Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST Aliuliza:- Je, Serikali imefikia wapi katika mchakato wa kulipa fidia kwa wananchi wa Kipunguni waliotakiwa kusitisha kuendeleza maeneo yao ili kupisha upanuzi wa kiwanja cha ndege?

Supplementary Question 1

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nitoe masikitiko kwamba leo ni mara ya nne ninauliza swali kuhusu kulipwa fidia kwa wananchi wa Kipunguni. Leo najibiwa kwa mara ya nne, mara ya tatu majibu yalibadilika nikaambiwa wangelipwa kwa mwaka wa fedha ulioisha, lakini kwa jibu la leo naona tumerudi nyuma. Serikali inasema watalipwa pale itakapopata fedha, sio sahihi kabisa hawa wananchi wamezuiwa kuendeleza maeneo yao kwa muda mrefu. Wananchi wengi wanakufa, wengine wanashindwa kujiletea maendeleo ni changamoto kubwa sana. Sasa swali langu halijajibiwa ni lini hawa wananchi watalipwa fidia kwa kuwa tuliambiwa wangelipwa mwaka jana?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili zaidi ya wananchi 322 walienda mahakamani baada ya kutoridhishwa na mchakato ambao ulikuwa ni pamoja na kutolipwa viwango stahili na kutokubalina na tathimini.

Sasa Serikali ipo tayari kurudi na kuongea na wananchi hawa waondoe kesi mahakamani wafanyiwe tadhimini upya ili walipwe stahili zao sambamba na tathimini ya sasa ili wapate faida ya maeneo yao? Naomba majibu.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mbunge Anatropia kuhusiana na fidia ya Ukonga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nitajibu swali la mwisho, suala la mahakamani kwa sababu wao wameenda mahakamani hatuwezi kulizungumza humu Bungeni. Niombe Mheshimiwa Mbunge tuache hatua za kimahakama ziendelee, ruling inatakapokuwa imekuja basi sisi ndio tutaendelea nalo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu fidia ndio utaratibu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inalipa fidia pale ambapo inatekeleza mradi. Awamu ya kwanza tulikuwa tunajenga Terminal III tulilipa fidia kupata lile eneo na ukuta tumejenga. Tutakapohitaji kufanya maendelezo ya ule mradi tena kama ambavyo jibu la msingi limesema basi tutaendelea, tutachukua hilo eneo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ni kweli kwamba tumezuia wananchi wasifanye maendelezo katika eneo ambalo tumeli-earmark kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Na hilo sio kwenye uwanja tu hata kwenye barabara. Kwa hiyo, tunafanya hivyo ili serikali pia isiingie gharama kubwa wakati wa ujenzi wa barabara wakati wa fidia.

Kwa hiyo, nikujibu tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ya Chama cha Mapinduzi ipo makini itahakikisha kwamba pale ambapo inatekeleza mradi watalipwa fidia kwa mujibu wa sheria.