Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Mradi wa umwagiliaji wa Karema ni wa muda mrefu toka umeanza:- Je, ni lini mradi huo utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, miradi mingi ya umwagiliaji imetumia fedha nyingi sana hapa nchini na miradi hiyo haijakamilika ukiwemo mradi wa Skimu ya Karema. Nilikuwa nataka kujua Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Skimu hiyo ya Karema?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, huu mradi umechukua takribani miaka 10 haujakamilika na kusababisha hasara kwa wakulima baada ya mifumo ya maji iliyotengenezwa kusababisha mafuriko makubwa kwenye maeneo ya uzalishaji. Serikali kupitia kwa Waziri je, yuko tayari kwenda pamoja kushuhudia ile miradi na kubomoa ule mradi ili uweze kuwasaidia Wananchi ambao kimsingi wanakula hasara?

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza anatambua kwamba, juhudi za Serikali ambazo tumezifanya tumetumia fedha nyingi sana katika miradi mingi ya umwagiliaji, ukiwepo huu wa Karema na fedha zote zilizohitajika tulipeleka, lakini tukiwa wakweli miongoni mwa miradi mingi ambayo pesa zake hazikutumika kwa mujibu wa malengo ya Serikali na kuwanufaisha wakulima ni pamoja na miradi ya umwagiliaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya Serikali kulitambua hilo nduo maana kwamba, kabla ya kuanza kupeleka pesa nyingine wala kuomba hapa kwenye Bunge lako utuidhinishie pesa nyingine nyingi zaidi tuliona kwanza tufanya tathmini ya kina, ili tubaini kasoro na tubaini ufanisi na changamoto ambazo tumezipitia kwenye miradi ile kabla ya kutenga fedha hizo. Na nimuarifu Mheshimiwa Kakoso kwamba, tathmini hiyo tumeshaimaliza na tumebaini mapungufu yalikuwa wapi na ni namna gani kwamba, tulifanya vizuri na vibaya; sasa ndio maana nimemuahidi kwamba, tutatenga fedha katika bajeti ijayo ya mwaka 2020/2021 baada ya kumaliza tathmini hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili anasema kwamba, kama Serikali niko tayari kuambatana naye kwenda katika mradi huu wa Karema, ili kwenda kuubomoa miundombinu, ili Wananchi hawa waweze kupata maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuko hapa kwa ajili ya kujenga, dhamira ya Serikali ilikuwa ni kusogeza na kuwaletea maendeleo Wananchi wale wa Karema, ili wawe na kilimo cha uhakika cha umwagiliaji na kuweza kulima zaidi ya mara mbilil kwa mwaka. Kwa hiyo, hatuko tayari kwenda kuiobomoa, ila niko tayari kuambana naye kwenda hapo Karema na timu yangu ya wataalam ili kwenda kuangalia kasoro hizo ili tuweze kutafuta ufumbuzi wa kuziboresha zaidi tuwaletee maendeleo Wananchi wa Karema.