Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MGENI JADI KADIKA aliuliza:- Utandawazi umechangia sana vijana kupoteza maadili:- Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kwa vijana wetu kuwekewa umri maalum wa kutumia mitandao ili kupunguza mmomonyoko wa maadili?

Supplementary Question 1

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu yake lakini bado nina maswali mawili ya kumuuliza. Swali la kwanza; kwa kuwa vijana wengi au vijana wetu wadogo wanatumia mitandao kwa kutumia simu au ku-chart au kuangalia picha za ngono ambazo kuwa huleta hisia mbalimbali. Watoto hao ndiyo wale wanaobeba ujauzito wakiwa na umri mdogo kati ya darasa la sita mpaka darasa la tatu. Je, Serikali inaonaje suala hili?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; ziko nhi za wenzetu wanazuia mitandao kurusha picha za chafu. Je, Serikali yetu inashindwa nini baada ya kukemea na kudhibiti ili kuzuia mambo haya yasiendelee na wale watakaofanya hivyo wachukuliwe hatua? (Makofi)

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ambayo yameulizwa na Mheshimiwa Mgeni:-

Mheshimiwa Spika, nikianza na swali lake la kwanza ambalo ametaka kujua kwamba kwa upande wa Serikali tunaonaje masuala haya ya utandawazi. Ni kweli tunatambua kwamba, changamoto imekuwa kubwa sana kwa suala zima la maadili na kwa kiasi kikubwa sana inchangiwa na hii mitandao ya kijamii. Ndiyo maana kwa kujua hilo sasa sisi kama Serikali tulikuja na Sheria mbalimbali na Wabunge wa Bunge hili ndiyo ambao walizipitisha hizo Sheria, lengo ni kuhakikisha kwamba, tunawazuia watoto wetu hususan vijana ambao wako chini ya umri wa miaka 18 kuweza kujihusisha na vitu ambavyo havifai kwa Taifa letu. Kwa hiyo, kama ambavyo nimejibu kwenye jibu langu la msingi kwamba jukumu hili siyo jukumu la Serikali peke yake ni jukumu letu sote.

Mheshimiwa Spika, pia katika swali la pili, ametaka kujua kwamba nchi zingine zimefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kuweza kudhibiti vijana wadogo ambao wako chini ya miaka 18 kuangalia vitu ambavyo havifai kwenye mitandao. Bado jibu langu liko pale pale kwamba ni wajibu wetu sote, upande wa Serikali na naweza nikasema kwamba kwa upande wa Serikali tumefanya kazi kubwa sana na ziko sheria ambazo tayari tumeshazipitisha ndani ya hili Bunge, lakini changamoto zimekuwa kubwa kwamba sheria hizi zinapopita Waheshimiwa Wabunge tumekuwa na ile tabia ya kuwa na mgawanyiko.

Mheshimiwa Spika, unakuta sheria tumepitisha kwa mfano, Sheria ya Cybercrime, lakini sasa unakuta wengine wanaanza kulalamika kwamba ile sheria inaminya uhuru na inakandamiza, kitu ambacho kinakuwa siyo cha kweli. Kwa hiyo nitoe wito ndani ya hili Bunge kwamba sheria kama hizi zinapopita katika Bunge ni vyema sisi kama viongozi tukawa wa kwanza kuzisimamia, lakini vilevile kwa yale maeneo ambayo sisi tunatoka, tuhamasishe jamii kuona kwamba namna gani ambapo suala zima la malezi siyo suala la Serikali peke yake ni suala la Serikali lakini pamoja na jamii kwa ujumla. Ahsante.