Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Barabara ya Mlalo kupitia Ngwelo – Mlalo –Makanya- Mlingano mpaka Mashewa ni ya muda mrefu sana ipo chini ya halmashauri licha ya kwamba barabara hiyo ni kichocheo muhimu cha uchumi katika majimbo manne ya Lushoto, Mlalo, Bumbuli na Korogwe Vijiji. Je, ni lini Serikali itaipandisha hadhi barabara hiyo na kuwa chini ya TANROADS kutokana na umuhimu wake kiuchumi kwa wananchi wa majimbo hayo?

Supplementary Question 1

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza, barabara hii ya Mlalo, Ngwelo, Mlola, Makanya, Milingano mpaka Mashewa ambazo ni kilomita 53. 7 inapita kwenye halmashauri tatu na majibo manne. Na barabara ya kutoka dochi Ngulu hadi Mombo ambayo yenye kilometa 16.3 inapita kwenye halmashauri mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na isitoshe tumeandika barua ya kupandisha hadhi barabara hizi kabla ya kuanzishwa kwa TARURA lakini mpaka sasa hakuna kinachoendelea zaidi ya wananchi kuendelea tabu ya usafiri pamoja na mazao yao. Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka barabara hizi ziweze kushughulikiwa kwa haraka ili tukiendelea kusubiri upandishwaji wa hadhi wa barabara hizi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kwakuwa mheshimiwa Waziri wewe mwenyewe ni shahidi kwa kuona barabara hii ya dochi Nguli Mombo na kuongea na wananchi wa kijiji cha Nguli na ukawahidi kwamba changamoto hii utaimaliza. Je, upo tayari sasa kutuma wataalam wako kwenda kuona hali halisi ya barabara hiyo ili kuondoa kadhia wanayoendelea kuipata wananchi wa Nguli?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hizi anazotaja Mheshimiwa Mbunge ni kweli kwamba inapita katika maeneo mengi kwa maana jimbo lake la Lushoto, Jimbo la Mlalo, Jimbo la Bumbuli, na Korogwe vijijini na eneo hili ni muhimu sana kwa sababu inapitisha watali wengi kwenda kwenye hifadhi yetu ya Mkomazi lakini pia kuna uzalishaji mkubwa wa mazao na nilitembelea eneo hili nilishuhudia changamoto ambazo ziko kwenye barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa kujibu swali lake niseme tu mkakati wa kwanza mkubwa ni uanzishwaji wa TARURA na TARURA wamefanya kazi kubwa wa kuzitambua barabara zote nchini kwa lengo la kuhakikisha kwamba barabara zinapata bajeti au zinapata fedha kulingana na changamoto na hali ya barabara ilivyo kwa hiyo hii zoezi ilikuwa inafanyika na kazi ya TARURA ilipokamilika imepelekwa taarifa zimepelekwa kamati maalum ambayo inashirikisha wenzetu wa TAMISEMI wenzetu wa Wizara inayoshughulikia mambo ya utalii wenzetu wa Wizara ya ardhi kwa hiyo kamati muhimu hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu Mheshimiwa Mbunge anahitaji wataalam waende nimuelekeze tu Meneja wa TANROAD wa Mkoa wa Tanga na coordinator wa TARURA wa Mkoa wa Tanga watembelee barabara hizi mbili muhimu ili waweze kushauri kamati maalum tuone namna gani ya kuzifanyia matengenezo makubwa barabara hizi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba uvute subira nitafuatilia kuona wataalam wanatembelea eneo lako ili kuweza kuwezi hizi juhudi ambazo unazifanya Mheshimiwa Mbunge kuhakikisha kwamba wananchi wako wanapata huduma nzuri ya barabara katika maeneo haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nitaifuatilia na niwaombe hao kwa sababu ni wajumbe wa bodi ya barabara kwenye mkoa mapendekezo yatakayokuwa nayo pia wayazungumze katika bodi ya mkoa ili tuweze kuzitendea haki barabara hizi.

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Barabara ya Mlalo kupitia Ngwelo – Mlalo –Makanya- Mlingano mpaka Mashewa ni ya muda mrefu sana ipo chini ya halmashauri licha ya kwamba barabara hiyo ni kichocheo muhimu cha uchumi katika majimbo manne ya Lushoto, Mlalo, Bumbuli na Korogwe Vijiji. Je, ni lini Serikali itaipandisha hadhi barabara hiyo na kuwa chini ya TANROADS kutokana na umuhimu wake kiuchumi kwa wananchi wa majimbo hayo?

Supplementary Question 2

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza naomba nishukuru sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuweza kukamilisha daraja la Sibiti na hiyo ni kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Singida pamoja na Simiyu kwa thamani ya daraja lile nilikuwa naomba nimuulize mheshimiwa Naibu Waziri, ili tuweze kuwa na dhamani ya daraja lile ni ujenzi wa Barabara ya lami unaotoka Iguguno, Nduguti, kupita Sibiti, Meatu na kuendelea mpaka Bunda ili wananchi wale waweze kufanya shughuli za maendeleo. Je, ni lini Serikali itaanza Ujenzi huo kama ilivyoahidi? Ahsante.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Mlata kwa sababu umekuwa umefuatilia barabara zote za Mkoa wa Singida na ninafahamu hata sasa tuna ujenzi mkubwa mwingine unaendelea katika daraja la Msingi ili tuweze kuwaunganisha wananchi wa Wilaya ile ya Kiomboi na waweze kupita nao Sibiti. Kwa hiyo, tunaendelea na ujenzi na ujenzi unaendelea vizuri, lakini niseme tu kwamba mkakati mkubwa wa kuiboresha barabara hii ambayo ni muhimu sana itapunguza pia wasafiri wanaokwenda Arusha, wanaokwenda Manyara, wanaokuja Singida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kukamilika daraja lile tunajenga kiwango cha lami kilometa 25 ili eneo lote la bonde hili ambalo lilikuwa na changamoto kubwa wananchi waweze kupita vizuri ujenzi ule unaendelea kilomita 25.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tunakamilisha usanifu wa barabara hii muhimu ambayo inaunganisha mikoa ya Kanda ya Ziwa tukipita Sibiti tunakwenda Haydom tutakwenda Ndogobeshi, itakwenda hadi Mbulu itoke Karatu. Kwa hiyo, juhudi kubwa zinafanyika kuiboresha barabara hii muhimu na itawafanya wakazi wote wa Manyara wakazi wote wa Arusha waweze kupita barabara hii kwa sababu itapunguza zaidi kilomita mia mbili kwa mtu anayekwenda Mwanza, Simiyu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaendelea na kazi nzuri kubwa inafanyika, vuta subira na kwakweli ninashukuru sana kwa ushirikiano unaotoa Mheshimiwa Mbunge kwa kutupa information nyingi ili tuweze kuwaudumia wananchi wa Singida.