Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:- Shule ya Msingi Kambarage ni shule pekee katika Wilaya ya Liwale inayochukua watoto wenye mahitaji maalum (walemavu); lakini shule hiyo haina walimu wenye taaluma hizo na vilevile miundombinu ya shule hiyo sio rafiki kwa watoto wenye ulemavu:- (a) Je, ni lini shule hiyo itapatiwa walimu wenye taaluma husika ili kukidhi mahitaji ya shule? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha mazingira ya shule hiyo ili iweze kukidhi mahitaji ya watoto hao?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Vilevile napenda kutoa shukrani kwa Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya msingi niliyosema shule hii ni shule pekee katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale, shule pekee yenye inawachukuwa watu wenye mahitaji maalum, kwa takwimu hiyo utaona kabisa kwamba bado kuna tatizo la miundombinu, shule hii inahitaji mabweni na ndiyo maana inakuwa na takwimu ndogo ya walemavu kwa sababu walemavu wengi kutoka vijijini wanashindwa kumudu kuandikishwa kwenye shule hii kwa sababu ya ukosefu wa mabweni, lakini siyo hivyo hata wale walimu hao anaowataja...

MWENYEKITI: Uliza swali basi Mheshimiwa.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, najenga hoja; je, Mheshimiwa Waziri haoni umuhimu wa kujenga mabweni kwenye shule hii ili watoto wanaotoka nje ya Halmashauri hii waweze kumudu kuingia shuleni?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kwa sababu ya mahitaji ya wanafunzi hawa wanatakiwa wafuatiliwe kule wanapokaa manyumbani kwa sababu hawakai bweni kwahiyo panahitajika usafiri wa walimu hao kuwafuatilia kule wanapoishi kuona maendeleo yao namna gani wanavyo catch yale masomo. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwanunulia vifaa kama vile mapikipiki hawa walimu watatu waliobaki ili waweze kumudu kuwafuatilia hawa watoto manjumbani kwao?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Serikali tunakubaliana na Mheshimiwa Mbunge, kwanza tunaunga jitihada za Mheshimiwa Mbunge katika kuhakikisha kwamba hawa wanafunzi wenye uhitaji maalum wanapewa kipaumbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge jana nilipata fursa ya kuongea na mkurugenzi na tukakubaliana kwamba hicho kiasi cha shilingi milioni 50 itatengwa kuanzia mwezi Desemba wakati tutakapokuwa wanafanya review ya bajeti yao kwa sababu na wanaona ni jambo la muhimu sana kuhakikisha watoto hawa wanakuwa katika mazingira yaliyo bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika swali lake la pili anaongelea swala zima la usafiri ili walimu waweze kwenda kupata fursa kwenda kuwabaini hata wanafunzi wengine ambao wanashindwa kujiunga kutokana na adha iliyoko huko, naomba ni muhakikishie Mheshimiwa Mbunge ni azma ya Serikali, siyo walimu peke yao ni pamoja watumishi wote ikiwepo wale wa Ustawi wa Jamii kuhakikisha kwamba tunawabaini watoto wetu wote bila kujali hali zao ili waweze kupelekwa katika maeneo ya kuweza kujufunza sawa na watoto wengine ambao hawana ulemavu.

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:- Shule ya Msingi Kambarage ni shule pekee katika Wilaya ya Liwale inayochukua watoto wenye mahitaji maalum (walemavu); lakini shule hiyo haina walimu wenye taaluma hizo na vilevile miundombinu ya shule hiyo sio rafiki kwa watoto wenye ulemavu:- (a) Je, ni lini shule hiyo itapatiwa walimu wenye taaluma husika ili kukidhi mahitaji ya shule? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha mazingira ya shule hiyo ili iweze kukidhi mahitaji ya watoto hao?

Supplementary Question 2

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, pale jimboni Kondoa tunazo shule mbili, Shule ya Iboni na Shule ya Ubembeni ambazo zinavitengo vya watoto wenye mahitaji maalum zote ziko kata moja ya Chemchem ambayo ni kata ya katikati kabisa katika jimbo zima. Hali ya mapato yetu ya ndani ya Halmashauri ni ndogo sana ambayo imetupelekea mpaka mimi mfuko wa jimbo kuweza kusaidia miundombinu stahiki kwa ajili ya wale watoto pamoja na choo, walimu pia hatuna.

Je, Waziri ni lini unaweza ukafanya utaratibu wa kutuupa uzito na kuja kufanya tathimini ya kina ili tuweze kuweka miundombinu stahiki na walimu wa kututosheleza ukizingatia watoto hao wenye mahitaji maalum wanaendelea kuongezeka siku hadi siku?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Sannda kwa jitihada zake kwa kutumia mfuko wa Jimbo ili kuhakikisha kwamba miundombinu wezeshwi inajengwa katika shule hizo, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba watoto wote wenye uhitaji maalum hawaachwi nyuma na suala zima la uhitaji wa walimu ambao wanatakiwa waajiriwe naomba nimuhakikishie kama sisi Serikali tutazingatia maombi yake.

Name

Joyce John Mukya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:- Shule ya Msingi Kambarage ni shule pekee katika Wilaya ya Liwale inayochukua watoto wenye mahitaji maalum (walemavu); lakini shule hiyo haina walimu wenye taaluma hizo na vilevile miundombinu ya shule hiyo sio rafiki kwa watoto wenye ulemavu:- (a) Je, ni lini shule hiyo itapatiwa walimu wenye taaluma husika ili kukidhi mahitaji ya shule? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha mazingira ya shule hiyo ili iweze kukidhi mahitaji ya watoto hao?

Supplementary Question 3

MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, Shule ya Msingi ya Uhuru iliyoko Arusha ni shule pia yenye watoto walemavu, shule hii inashida pia ya miundombinu, vyoo vyake havifai ukizingatia kuwa walemavu wengi au baadhi ya walemavu ni wale ambao wanatambaa, ukiangalia vile vyoo ni vichafu, havifanyi kazi vizuri maji mpaka yanatitirika nje na tunavyoelewa ukiongelea swala zima la vyoo ni afya.

Je, Serikali itarekebisha lini miundombinu ile ya vyoo katika hile shule ya Uhuru ya Arusha Mjini ili kuwasaidia walemavua hawa watoto? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba nichukuwe fursa hii kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Arusha kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu katika swali langu la msingi nikimuelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri


ya Liwale naomba nitumie fursa hii kumuelekeza Mkurugenzi wa Jiji Arusha kwa sababu nina uhakika wanavyanzo vya mapato vya kutosha, atizame namna gani wataweza kuboresha miundombinu ili wanafunzi wetu wenye uhitaji maalum wasome katika mazingira yaliyo bora.