Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA (K.n.y. MHE. AUGUSTINE V. HOLLE) aliuliza:- Migogoro ya wafugaji na wakulima nchini imekuwa ya kudumu na hivyo kusababisha vifo kwa watu na uharibifu wa mali:- Je, Serikali haioni ni wakati muafaka kuja na Sera ya kupunguza idadi ya mifugo nchini ili kuwa na ufugaji wenye tija?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Waziri naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

(i) Kwa kuwa Msitu wa Makele kusini ambao tayari umesha poteza sifa ya uhifadhi, na kwa kuwa tayari yapo maelekezo ya kutoa sehemu ya misitu hii kwa sababu ya wafungaji ili kuondoa usumbufu uliopo kwa nini sasa Serikali isitoe msitu huu wa Makele kusini kwa ajili ya wafugaji?

(ii) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa suala hili la mifugo imekuwa na changamoto kubwa, sambamba na Jimbo la Nyamagada unapozungumzia masuala ya mifugo kwenye minada ya upili watu wana Nyamagana hawana kabisa eneo la kufanyika shughuli zao za uchinjaji na kwa maana mnada. Na kwa sababu na mifugo hii imekuwa inatangatanga mtu anayetoa mfugo Magu lileta Mwanza au anayetoa mfugo Kwimba kuleta Mwanza analazimika kupeleka Misungwi kwenye mnada wa upili ndio arudishe Nyamagana kwa ajili ya uchinjaji au Ilemela na matokeo yake kuongeza gharama za mchinjaji. Ni nini Serikali inatoa kauli gani juu ya minada hii kwa nini usirudishwe pale pale ulipo Nyamgana na watu wakachinja kwa uzuri?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza ni juu ya kuomba msitu wa Makele kusini kupewa wafugaji. Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Joseph Magufuli mwaka 2016 alipotembelea katika Mkoa wa Kigoma, alipita katika Wilaya Kasulu na wananchi wa Kasulu walimpa maombi yao ya kuomba msitu huu wa Makele kusini upewe wananchi kwa maana ya shughuli za ufugaji na kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais alielekeza hekta zipatazo 10,000 zitolewe kwa vijiji viwili 5,000 na 5,000 zigawiwe kwa Halmashuri ya Kasulu. Watendaji wa TFS kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii wametekeleza agizo hili na wananchi wa Kasulu wamepatiwa. Hivi sasa tulichokipendekeza baada ya maelekezo mengine juu ya Rais wetu juu ya kuwapa wafugaji na wakulima maeneo ya ziada kwa ajili shughuli zao tumependekeza eneo la Mkuti katika Wilaya Kasulu na Uvinza ndio sasa yaelekezwe kuangaliwa kama yamepoteza sifa yapewe wafugaji na wakulima. Naomba Mheshimiwa Vuma na wafugaji na wakulima wote katika Wilaya ya Kasulu waendelee kuwa na subra pindi jambo hili litakapokuwa tayari watapata manufaa hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili linahusu minada ya Upili na kwa nini wachinjaji wa pale Mwanza Jiji wanalazimishwa kupeleka mifugo yao katika mnada wa Upili wa Msungwi ndipo waende kuchakata mifugo hiyo pale Mwanza Jiji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huu ni urasimu kwa sababu mifugo tumekubaliana ya kwamba minada ya Upili dhumuni lake ni kwa ajili ya wafanyabishara kwa kiwango cha kati na kuwango cha juu. Kwa wale wafanyabishara wadogo wadogo wenye ng’ombe mmoja wawili ama mbuzi mmoja wawili wanaruhusiwa kununua katika minada yao ya misingi na kwenda kuchakata moja kwa moja kwa ajili yakuweza kufanya shughuli hizi za kujipatia kipato na kuhudumia wananchi. Natoa maelekezo kwa watendaji wetu wasimamie sheria kanuni zetu bila kuathiri wananchi wetu na kuinua vipato vyao na kuendeleza maisha yao.