Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE (K.n.y. MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) aliuliza:- Utalii wa uwindaji, utalii wa picha na ufugaji wa mapori ya misitu na Hifadhi ya Ugunda, Isuvangala na Ipembampazi ni miongoni mwa fursa kuu za utalii kwenye Jimbo la Sikonge:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Uwanja wa Ndege uliokuwa umeanza kujengwa karibu na Mlima wa Ipole ambao ulijumuisha pia ujenzi wa nyumba za kufikia watalii (tourist rest houses) kwenye Kijiji cha Ugunda?

Supplementary Question 1

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya kitaalam kuhusu uUwanja wa Ndege wa Ipole nilitaka kujua sasa, je, lini uwanja unaopendekezwa katika mapori ya Ugala utamalizika?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia nina swali la pili, Serikali ina mpango gani wa kuyatangaza maeneo ya Kwihara pamoja na yaliyokuwa makazi ya Marehemu Mirambo kwa ajili ya utalii? Ahsate sana.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Almas, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba kumpongeza Mheshimwia Almasi pamoja na kwamba ameuliza kwa niaba ya Mheshimiwa Joseph Kakunda, pia amekuwa ni mshauri mzuri na mdau mzuri sana wa mambo ya utalii. Kama nilivyojibu kwenye jibu letu la msingi ni kwamba tulisitisha ujenzi wa Uwanja wa Ndege ya Ipole kutokana na ushauri wa kitaalam tuliopata kutoka Wizara ya Mawasiliano. Tulielekeza Wilaya kuangalia eneo lingine ambalo linafaa kwa ajili ya ujenzi. Kwa bahari mbaya eneo lote linalozunguka maeneo hayo ni ardhi oevu na ni eneo ambalo ni chepechepe yaani wetland na imekuwa vigumu kupata eneo ambalo tunaweza tukajenga uwanja kwa sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika Hifadhi mpya ya Ugala tunavyo viwanja viwili vidogo vya ndege, kiwanja cha Siri na kiwanja cha Muhuba ambavyo vipo kama takribani kilometa 100 kutoka uwanja wa Ipole ulipokuwa. Kwa sasa Wizara yetu imebadilisha hadhi ya Pori la Akiba la Ugala na kuwa Hifadhi ya Taifa, tumeelekeza TANAPA kuboresha viwanja hivyo ili viweze kutumika wakati wote kwa huduma ambazo zilikuwa zimekusudiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili ni mpango wa kuyatangaza makazi au maeneo ya kale ya Mtemi Mirambo. Kama tulivyofanya nchi nzima tumeelekeza maeneo mengi ya mali kale kuchukuliwa na Taasisi zetu zote zinazofanya utalii nchini. Eneo hili la Mirambo kama tulivyofanya kule Iringa tutawaelekeza TANAPA kuwekeza pale utaalam na nguvu ili kuhakikisha kwamba tunayahusisha katika product ya utalii kuwawezesha watalii wanaotua Tabora na maeneo mengine ya Mkoa wa Tabora kuyafahamu maeneo haya ya historia.

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE (K.n.y. MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) aliuliza:- Utalii wa uwindaji, utalii wa picha na ufugaji wa mapori ya misitu na Hifadhi ya Ugunda, Isuvangala na Ipembampazi ni miongoni mwa fursa kuu za utalii kwenye Jimbo la Sikonge:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Uwanja wa Ndege uliokuwa umeanza kujengwa karibu na Mlima wa Ipole ambao ulijumuisha pia ujenzi wa nyumba za kufikia watalii (tourist rest houses) kwenye Kijiji cha Ugunda?

Supplementary Question 2

MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa wananchi wa Vijiji vya Myesi, Utimbe, Naliongolo na maeneo ya Mchoti wamekuwa wakipoteza maisha, pia kujeruhiwa kutokana na wingi wa mamba waliopo katika Mto Ruvuma. Serikali kupitia Bunge Tukufu ilishawagiza TAWA ili waende kuchimba visima kuwaokoa wananchi hawa kutokana na kutegemea Mto Ruvuma kwa matumizi ya maji yao. Je, Serikali inatoa tamko gani kuwaelekeza TAWA waende wachimbe visima hivyo haraka iwezekanavyo?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA WALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwanausi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikiri kwamba itakuwa swali la tatu la aina hiyo nalijibu lenye uhusiano na wingi wa mamba kwenye maeneo mbalimbali ya Mto Ruvuma. Ni kweli kwamba kuna ongezeko la wanyama wa aina mbalimbali wakiwemo mamba na wamekuwa wakiathiri matumizi ya asili ya wananchi ya maji ya Mto Ruvuma.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuliekeleza hapa kwamba katika ushauri tuliopata kutoka kwa wanasayansi wa Wizara yetu ni kwamba maeneo ambayo wananchi wanatumia yanaweza kuwekewa kingo maalum ili kuzuia mamba kufika na ushauri wa pili ilikuwa ni kuchimba visima kandokando ya eneo hilo. Kwa kushirikiana na Wizara husika, Wizara yangu ilizungumza na watu wa Wizara ya Maji na waliahidi kupeleka visima maeneo hayo. Naomba nichukue ushauri wa Spika kuwaekeleza tena TAWA kufanya tathmini na kupitia na kuona kama TAWA tunaweza tukafanya kazi ingawa kazi ya msingi kabisa ya kupeleka maji maeneo hayo itafanywa na Wizara ya Maji.