Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA aliuliza:- Mradi wa Maji unaotekelezwa chini ya Programu ya WSDP katika Vijiji vya Malinyi, Kipingo na Makerere unasuasua sana toka 2015 hadi sasa mradi huo haujakamilika:- (a) Je, ni lini mradi huo utakamilishwa ili kuwawezesha wakazi wapatao 18,000 wa vijiji hivyo kupata maji safi na salama? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapelekea maji wakazi wa Vijiji vya Miembeni, Mchangani na Misegese Kata ya Malinyi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza wana-Malinyi tunampongeza Mheshimiwa Waziri wa Maji, mwezi wa Nane alikuja Wilayani akaahidi kutatua matatizo ya maji katika Wilaya ya Malinyi ndani ya miezi miwili na nusu. Mheshimiwa Waziri ahadi hiyo mpaka leo haijatimizwa.

Swali la kwanza, katika Kijiji cha Igawa mradi wa Bonde la Mto Rufiji wamechimba kisima kwa njia ya utafiti, lakini kisima hicho wamekitelekeza. Halmashauri Wilaya ya Malinyi tumeomba zaidi ya mara mbili kibali cha kutumia kisima hiki ili tutengeneze miundombinu kusambaza maji, kutatua kero ya maji kwa wananchi wa Kata ya Gawa. Sasa Serikali inasema nini juu ya kuomba kibali hicho cha kutumia kile kisima walichochimba Rufiji Basin?

Swali la pili, pia Mheshimiwa Waziri aliahidi Tarafa ya Mtimbila; Kata ya Mtimbila yenye vijiji saba ipate maji ya mtiririko. Maji yale hayatoshelezi na kuna mpango pale wa kuboresha ule mradi na Mkandarasi ameteuliwa lakini mpaka leo hajafanya chochote. Vile vile Mheshimiwa Waziri aliahidi kwamba ndani ya miezi miwili na nusu atamwondoa Mkandarasi, atafanya utaratibu wa force account ili mradi ule ukamilike. Nini kauli ya Waziri kwenye ahadi hiyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji
wake, lakini kikubwa tunatambua maji ni uhai na sisi kama Viongozi wa Wizara ya Maji hatupo tayari kupoteza uhai wa Wana-Malinyi. Kubwa namwomba Mheshimiwa Mbunge kutokana na concern yake na jitihada kubwa ambazo zinafanyika pale kuwasimamia wale Wakandarasi, tukutane leo saa 7.00 ili tuweze kutoa uamuzi wa haraka ili wananchi wake waweze kupata huduma ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA aliuliza:- Mradi wa Maji unaotekelezwa chini ya Programu ya WSDP katika Vijiji vya Malinyi, Kipingo na Makerere unasuasua sana toka 2015 hadi sasa mradi huo haujakamilika:- (a) Je, ni lini mradi huo utakamilishwa ili kuwawezesha wakazi wapatao 18,000 wa vijiji hivyo kupata maji safi na salama? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapelekea maji wakazi wa Vijiji vya Miembeni, Mchangani na Misegese Kata ya Malinyi?

Supplementary Question 2

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara kwa zaidi ya miaka mitatu imeshindwa kuongeza hata asilimia tatu ya upatikanaji wa maji pamoja na Serikali kuleta pesa nyingi na ipo miradi ya Mayaya na Liyo ambayo kwa zaidi ya miaka mitano haijakamilika:-

Je, Serikali ipo tayari kuunda Tume na kufuatilia kujua kwenye wilaya hiyo kuna tatizo gani ambalo linashinda kutekeleza miradi ya maji? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kubwa ambalo nilishukuru sana Bunge lako Tukufu kwa kutupitishia Sheria (Na. 5) ambayo imetupa nafasi sisi kama Wizara ya Maji na rungu la kuwawajibisha Wakandarasi lakini hata kuwawajibisha Wahandisi wetu wa maji. Ninachotaka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tumeshaunda kikosi kazi katika kila mkoa. Labda niagize kikosi kazi hicho kihakikishe kwamba kinafika katika Halmashauri ya Mtwara Vijijini katika kuhakikisha inatatua tatizo la maji, nami nitafanya ufuatiliaji wa kufika mwenyewe.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA aliuliza:- Mradi wa Maji unaotekelezwa chini ya Programu ya WSDP katika Vijiji vya Malinyi, Kipingo na Makerere unasuasua sana toka 2015 hadi sasa mradi huo haujakamilika:- (a) Je, ni lini mradi huo utakamilishwa ili kuwawezesha wakazi wapatao 18,000 wa vijiji hivyo kupata maji safi na salama? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapelekea maji wakazi wa Vijiji vya Miembeni, Mchangani na Misegese Kata ya Malinyi?

Supplementary Question 3

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniruhusu nami niulize swali la nyongeza katika swali la 79 linalohusu maji. Naishukuru sana Serikali yangu, imetuletea maji kutoka Ziwa Victoria na inachukua kata 10 za Jimbo langu, lakini kuna kata zinazobaki zaidi ya nane hazipati maji:-

Je, Serikali ina mpango gani kupeleka maji kwenye kata ambazo hazipati maji ya mradi wa Ziwa Victoria?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge na nimeshafika pale Uyui, lakini ninachotaka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge, Serikali imefanya jitihada kubwa sana zaidi ya shilingi bilioni 600 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi mkubwa utakapofika katika Jimbo lake la Uyui.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kubwa naaka nimhakikishie maji yatafika Uyui na maeneo ambayo hayana maji tutahakikisha yale maji yaweze kufika na wananchi wake waweze kupata huduma ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA aliuliza:- Mradi wa Maji unaotekelezwa chini ya Programu ya WSDP katika Vijiji vya Malinyi, Kipingo na Makerere unasuasua sana toka 2015 hadi sasa mradi huo haujakamilika:- (a) Je, ni lini mradi huo utakamilishwa ili kuwawezesha wakazi wapatao 18,000 wa vijiji hivyo kupata maji safi na salama? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapelekea maji wakazi wa Vijiji vya Miembeni, Mchangani na Misegese Kata ya Malinyi?

Supplementary Question 4

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Miradi ya maji mitano iliyojengwa chini ya mpango wa WSDP katika Wilaya ya Karatu, Kijiji cha Buger, Kansay, Getamok bado haifanyi kazi kwa ajili ya kujengwa chini ya kiwango:-

Ni lini Serikali itawawajibisha Wakandarasi hao ili wananchi wapate huduma stahiki?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kwa ufupi sana, hatuna sababu tena ya kumwona Rais wetu anasononeka au Waheshimiwa Wabunge wanasononeka, mmeshatupa rungu. Ninachotaka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge, baada ya Bunge nitafika Karatu kwa wale wote waliohujumu miradi ya maji, tutawachukulia hatua na kama fedha, watazitapika. Ahsante.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA aliuliza:- Mradi wa Maji unaotekelezwa chini ya Programu ya WSDP katika Vijiji vya Malinyi, Kipingo na Makerere unasuasua sana toka 2015 hadi sasa mradi huo haujakamilika:- (a) Je, ni lini mradi huo utakamilishwa ili kuwawezesha wakazi wapatao 18,000 wa vijiji hivyo kupata maji safi na salama? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapelekea maji wakazi wa Vijiji vya Miembeni, Mchangani na Misegese Kata ya Malinyi?

Supplementary Question 5

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Naibu Waziri alifanya ziara Vilayani Nyang’hwale mwezi wa Nne na kumpeleka kwenye mradi mkubwa wa maji kutoka Nyamtukuza, Kaluma, Bukwimba na kujionea hali halisi ya Wakandarasi wetu wanavyosuasua kuutekeleza mradi huo; na kwa kuwa aliwaita Wakandarasi Wizarani, tulikuja tukakaa nao pamoja; na Mkandarasi anayeitwa Pety, alielezea tatizo la kwamba amecheleweshewa fedha kwa ajili ya kuagizia pump nje:-

Je, Serikali inatoa tamko gani kukamilisha mradi huu kwa haraka iwezekanavyo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Nyang’hwale kwa kazi kubwa ambayo anaifanya. Moja ya changamoto kubwa sana ya Sekta yetu ya Maji ilikuwa eneo la maji vijijini. Nilifika Nyang’hwale tukaona Mkandarasi akifanya kazi kwa kusuasua, baadhi ya kazi tulimnyang’anya tukaomba wataalam wetu wa ndani na anaona kasi inavyofanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kusema, tutalifanya hili jambo la haraka. Ile kazi ya kununua pump kama itakuwa imemshinda, tutainunua sisi Serikali ili wananchi wako waweze kupata huduma ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA aliuliza:- Mradi wa Maji unaotekelezwa chini ya Programu ya WSDP katika Vijiji vya Malinyi, Kipingo na Makerere unasuasua sana toka 2015 hadi sasa mradi huo haujakamilika:- (a) Je, ni lini mradi huo utakamilishwa ili kuwawezesha wakazi wapatao 18,000 wa vijiji hivyo kupata maji safi na salama? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapelekea maji wakazi wa Vijiji vya Miembeni, Mchangani na Misegese Kata ya Malinyi?

Supplementary Question 6

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo la maji. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri Mkuu alipofanya ziara katika mkoa wetu wa Iringa aliweka jiwe la msingi katika mradi mkubwa sana wa maji katika Mji Mdogo wa Ilula:-

Je, ni lini sasa mradi ule utaanza kufanya kazi ili wananchi wa Iringa waweze kutuliwa ndoo kichwani?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, anatosha sana mama yangu kwa kuwapigania…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri!

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa ambacho nataka kusema, utekelezaji wa miradi ya maji unategemeana na fedha, mkandarasi ame-raise certificate kwa ajili ya kumlipa. Tutamlipa kwa wakati.

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA aliuliza:- Mradi wa Maji unaotekelezwa chini ya Programu ya WSDP katika Vijiji vya Malinyi, Kipingo na Makerere unasuasua sana toka 2015 hadi sasa mradi huo haujakamilika:- (a) Je, ni lini mradi huo utakamilishwa ili kuwawezesha wakazi wapatao 18,000 wa vijiji hivyo kupata maji safi na salama? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapelekea maji wakazi wa Vijiji vya Miembeni, Mchangani na Misegese Kata ya Malinyi?

Supplementary Question 7

MHE. RHODA E. KUMCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Changamoto ya ukosefu wa maji katika Manispaa ya Mpanda pia nayo ni tatizo kubwa. Kata ya Mwamkulu, Kasokola, Kakese pamoja na Makanyagio ni Kata ambazo zina uhaba wa maji na upungufu wa maji. Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari kuhakikisha miradi ya maji pamoja na visima vilivyopo katika maeneo hayo vinatoa maji yenye uhakika ambayo yatawatosheleza wakazi wa Kata hizo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Waziri alishafika Mpanda na tumeunda timu maalum kwa ajili ya kutatua tatizo la maji. Kwa hiyo, ipo kazi inayofanyika katika eneo la Mpanda katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji.