Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Mgogoro wa ardhi kati ya Jeshi la magereza na wananchi wa Kata ya Ukondamayo hususan Kijiji cha Tumaini umedumu kwa muda mrefu sasa. Je, Serikali inachukua hatua gani kutatua na kumaliza mgogoro huu?

Supplementary Question 1

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa niulize maswali ya nyongeza mawili kama ifutavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimhakikishie Naibu Waziri aliyejibu maswali pamoja na Bunge kwa ujumla kwamba Mgogoro bado upo kati ya magereza na Kijiji cha Tumaini. Na uthibitisho ninao naomba nikukabidhi vithibitisho nilivyonavyo. Wananchi wanajua haki zao wanajua beacons zilizowekwa na baadaye kuondolewa, kwa hiyo mgogoro bado upo sasa maswali mawili kama ifuatavyo:-

(i) Kwa kuwa Serikali inasema imemamliza mgogoro wananchi wa kijiji cha Tumaini wanasema mgogoro bado upo. Je huoni kwamba kuna umuhimu wa wewe mwenyewe kwenda kuangalia nani anayesema ukweli na kutatua tatizo hili?

(ii) Kwa kuwa urambo kuna migogoro mingi kuhusiana na mipaka na hata ile inayopakana pori la akiba la ugala ikiwemo sehemu Indenda, Lunyeta, Uyumbu, Tevela pamoja na Ukondamoyo.

Je huoni Mheshimiwa Waziri kwamba utakapokwenda kutatua tatizo la Tumaini na magereza pia utatue migogoro mingine iliyopo hapa na ninapendekeza pia kwamba ufuatane na Waziri wa Maliasili kwa sababu pia vinahusiana pamoja?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI (K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kulikuwa mgogoro kama ambavyo nimeeleza katika jibu langu la msingi na mgogoro huo ulitatuliwa lakini tukumbuke tu kwamba vijiji hivi vilipimwa mwaka 2013. Lakini wakati huo gereza lile lilipimwa mwaka 1988 maana yake gereza lilitanguliwa likiwa na ekari 10,416 baada ya kuwa na mgogoro walipunguza kiasi cha ekari 7,198 kama nilivyotaja kwa vijiji ambavyo nimevitaja kwenye jibu la msingi la gereza likabaki na ekari 3,218.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Mheshimiwa Mbunge kwa sababu amekuwa akilifuatilia hili suala la mgogoro na ana vielelezo vingi vya wananchi wake wakilalamika nipende kumkubalia alichosema kwamba twende pengine tukaangalie uhakika uliopo nasema nipo tayari kwenda kwa ajili kuangalia mgogoro uliopo ili tuweze kuumaliza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili alikuwa anaongelea mgogoro wa mipaka katika maeneo mengine ambao yanaingiza kwenye pori la akiba sasa niseme hili pia katika ule msafara wa mawazie nane walikuwa wakipitia migogoro hii yote ilikuwa imehusisha Wizara ya Maliasili, TAMISEMI lakini wakati huo huo aridhi na Mambo ya Ndani pia walikuwapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, cha msingi hapa ni kufanya ufuatiliaji wa kina kwanza tuone hivi vijiji alivyovitaja vya Senda, Tundu na Ukomola kama vipo kwenye vile vijiji 366 ambavyo vilikuwa vimeainishwa katika kile kitabu kibwa cha migogoro. Kama napo kutakuwa kuna shida basi nitakapokuwa nina-solve mgogoro wa hili gereza na vijiji vya tumaini basi tutafika na hili pori la akiba tuweze kuona nini cha kufanya. Ahsante.