Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA (K.n.y. MHE. MARGARET S. SITTA) aliuliza:- (a) Je, Serikali ipo tayari kuangalia bajeti ya Hospitali ya Wilaya ya Urambo ambayo inahudumia wananchi wa maeneo ya Kaliua, Ulyankulu na maeneo ya jirani ili kuongeza uwezo wa kutoa huduma? (b) Hospitali ya Wilaya ya Urambo ina majengo mawili ya ICU na maabara ambayo hayajakamilika tangu yalipoanza kujengwa 2011 kupitia utaratibu wa LGDG ya mradi wa ADB. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu ombi la wananchi wa Urambo la shilingi milioni 200 ambazo zinaweza kumaliza majengo hayo? (c) e, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kuongeza wafanyakazi angalau Manesi 12 na Wafamasia 6 kutokana na kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa Hospitalini hapo?

Supplementary Question 1

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize maswali madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa jengo la ICU muhimu sana na kwa kuwa mradi ule mpaka sasa hauna fedha na Serikali imesema itatenga fedha mwaka huu wa fedha, je, Serikali iko tayari kupeleka angalau hizo milioni 200 za dharura?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa idadi ya watumishi ni ndogo sana hususan kitengo cha nursing, je, Serikali haioni sasa umuhimu wa kuongeza angalau watumishi sita katika Hospitali ya Wilaya?

Mheshimiwa Naibu Spika, mbali na maswali hayo, nipongeze sana majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwanne Mchemba, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Tabora, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Serikali, naomba tupokee pongezi ambazo Mheshimiwa amezitoa. Kipekee naomba na mimi nimpongeze kwa jinsi ambavyo amekuwa akipigania kuhakikisha afya na hasa ya akina mama inaboreshwa katika Mkoa wa Tabora.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la kwanza anaomba walau Serikali itoe jumla ya shilingi milioni 200 za dharura. Hata hivyo, katika majibu ya msingi na swali la msingi kinachoombwa ili kumalizia majengo yote mawili ni jumla ya shilingi milioni 200. Naomba Mheshimiwa Mbunge aendelee kuiamini Serikali, tumeahidi kwamba katika bajeti ya 2020/2021 tunaenda kutekeleza na hii inatokana na baadhi ya maboresho makubwa ambayo yamefanyika katika Hospitali ya Urambo ambapo sasa hivi hata makusanyo yanayokusanywa pale ni mengi. Naomba Mheshimiwa aendelee kuiamini Serikali, tutatekeleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili anaomba kuongeza idadi ya watumishi walau sita. Juzi Waziri mwenye dhamana amejibu akieleza namna ambavyo Serikali inaenda kutoa jira zisizopungua 45,000. Katika watumishi watakaoajiriwa upande wa afya, hakika nimhakikishie Mbunge na Tabora kwa ujumla wake hatutaisahau. (Makofi)

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA (K.n.y. MHE. MARGARET S. SITTA) aliuliza:- (a) Je, Serikali ipo tayari kuangalia bajeti ya Hospitali ya Wilaya ya Urambo ambayo inahudumia wananchi wa maeneo ya Kaliua, Ulyankulu na maeneo ya jirani ili kuongeza uwezo wa kutoa huduma? (b) Hospitali ya Wilaya ya Urambo ina majengo mawili ya ICU na maabara ambayo hayajakamilika tangu yalipoanza kujengwa 2011 kupitia utaratibu wa LGDG ya mradi wa ADB. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu ombi la wananchi wa Urambo la shilingi milioni 200 ambazo zinaweza kumaliza majengo hayo? (c) e, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kuongeza wafanyakazi angalau Manesi 12 na Wafamasia 6 kutokana na kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa Hospitalini hapo?

Supplementary Question 2

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi hii uliyonipa ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, tabu wanayopata wananchi wa Urambo, wanapata wananchi wangu wa Wilaya ya Mpwapwa, Jimbo la Kibakwe, Kata ya Mlunduzi ambayo ina zahanati tatu na zahanati hizi majengo yameshakamilika lakini milango, madirisha, ceiling board havijawekwa, kwa hiyo wanawake na watoto wanapata shida wakitafuta matibabu mbali na maeneo yao wakati majengo yako pale. Je, ni lini Serikali itakamilisha majengo yale ya zahanati ya Kata ya Mlunduzi, Jimbo la Kibwakwe ili wananchi wa pale waweze kupata huduma ya karibu?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Felister Bura, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Dodoma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama hicho anachosema Mheshimiwa Mbunge ndiyo uhalisia maana yeye mwenyewe anakiri kwamba almost ni kama majengo yamekamilika imebaki vitu vichache tu ili kukamilisha majengo hayo. Naomba nichukue fursa hii kumuagiza Mkurugenzi Mtendaji ahakikishe kwamba tathmini inafanyika kwa sababu katika hayo ambayo anayasema ni pesa kiasi kidogo sana kinahitajika ili kuweza kukamilisha zahanati hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nimtoe wasiwasi. Kama kuna mikoa yenye neema kwa sasa hivi ambayo watumishi wengi wa Serikali wanapenda kuhamia ni pamoja na Mkoa wa Dodoma. Kwa hiyo, adha ya ukosefu wa watumishi kwa Dodoma itabaki ni historia.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA (K.n.y. MHE. MARGARET S. SITTA) aliuliza:- (a) Je, Serikali ipo tayari kuangalia bajeti ya Hospitali ya Wilaya ya Urambo ambayo inahudumia wananchi wa maeneo ya Kaliua, Ulyankulu na maeneo ya jirani ili kuongeza uwezo wa kutoa huduma? (b) Hospitali ya Wilaya ya Urambo ina majengo mawili ya ICU na maabara ambayo hayajakamilika tangu yalipoanza kujengwa 2011 kupitia utaratibu wa LGDG ya mradi wa ADB. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu ombi la wananchi wa Urambo la shilingi milioni 200 ambazo zinaweza kumaliza majengo hayo? (c) e, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kuongeza wafanyakazi angalau Manesi 12 na Wafamasia 6 kutokana na kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa Hospitalini hapo?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Adha iliyopo Urambo ya Hospitali ya Wilaya kuhudumia population nje ya eneo linalohitajika ni sawa na ile ya Hospitali ya Mji wa Tarime ambayo kwa kweli na nimeshaongea mara nyingi sana hapa Bungeni, inahudumia watu nje ya population ya Mji wa Tarime, wanatoka Shirati, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na Serengeti.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Kata ya Kinyemanyoli waliamua kujenga kituo cha afya ili kupunguza ile population ambayo inaenda kupata huduma ya Halmashauri ya Mji wa Tarime na nilishauliza hapa akaahidi kwamba angeweza kupeleka fedha. Nataka kujua sasa ni lini Serikali itapeleka fedha ku-support nguvu za wananchi ili tuweze kuwa na kituo cha afya Kinyemanyoli kupunguza adha wanayopata wajawazito na watoto?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri kwa maswali yaliyoulizwa hapo awali.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu Mkoa wa Mara umekuwa na changamoto mbalimbali za sekta ya afya lakini tumefanya investment kubwa katika mkoa huo na tukifahamu kwamba eneo la Tarime Mji napo kuna changamoto hizo. Ni jukumu la Serikali kuangalia nini kifanyike katika maeneo hayo kama tulivyofanya kazi katika Mkoa mzima wa Mara. Kwa mfano, kwa sasa hivi tunajenga Hospitali za Wilaya takriban tatu na kuimarisha vituo vya afya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Esther Matiko kwamba tunaifahamu changamoto zilizopo kule na tunazishughulikia. Kikubwa zaidi naomba nimuagize Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara kwenda kufanya tathmini na kutuletea taarifa ili katika mchakato wetu wa bajeti unaokuja mwezi wa tano tuangalie jinsi gani tutaweza ku-address matatizo ya maeneo hayo kwa sababu lengo letu kubwa ni kuhakikisha kwamba wananchi wa Tarime Mji wanapata huduma vizuri. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA (K.n.y. MHE. MARGARET S. SITTA) aliuliza:- (a) Je, Serikali ipo tayari kuangalia bajeti ya Hospitali ya Wilaya ya Urambo ambayo inahudumia wananchi wa maeneo ya Kaliua, Ulyankulu na maeneo ya jirani ili kuongeza uwezo wa kutoa huduma? (b) Hospitali ya Wilaya ya Urambo ina majengo mawili ya ICU na maabara ambayo hayajakamilika tangu yalipoanza kujengwa 2011 kupitia utaratibu wa LGDG ya mradi wa ADB. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu ombi la wananchi wa Urambo la shilingi milioni 200 ambazo zinaweza kumaliza majengo hayo? (c) e, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kuongeza wafanyakazi angalau Manesi 12 na Wafamasia 6 kutokana na kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa Hospitalini hapo?

Supplementary Question 4

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Hospitali ya Mji wa Kondoa inahudumia takriban Halmashauri sita. Tunazungumzia Kondoa Vijijini, Chemba, Kiteto, wakati mwingine mpaka Hanang’ na Babati. Bajeti tunayopata ni shilingi milioni 45 kati ya milioni 160 ambayo tunahitaji kutoka Basket Fund. Nimelizungumzia sana suala hili Bungeni hapa.

Je, ni lini sasa Serikali itakubaliana na uhalisia wa mahitaji hayo na kutuongezea bajeti yetu kukidhi mahitaji ya wananchi wa maeneo hayo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sannda, Mbunge wa Kondoa Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, tuna changamoto katika maeneo ya miji ukiachia ile Halmashauri ya Mji wa Kondoa lakini kwa dada yangu Mheshimiwa Esther Matiko pale Tarime na hali kadhalika kwa Mheshimiwa Chumi pale Mafinga. Ndiyo maana tumewaagiza wataalam wetu sasa hivi wanafanya analysis kuangalia changamoto kubwa ya idadi ya watu na mgawanyo wa fedha ili tuweze ku-regulate vizuri ili mradi maeneo hayo yaweze kupata huduma vizuri. Kwa hiyo, naomba tuwe na subira kidogo, wataalam wetu wanafanya kazi hiyo, naamini katika Mpango wa Bajeti yetu ya mwaka wa fedha 2020/2021 jambo hilo tutali-address vizuri kwa maslahi mapana ya wananchi wetu.