Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. JEROME D. BWANAUSI aliuliza:- Wananchi wa Mipande – Mtengula na Mwitika Maparawe wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa madaraja na Rais wa Awamu ya Tano aliwaahidi Wananchi hao kuwajengea madaraja:- Je, ni lini ahadi hiyo ya Mheshimiwa Rais itatekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri lakini kwa kuwa wananchi hawa wa maeneo ya Mipande na Mtegula, lakini pamoja na Mwitika - Maparawe, wamekuwa wanapata adha kubwa sana kutokana na kukosekana kwa madaraja haya makubwa; na kwa kuwa Mheshimiwa Rais alishahaidi kuyashughulikia madaraja haya, naomba Serikali itoe kauli ni lini madaraja haya ya Mtengula - Mipande na Mwitika - Maparawe yatajengwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kwa kuwa madaraja haya ambayo Mheshimiwa Rais aliahidi jumla ni manne na tayari daraja la Shaurimoyo na Nanjocha yalishajengwa kwa kutumia TANROADS. Je, Serikali haioni umuhimu TANROADS kumaliza madaraja haya mawili yaliyobaki? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la kaka yangu Mheshimiwa Jerome Dismas Bwanausi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli madaraja haya yamekuwa na kadhia kubwa sana na nikiri wazi Mheshimiwa Bwanaus alikuja pale mpaka nikamkabidhi kwa Mkurugenzi wetu wa TARURA Bwana Seif wakaweza kuongea vya kutosha na ndiyo imewezesha sasa hivi usanifu unafanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kutokana na shida iliyo pale na hili ni agizo la Mheshimiwa Rais na Serikali imeshakamilisha kile kipande kingine cha madaraja, jukumu kubwa sasa ni kwamba usanifu huu utakapokamilika tutaangalia ni wapi fedha zitapatikana. Mimi na kaka yangu Kamwelwe tunashirikiana kwa karibu zaidi na baada ya usanifu tutashirikiana kuona jinsi gani tutafanya ikiwezekana wenzetu wa TANROADS waweze kusaidia katika eneo lile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Lulindi kwamba kama Mheshimiwa Rais alivyoelekeza madaraja haya yatajengwa ili wananchi hawa wanaopata shida kwa kipindi kirefu waweze kuondokana na adha hii inayowakabili.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. JEROME D. BWANAUSI aliuliza:- Wananchi wa Mipande – Mtengula na Mwitika Maparawe wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa madaraja na Rais wa Awamu ya Tano aliwaahidi Wananchi hao kuwajengea madaraja:- Je, ni lini ahadi hiyo ya Mheshimiwa Rais itatekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa madaraja katika maeneo mengi nchini ikiwemo Jimbo la Mbulu Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Daraja la Gunyoda katika Jimbo la Mbulu Mjini linahitaji zaidi ya shilingi milioni 700 na hadi sasa ni mwaka wa nane (8) Serikali ikiombwa kujengwa daraja hilo. Je, Serikali haioni umuhimu mkubwa wa kuja na mpango mkakati kupitia TARURA na TANROADS ili kuainisha baadhi ya madaraja ambayo yanakwamisha huduma za jamii ili kuweza kutatua tatizo hili kwa nchi nzima?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la kaka yangu Mheshimiwa Zacharia Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikiri wazi kwamba Mheshimiwa Issaay tumeshafika Jimboni kwake takribani mara kadhaa na mwezi mmoja na nusu uliopita nilikuwa kule na kweli wana changamoto hizo. Nadhani kwa juhudi yake aliyoifanya na mwenzake kule Mheshimiwa Flatei walikuwa na changamoto kubwa la Daraja la Magara ambapo leo hii Serikali imeshasikia na kuweza kujenga lile daraja la Magara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii maana yake ni nini? Ni mpango wa Serikali maeneo yote yenye vikwazo aidha kupitia TARURA au kupitia TANROADS kuondoa changamoto zilizopo na mpaka sasa kazi kubwa imefanyika maeneo mbalimbali. Nimtoe hofu Mheshimiwa Zacharia ni mpango wa Serikali kupitia TARURA na TANROADS kuhakikisha tunaondoa vikwazo kwa wananchi ambao wanashindwa kusafiri katika maeneo hayo.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JEROME D. BWANAUSI aliuliza:- Wananchi wa Mipande – Mtengula na Mwitika Maparawe wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa madaraja na Rais wa Awamu ya Tano aliwaahidi Wananchi hao kuwajengea madaraja:- Je, ni lini ahadi hiyo ya Mheshimiwa Rais itatekelezwa?

Supplementary Question 3

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tatizo la daraja linawakumba pia wananchi wa Mbagala – Nzasa – Kilungule
- Mwanagati - Buza. Eneo hilo maji yanapojaa katika Mto Mzinga wananchi wanashindwa kuvuka na hata watoto wanashindwa kwenda shuleni mpaka wananchi wamejijengea daraja lao la miti. Je, Serikali lini itajenga daraja hilo ili kuwasaidia wananchi hao?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la mama yangu Mheshimiwa Kisangi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, ukiangalia maeneo ya Mbagala yote yalikuwa na changamoto kubwa sana na ndiyo maana Serikali tumeanza awamu kwa awamu. Mheshimiwa Kisangi unakumbuka kulikuwa na changamoto kubwa kati watu wa Mbagala Kuu na Kibada kupitia Twangoma. Serikali imekalisha ujenzi wa daraja kubwa maeneo yale kwa mabilioni ya fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, nafahamu changamoto iliyopo katika Mto Mzinga na mimi mwenyewe nimeshatumia barabara ile kwa kutumia pikipiki mara kadhaa, nalifahamu eneo hilo. Nimhakikishie kwamba ni jukumu la Serikali eneo lote la Jiji la Dar es Salam miundombinu ambayo ilikuwa ina changamoto kubwa kupitia mpango wa awamu kwa awamu maeneo yote tutaweza kuyaunganisha ili wananchi waweze kusafiri kutoka eneo moja mpaka eneo lingine.

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. JEROME D. BWANAUSI aliuliza:- Wananchi wa Mipande – Mtengula na Mwitika Maparawe wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa madaraja na Rais wa Awamu ya Tano aliwaahidi Wananchi hao kuwajengea madaraja:- Je, ni lini ahadi hiyo ya Mheshimiwa Rais itatekelezwa?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba niulize swali, barabara ya kutoka Igunga - Itumba - Loya madaraja yake pamoja na barabara yenyewe imeharibika sana na ilipata fedha kwenye bajeti iliyopita lakini mchakato wa kumpata mkandarasi umechukua muda mrefu sana. Nimeongea na TARURA hata Makao Makuu bado sasa ni miezi sita. Je, ni lini barabara hii itakarabatiwa kwa sababu fedha ipo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la kaka yangu Mheshimiwa Dalaly Peter Kafumu, Mbunge wa Igunga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tuseme kwamba kulikuwa na changamoto kwako na Nzega kule kwa Mheshimiwa Bashe, tumepeleka hela kwa pamoja daraja kule kwa Mheshimiwa Bashe limekamilika lakini kwako Mheshimiwa Dalaly bado kuna changamoto kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kueleza maneno mafupi, nimuagize Mtendaji Mkuu wa TARURA, Bwana Victor Seif ahakikishe kwamba ndani ya mwezi mmoja nipate matokeo nini kinafanyika eneo hilo kwa sababu fedha zipo hatuna sababu ya kuchelewa. Kwa hiyo Mheshimiwa Kafumu haya ni maelekezo yangu ndani ya mwezi mmoja nipate status ya ujenzi huo na ndiyo maana namuagiza Mtendaji wangu Mkuu wa TARURA afuatilie eneo hilo.