Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:- Je, ni lini barabara ya Mvumi Mission itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Swali la kwanza Mheshimiwa Naibu Waziri katika jibu lake amesema ujenzi umeshaanza. Je, yuko tayari kuongozana na mimi kesho ili akaone ujenzi kama umeanza au watu wake wamemdanganya?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kutokana na kunyesha kwa mvua barabara nyingi siyo tu zimeharibika bali zimeoza na hii imepelekea wazazi kupata shida kufika hospitali hasa kwa barabara ya Huzi kuja Manda ambapo ukitoka Manda kuja Huzi kuja kwenye Kituo cha Afya cha Mpwayungu, lakini Mvumi Mission hakuingiliki pande zote, madaraja yamezingirwa na maji na yamevunjika.

Mheshimiwa Naibu Waziri anatuambiaje kuhusu kutengeneza kwa haraka ili kunusuru maisha ya akinamama na watoto na wagonjwa akinababa ili waweze kufika hospitali? Ahsante sana.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nakushukuru na naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Lusinde, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, jibu langu la msingi nimesema kwamba maandalizi ya ujenzi wa barabara umeshaanza si kwamba barabara umeanza, maandalizi yamekwishaanza. Kama tumeshaanza niko tayari nipo tayari kuongozana naye kwenda kuangalia hatua ambayo imekwishafikiwa.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ambalo kimsingi ni swali ambalo linahusu Wabunge wote humu ndani kwamba baada ya mvua ambazo kimsingi zimeanza na zinaendelea sana barabara nyingi zimeharibika, Mheshimiwa Waziri wa Nchi ameshaagiza Meneja wa TARURA wa Tanzania na Mameneja wa Mikoa na Wilaya wafanye tathmini na walete bajeti ili tufanye utengenezaji wa haraka katika maeneo mbalimbali ili huduma muhimu ziweze kufanyika.

Kwa hiyo, naomba nitumie nafasi hii kuwaelekeza pia, Meneja wa TARURA wa Mikoa na Wilaya kwamba kazi ambayo wamepewa na Mheshimiwa Waziri wa Nchi waifanye haraka sana na kuchukukua hatua ya dharura ili kuhakikisha kwamba huduma za afya zinaendelea, vijana wanaenda shule na watumishi wa Serikali na watumishi wengine wanafanya shughuli zao za maendeleo. Ahsante.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:- Je, ni lini barabara ya Mvumi Mission itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Spika, nakushuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mtama, napenda kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa uamuzi wake wa kuamua kutupa watu wa Mtama Halmashauri yetu. Sasa je, Serikali iko tayari kumuunga mkono Mheshimiwa Rais kwa kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya kujenga barabara za Mji wa Mtama na kuzikarabati zile ambazo zimeharibiwa na mvua ili Mji wa Mtama sasa uwe na hadhi ya kubeba Halmashauri hii ambayo Mheshimiwa Rais ametupa? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nakushukuru na naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nape, Mbunge wa Mtama, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Nape na Halmashauri zingine zote kwamba Serikali ipo tayari kutenga fedha za kutosha kujenga barabara katika Makao Makuu ya Halmashauri mpya na zile za zamani, pia na kujenga majengo muhimu katika maeneo hayo ili huduma ziweze kutolewa kwa uhakika zaidi. Ahsante.