Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Ali Abbas Mangungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ISSA A. MANGUNGU aliuliza:- Tangu TRA ianze kukusanya kodi ya majengo imekusanya kiasi gani katika Mkoa wa Kodi Temeke kwa mwaka 2017/2018 na ni asilimia ngapi ya lengo?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Spika, nashukuru, lakini ningemuomba Mheshimiwa Waziri kama atakubali ombi langu la kuongozana na mimi ili akaangalie jinsi gani wananchi wanavyokadiriwa makadirio ya juu yasiyokuwa na haki na kuwapa usumbufu mkubwa hasa wale ambao wanaishi katika maeneo ambayo hayajapimwa.

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; je, ni lini Serikali itaifanya sasa Wilaya ya Mbagala kuwa mkoa wa kikodi ili waweze kukusanya vizuri kodi katika maeneo yasiyopimwa, yameachwa kwa asilimia nyingi sana na wanashindwa
kufikia huko kwa sababu TRA hawana man power ya kutosha? Kama hawawezi basi warudishe kwenye halmashauri zetu ili waendelee na zoezi hili.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la kwanza, wananchi kukadiriwa gharama kubwa kwa ajili ya kulipa kodi ya majengo. Naomba niwaambie wananchi wa Tanzania kwamba dhamira njema ya Serikali ya Chama cha Mapinduzi inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli ya kuhakikisha Watanzania hawaumizwi tena na kodi hizi tayari Bunge hili lilishapitisha sheria.

Mheshimiwa Spika, sasa kila jengo ambalo ni la chini ni shilingi 10,000 kwa hiyo hakuna anayelipa zaidi ya 10,000 kwa kila jengo ambalo ni la chini na kwa majengo ya ghorofa kwa kila ghorofa moja naomba niwaambie Watanzania kwa kila floor ya ghorofa lako ni shilingi 50,000 kwa hiyo hakuna makadirio yoyote ambayo yako juu na Mheshimiwa kaka yangu Issa Ali Mangungu niko tayari kwenda na wewe Mbagala tukaongee na wananchi wetu tuwaeleweshe nini dhamira ya Serikali yao na nini tumeanza kutekeleza.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili; hili ni jambo la kiutaratibu, naomba nilichukue tutakwenda kulifanyia kazi ili tuone ni lini sasa Wilaya ya Mbagala inaweza kuwa sasa ni Mkoa wa Kikodi ili tuweze kushughulikia ukusanyaji wa kodi hii kwa ufanisi.