Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:- ATM za Benki nyingi hapa nchini hazikidhi mahitaji ya watu wenye ulemavu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa ATM za Benki zinawekewa mifumo inayokidhi mahitaji ya watu wenye ulemavu?

Supplementary Question 1

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa unyenyekevu mkubwa ninakupongeza wewe, na nichukue nafasi hii kukupongeza kwa kuwa mfano bora kutokana na miundombinu ya taasisi unayoingoza, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa rafiki, kila sehemu unapokwenda kwa kweli imejali mahitaji ya watu wenye ulemavu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa moyo wa dhati ninakupongeza na ninaomba taasisi nyingine waige mfano katika Bunge ambapo miundombinu kwa watu wenye ulemavu imezingatiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niulize maswali yangu mawili ya nyongeza. Nashukuru kwa majibu mazuri kwa Naibu Waziri na kwa Serikali pia. Kama alivyosema kwamba Serikali itaendelea kufuatilia kwa karibu suala hili, ninapenda kufahamu sasa ni lini basi utekelezaji wake utakamilika?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; baadhi ya benki hapa nchini pamoja na kwamba zimejali mahitaji ya watu maalum, hasa walemavu wa viungo, lakini bado ramps zilizojengwa zina mteremko mkali ambao ni hatari zaidi kwa watu wenye ulemavu. Je, ni hatua gani sasa zinachukuliwa na Serikali kuhakikisha kwamba, ikiwa ni pamoja na kutoa maagizo kwa wafanyakazi au wahudumu wa benki kuwahudumia watu wenye ulemavu kwa kuwafuata nje na kuwapa huduma hiyo pale wanapofika katika benki hizo?

Mheshimiwa Spika, nakushukuru, ahsante.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza ameuliza ni lini basi utekelezaji utakamilika. Kama ambavyo nimesema kwenye jibu langu la msingi, Serikali tunaendelea kufuatilia na nimeeleza wazi kwamba miundombinu hii ina gharama kubwa, hasa hii yenye nuktanundu kwa ajili ya ndugu zetu ambao wana mahitaji maalum, hasa walemavu wa macho. Serikali tunaendelea kufuatilia kwenye mabenki yote ili kuhakikisha angalau katika ATM hizi wanafunga kwa uharaka mashine hizi ili kuwasaidia ndugu zetu waweze kupata huduma stahiki.

Mheshimiwa Spika, na hili alilolisema naomba nizielekeze benki zote nchini na naamini kwa Utanzania wetu, kwa utamaduni wetu tulivyolelewa Watanzania, huduma hizi zinatolewa, mtu mwenye ulemavu anapokuwa kafika benki kuhitaji huduma hizi watumishi wa benki zetu wamekuwa wakiwahudumia wakitoka nje kwenda kuwahudumia. Naomba tu nisisitize kwa zile benki na taasisi za kifedha ambazo hawajaanza kufanya huduma hizi basi waweze kuwahudumia ndugu zetu kutokana na uhitaji huo, nawaomba sana, na haya yachukuliwe kama maelekezo ya Serikali. Wakati huohuo benki zote kwenye miundombinu ya kuingia kwenye ATM ambapo wametengeneza step slopes basi warekebishe ili iwe rahisi kwa ndugu zetu wenye ulemavu kuweza kufikia huduma hizi kwenye mashine hizi.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:- ATM za Benki nyingi hapa nchini hazikidhi mahitaji ya watu wenye ulemavu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa ATM za Benki zinawekewa mifumo inayokidhi mahitaji ya watu wenye ulemavu?

Supplementary Question 2

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya watu wenye ulemavu naomba niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa hivi karibuni kumekuwa na uhakiki wa simu, uhakiki wa passports zetu na shughuli za kibenki. Na kuna walemavu wengi ambao hawana vidole, na wanatumia vidole ili kuhakiki; je, Serikali imeweka mpango gani madhubuti wa kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata haki zao?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, nimeipokea changamoto hii na ninaomba tufanye kazi kwa pamoja Wizara yetu ya Fedha, hasa kwenye taasisi zetu za kifedha na mabenki yetu na Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano ili tuone jambo hili tunalishughulikia kwa haraka na ndugu zetu hawa waweze kupata huduma hii.