati ya wananchi na hifadhi zetu ni ya muda mrefu kwanza ni-declare interest kwamba nilikuwa kwenye Bodi ya TANAPA, na wakati ule walitayarisha ramani ambayo wameainisha maeneo ambayo wanaweza kuwaachia wananchi na maeneo ambayo watawatoa wananchi kwa kuwapa fidia kwa sababu ya ikolojia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni kwanini Serikali haitumi hiyo ramani ya TANAPA ambayo walishaitayarisha kuweza kutoa suluhu ya hii migogoro kati ya wananchi na hifadhi ambayo imekuwa inaendelea kwa muda mrefu.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba migogoro hii ya maeneo ya hifadhi na vijiji imekuwepo kwa muda mrefu, na nadhani kama Mheshimiwa Mbunge anafahamu, wakati Mheshimiwa Rais anatoa maelekezo ya kutokuviondoa vijiji 366 ambavyo vinapakana na hifadhi. Vijiji hivi havikuwa vimeanza migogoro miaka ya hivi karibuni vingine vipo vimesajiliwa tangu miaka ya 70.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya Tume Maalumm iliyoundwa na Serikali kupitia jambo, hili imegundua kuna vitongoji zaidi ya 800 ambayo vina migogoro pamoja na hifadhi zetu za taifa. Kwa hiyo, nimuombe tu Mheshimiwa Mbunge kwamba ushauri wake huu wa kutumia ramani ambayo ilipendekezwa na watu wa TANAPA tumeupokea, lakini pia tuendelee kusubiri maelekezo ya Tume Maalum iliyoundwa kumaliza kabisa migogoro hii ya hifadhi.

Name

Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Primary Question

MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:- Hivi karibuni Mheshimiwa Rais alitoa agizo la kutatua migogoro ya vijiji na hifadhi mbalimbali na orodha ya vijiji vyenye migogoro toka Jimbo la Nkasi imefikishwa na kupokelewa na Wizara:- Je, ni lini migogoro ya vijiji vya Kasapa, King’ombe, Mlambo, China, Nkomanchindo na vinginevyo vilivyoondoshwa vitapatiwa ufumbuzi?

Supplementary Question 3

MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Pamoja na Serikali kuendelea kutatua mgogoro wa hifadhi, uko mgogoro mkubwa kando kando ya mapori yetu wanyama wakali tembo kusababisha vifo kwenye maeneo ya Mwalali, Kuyu na Matongo. Serikali ina mkakati gani sasa kutatua mgogoro mkubwa huu kwa sababu tembo wanaendelea kuzaliana, na wanaleta madhara makubwa katika maeneo yetu?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nikiri kwamba baada ya Serikali kuongeza juhudi za ulinzi wa hifadhi na kudhibiti majangili, limekuwepo tatizo la wanyama wengi sasa kuanza kuvamia maeneo ya vijiji na maeneo mengi ambayo taarifa tumezipokea ni kwamba, wanyama kama tembo na wanyama wengine wamevamia mashamba na kuna maeneo ambayo wamesababisha vifo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua ambayo Wizara imechukua, kwanza tumeimarisha kikosi chetu cha ulinzi lakini tunaelekea sasa kuanzisha vituo maalum kwa ajili ya ulinzi kwenye kanda. Katika maelekezo ambayo tumeyatoa, maeneo mbalimbali tuliyokwenda tumezielekeza halmashauri zote ambazo zinapakana na maeneo ya hifadhi kuhakikisha kwamba katika maombi yao ya watumishi wanaajiri Maafisa Wanyamapori ambao wataweza kufika kwenye maeneo yenye migogoro kabla sisi askari wetu hawajafika.