Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Ujenzi wa Bwawa la Matwiga Wilayani Chunya umechukua zaidi ya miaka mitano bila kukamilika:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi huo?

Supplementary Question 1

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Napenda niseme tu nimefarijika sana kuona kwamba Serikali inatambua kwamba Wilaya ya Chunya ina changamoto ya uhaba wa maji vijijini sababu ya uchache wa vyanzo vya maji. Kwa hiyo, tunapoomba miradi ya Chunya, Serikali iitikie haraka kupeleka miradi hiyo Wilayani Chunya.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, nina maswali mawili madogo ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivi karibuni alitembelea Wilaya ya Chunya na pale Chunya Mjini alikuta kuna changamoto ya usambazaji wa maji katika Mji wa Chunya. Mheshimiwa Rais aliamuru Wizara itoe fedha ya ziada ili kurekebisha usambazaji wa mabomba ambayo yalikuwa yameharibika na nashukuru Serikali imetoa hiyo fedha na sasa hivi usambazaji unaendelea. Je, usambazaji huu utaisha lini?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, katika Mradi wa Maji wa Miji 26 nchini Tanzania, Chunya ni mojawapo ya miji hiyo
26. Je, mkandarasi atakuwa site lini kuweza kurekebisha maji mjini Chunya?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza, napenda nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Chunya, Lupa pale, Mheshimiwa Mwambalaswa umekuwa miongoni mwa Wabunge ambao wamekuwa wakifuatilia sana suala la maji katika majimbo yao. Sisi kama Wizara ya Maji hatutokuwa kikwazo na ndiyo maana tumewapa fedha zaidi ya shilingi milioni 372 kwa ajili ya usambazaji wa maji kwa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Mbeya katika kuhakikisha wanakamilisha mradi ule. Nachotaka kumhakikishia, kazi kama tulivyopanga itakamilika na tunaiagiza Mamlaka ya Maji ya Mbeya kuhakikisha mradi ule unakamilika kwa wakati ili wananchi wake waweze kupata huduma ya maji.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Mradi wa Maji kwa Miji 28, kwa kutambua changamoto ya maji maeneo mbalimbali, Mheshimiwa Rais ametupatia fedha zaidi ya dola milioni 500, ni fedha za mkopo, kwa ajili ya miji 28. Mhandisi Mshauri ameshapita site zote, sasa hivi tunasubiri kibali kwa ajili ya kumpata mkandarasi ambaye tutahakikisha tunampata kwa wakati ili aweze kutekeleza miradi hiyo. Nataka nimhakikishie ndani ya mwezi Oktoba mkandarasi atakuwa amekwishapatikana na utekelezaji utakuwa umeanza.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Ujenzi wa Bwawa la Matwiga Wilayani Chunya umechukua zaidi ya miaka mitano bila kukamilika:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi huo?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa ucheleweshaji wa ukamilishwaji wa miradi ya maji wakati mwingine imepelekea kuwa na matatizo makubwa hasa kwa watumiaji. Hii inaenda sambamba na mamlaka zinazosimamia maji kulazimika kuangalia utaratibu mpya wa kuongeza gharama za maji kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) na matokeo yake bill za maji zimekuwa zikipanda sana kila wakati. Hivi tunavyozungumza kuna upandishwaji wa bill ambao unatokana tu na upungufu wa miradi mingi inayoweza ikazalisha maji kwa kiwango kikubwa.

Mheshimiwa Spika, nataka kufahamu kutoka kwa Mheshimiwa Waziri, nini mkakati madhubuti wa Serikali wa kuendelea kuwapunguzia wananchi mzigo wa kulipa bill kubwa kila wakati kutokana na miradi mingi kukwama pengine kutokana na mikataba ya kifedha iliyocheleweshwa ili fedha hiyo iweze kutoka na miradi hii iweze kukamilika kwa wakati?

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza Mheshimiwa Stanslaus Mabula, kiukweli ni Mbunge ambaye anayefanya kazi na anawatendea haki wananchi wake wa Nyamagana.

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha miradi ya maji inakamilika kwa wakati, sisi Wizara ya Maji tumejipanga baadhi ya miradi mingi tutaitekeleza kutumia Force Account kwa maana ya wataalam wetu kuweza kutekeleza miradi ile ili iweze kukamilika na wananchi wapate huduma ya maji.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la bei za maji, tulipata malalamiko kwa wananchi wa Mwanza na Mheshimiwa Waziri ametoa maagizo maalum kwa EWURA kuhakikisha zile bei zinapitiwa ili wananchi wa Mwanza na maeneo mengine waweze kupata bei ambazo zitakuwa rafiki na waweze kupata huduma hii kwa urahisi. Katika kuhakikisha tunaondoa changamoto hii ya bill, sisi kama Wizara ya Maji tumejipanga na agizo maalumu la Mheshimiwa Waziri ni kuhakikisha kwamba tufunga pre-paid meter katika kuhakikisha wananchi wanalipa kutokana na kile ambacho wamekitumia.

Mheshimiwa Spika, kingine naomba niwasisitize wananchi matumizi ya maji yasiyokuwa na ulazima yanasababisha kuongezeka kwa bili za maji. Leo mvua inanyesha lakini mwananchi anatumia bomba kumwagilia maji maua, haipendezi na wala haifurahishi. Hii ni changamoto lakini naomba Waheshimiwa Wabunge tutoe elimu hii ili kuhakikisha kwamba wananchi wanatumia vizuri maji na wanapata nafuu kabisa katika matumizi haya ya maji.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Ujenzi wa Bwawa la Matwiga Wilayani Chunya umechukua zaidi ya miaka mitano bila kukamilika:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi huo?

Supplementary Question 3

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Serikali imekuwa ikitenga fedha kupeleka katika miradi mbalimbali ya maji. Miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na Mradi wa Mfili ambao uko Wilaya ya Nkasi lakini mradi huo umeshindwa kabisa kumaliza changamoto ya maji. Napenda kujua, Serikali ina mkakati gani wa ziada wa kuweza kumaliza changamoto hizo ili kuendena na kauli ya kumtua mama ndoo kichwani?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha tunatatua tatizo la maji vijijini, Bunge lako Tukufu limetenga zaidi ya shilingi bilioni 301. Pia, tumepata zaidi ya dola milioni 500 kwa ajili ya kutatua tatizo la maji zaidi ya miji 28. Vilevile tumepata fedha zaidi ya shilingi bilioni 25.9 kwa ajili ya kukarabati vituo (Payment by Result- PbR) katika kuhakikisha tunatatua tatizo hili la maji.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge sisi kama Wizara ya Maji hatutakuwa kikwazo tutahakikisha tunafuatilia miradi yetu na mingine tutaifanya kwa kutumia wataalam wetu wa ndani ili kukamilisha kwa wakati na wananchi wapate huduma ya maji.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.