Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL aliuliza:- Halmashauri ya Manispaa ya Moshi kwa muda mrefu imekuwa na maombi ya kupandishwa hadhi kwa Zahanati za Msarango, Longuo B na Shirimatunda kuwa Vituo vya Afya:- Je, ni lini Zahanati hizo zitapandishwa hadhi kuwa Vituo vya Afya?

Supplementary Question 1

MHE. RAPHAEL H. MICHAEL: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri ya Kikanuni, lakini kutokana na jiografia ya Manispaa ya Moshi, Kata ya Msaranga, Ng’ambo na Kibororoni zipo karibu na wananchi hawa wanashirikiana pamoja katika kutafuta huduma za afya. Sasa je, Serikali kwa maelekezo hayo kwamba wanahamasisha kujenga vituo vya afya, ni lini itatupatia fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya katika Kata hiyo ya Msaranga ili tuweze kusaidia hizo Kata tatu kwa pamoja ili wananchi wapate huduma za afya?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Manispaa ya Moshi tuna ombi la muda mrefu kwa Serikali kuhusiana na Hospitali ya Wilaya na kuna uhitaji mkubwa sana ili kusaidia wagonjwa ambao wamezidi Hospitali ya KCMC na Hospitali ya Mawenzi. Je, ni lini sasa ombi letu litakubaliwa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya Wilaya?

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, katika swali lake la kwanza anaongelea Kata mbili ambazo ziko tayari kushirikiana ili waweze kupata Kituo cha Afya. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, sisi kama Serikali tuko tayari pale ambapo wazo limeanzia kwa wananchi na eneo linakuwepo na utayari wa wananchi katika kujenga Kituo cha Afya, nasi kama Serikali tunapeleka nguvu yetu.

Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili anaongelea juu ya suala zima la ujenzi wa Hospitali ya Wilaya kwa ajili ya Manispaa ya Moshi. Katika jibu langu la msingi nimemwambia Mheshimiwa Mbunge kwamba nia ya Serikali ni kuhakikisha kwamba huduma kwa ajili ya sehemu ambazo hakuna Hospitali ya Wilaya zinapatikana na ndiyo maana sisi kama Serikali kwa kushirikiana na St. Joseph tumewapa hadhi ya kuwa kama Hospitali ya Wilaya kwa ajili ya kutoa huduma hiyo, lakini itekelezwe kwa muda wa mpito pale ambapo Hospitali ya Wilaya haipo.

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba sisi kama Serikali tuko tayari kama ambavyo tumeanza maeneo mengine, tutahakikisha kwamba hata Manispaa ya Moshi nayo inapata Hospitali ya Wilaya.