Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kifungu cha 31(1) cha Sheria ya Watu Wenye Ulemavu ya mwaka 2010 kinatekelezwa ipasavyo?

Supplementary Question 1

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi kwanza nishukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa namna anavyozifikia Halmashauri zetu na kutoa maelekezo namna ya kuitekeleza mahitaji ya watu wenye ulemavu. Nilikuwa nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mkakati wa kuanzisha kanzidata nilitaka kufahamu ni utaratibu gani unaotumika kuwapata wahitimu wenye ulemavu ili waweze kuingizwa katika kanzidata?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili katika Halmashauri zetu kuna vikundi vya wajasiriamali wenye ulemavu wakiwepo mafundi selamala, lakini wameshindwa kupata masoko katika ofisi za umma. Nilitaka kufahamu Serikali ina utaratibu gani wa kuwasaidia kupata masoko ili waweze kukuza mitaji yao? (Makofi)

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, WENYE ULEMAVU (MHE. STELLA A. IKUPA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ninaomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Leah Komanya Mbunge wa Viti Maalum, pia nitumie nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Leah kwa jinsi ambavyo amekuwa akihakikisha kwamba watu wenye ulemavu Mkoani Simiyu wanaenda vizuri. Nilienda ziara Mkoani Simiyu tulikuwa naye na kuna mambo niliahidi na niliweza kutekeleza pia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza ameuliza kwamba ni utaratibu gani ambao Serikali tunautumia kuwapata wahitimu hao wenye ulemavu na kuweza kuwaingiza kwenye kanzidata yetu.

Awali ya yote tuliweza kuviandikia vyuo vyote vya elimu ya juu pamoja na vyuo vingine ambavyo vinatoa mafunzo kwamba watu wenye ulemavu wanapohitimu basi Ofisi ya Waziri Mkuu kuna kanzidata ambayo tunawaingiza na kuweza kuwapatia ajira. Lakini njia nyingine ambayo tumekuwa tukiitumia ni watu wenye ulemavu mara nyingi wamekuwa wakipiga simu na wakija ofisini wao wenyewe physically kwa ajili ya kutafuta ajira. Kwa hiyo, wanapokuja pale ofisini tunapata zile details zao na kuweza kuwaingiza kwenye kanzidata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niiongee tu kwa kifupi kwamba kanzidata hii imekuwa na manufaa makubwa, hata mwaka jana tuliweza kupata walimu ambao waliajiriwa pale nafasi za ajira zilipotangazwa kupitia kanzidata hii. lakini pia sasa hivi tuna programy ya internship kwa vijana na tunaposema vijana ni pamoja na vijana wenye ulemavu na tunaposema vijana ni pamoja na vijana wenye ulemavu. Kupitia kanzidata hii tumepata wahitimu wenye ulemavu zaidi ya 100 ambao watanufaika nah ii program ya internship. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ameuliza kwamba ni kwa jinsi gani Serikali inafanya kuhakikisha kwamba watu wenye ulemavu wanapata masoko ya bidhaa zao, tumekwisha kuzielekeza Halmashauri kutenga maeneo kwa ajili ya biashara za watu wenye ulemavu, lakini pia masoko ambayo yamekuwa yakiandaliwa sasa hivi tumesisitiza kwamba miundombinu ni lazima iwe rafiki kwa watu wenye ulemavu, lakini pia ndani ya hayo masoko wahakikishe kwamba kunakuwa na maeneo ambayo ni maalum kwa ajili ya watu wenye ulamavu. Mikakati ya Serikali iko migni lakini kwa ufupi ni hiyo. (Makofi)

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kifungu cha 31(1) cha Sheria ya Watu Wenye Ulemavu ya mwaka 2010 kinatekelezwa ipasavyo?

Supplementary Question 2

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na nimshukuru pia Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Pamoja na jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali na hasa katika sekta ya elimu imefanikiwa kuajiri walimu wengi wenye mahitaji maalum, lakini changamoto kwa walimu hawa wanaoajiriwa tatizo kubwa ni vifaa maalum ambavyo vinawasaidia hasa walimu wasiioona, changamoto ni kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nini kauli ya Serikali katika kuhakikisha kwamba walimu hawa wanaoajiriwa kwanza wanapelekwa katika shule zenye miundombinu rafiki, lakini pia vifaa hivyo kwamba wanawasaidia ili waweze kufanya kazi zao kwa ufasaha? Ahsante.

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, WENYE ULEMAVU (MHE. STELLA A. IKUPA): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mwongozo wa watumishi wenye ulemavu na mwongozo huu tumekuwa tukiutumia kuhakikisha kwamba mtumishi yeyote mwenye ulemavu anapata mahitaji yake ya msingi kwa mujibu wa yale ambayo yameelekezwa ndani ya mwongozo.

Kwa upande wa walimu wenye ulemavu tumekuwa tukielekeza ama mtu mwenye ulemavu yeyote si walimu peke yake, lakini mtu mwenye ulemavu yoyote anapokuwa anafika mahali akaajiriwa basi yeye ni wajibu wake na ndio mwongozo unavyosema kwamba ni wajibu wake kuweza kueleza mahitaji yake kwa mwajiri wake kwamba ili aweze kutekeleza majukumu yake basi mahitaji yake ya msingi ni nini na pale ambapo mwajiriwa huyu anapeleka mahitaji yake kwa mwajiri sisi kama Serikali tumekuwa tukifanya ni sawa na ambavyo tulikuja hapa Bungeni tulikaa na uongozi pia wa Bunge tukiwa Wabunge tukaeleza kwamba kama Wabunge wenye ulemavu tuna mahitaji gani na ili ufanisi wetu katika kazi uweze kwenda vizuri basi Bunge lifanye nini ili tuweze kufanya vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ndani ya Serikali haya yamekuwa yakifanyika, walemavu wa viungo wamekuwa wakipatiwa usafiri, lakini pia na wengine kulingana na mahitaji yao. (Makofi)

Name

Catherine Nyakao Ruge

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kifungu cha 31(1) cha Sheria ya Watu Wenye Ulemavu ya mwaka 2010 kinatekelezwa ipasavyo?

Supplementary Question 3

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru Sheria ya Watu Wenye Ulemavu ya mwaka 2010 kifungu cha 31 kinataka waajiriwa waajiri wote kuajiri angalau asilimia tatu ya watu wenye ulemavu. Ni nini sasa mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba Bunge ambalo ndio chombo kinachotunga sheria kinatimiza matakwa haya ili kutoa mfano kwa waajiri wengine? (Makofi)

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, WENYE ULEMAVU (MHE. STELLA A. IKUPA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ameuliza Bunge kama nimemuelewa vizuri ameuliza kwamba ni nini sasa kwamba Bunge ili lioneshe mfano nadhani sasa hilo ni suala uongozi wa Bunge kwamba ni kwa jinsi gani sasa Bunge litafanya ili kuonesha mfano kwa kuajiri watumishi wenye ulemavu kwa kuzingatia sheria kwamba asilimia tatu ni lazima iwe ni watu wenye ulamavu. (Makofi)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kutendea haki sana kiti chake na kujibu maswali mazuri yaliyoulizwa kwa niaba ya Ofisi ya Waziri Mkuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba kupitia Tume ya Huduma za Bunge ambayo ndio yenye Mamlaka ya Ajira katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ajira kwa watu wenye ulemavu pia zimekuwa zikizingatiwa na kama Waheshimiwa Wabunge mtaona mnapishana na watumishi wengine baadhi ya watumishi kwenye Ofisi ya Bunge wakiwa wenye ulemavu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ili kuweza kupitia hizo quota na viwango vinavyotakiwa kisheria yako mambo mengi ambayo pia yanatakiwa kuzingatiwa kwa mujibu wa Sheria za Utumishi wa Umma. Hata hivyo Tume ya Utumishi wa Bunge itaendelea kuzingatia sheria nyingine pamoja na sheria hii ya mwaka 2010 ya Watu Wenye Ulemavu ili kuhakikisha kwamba kadri watu wenye ulemavu wanavyoweza kutoa huduma na kuajirwa katika taasisi za Serikali na sekta binafsi waendelee kupewa nafasi na haki sawa kama Watanzania wengine. (Makofi)