Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE Aliuliza:- Kumekuwa na mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kuelekea Mikoa ya Shinyanga na Tabora vyenye mitambo yake chanzo cha maji kule Ihelele Wilayani Misungwi, aidha maeneo yanayozunguka mitambo hiyo na yanayopitiwa na mabomba ya mradi huo hayana maji safi na salama. Je, nini mpango wa Serikali kusambaza maji safi na salama kutoka Ziwa Victoria kwa wananchi wa vijiji vya Mkoa wa Mwanza hususan maeneo yanayopitiwa na bomba hilo?

Supplementary Question 1

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nianze kwa kuipongeza Serikali kwa majibu mazuri ambayo inaonesha jitihada ya kusambaza maji ndani ya Mkoa wa Mwanza. Pamoja na majibu hayo naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

(i) Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji alivyokuja Misungwi aliahidi kukamilisha malipo ya mkandarasi mradi huu tajwa hapa wenye gharama ya shilingi bilioni 6.1. Lakini mpaka sasa hivi kwa taarifa niliyonayo ni kwamba kuna sintohamu nyingi, mimi ombi langu moja ningependa kujua ni lini Waziri atapata muda wa kuambatana na mimi pamoja na Mbunge wa Jimbo ili tuende tukae na makandarasi na wananchi ili tupate jibu sahihi ya lini watapata maji safi na salama?

(ii) Mara ya Mwisho Mheshimiwa Waziri Mkuu alivyotembelea Misungwi aliahidi mradi wa maji wa Misungwi pamoja na Igokelo kukamilishwa na kukabidhiwa mwezi wa tano. Ikasogezwa ikawa ni mwezi wa nane, leo hii tunavyongea ni mwezi wa tisa. Ningependa kujua ni nini mpango wa Serikali wa kukamilisha mradi huu ili wananchi wa Misungwi waweze kupata maji safi na salama?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kiukweli Mheshimiwa Maria Kangoye ni Mbunge king’anga’nizi katika kutetea wananchi wake. Lakini niungane pamoja na Mheshimiwa Kitwanga kwa kazi kubwa wanaifanya katika Jimbo la Misungwi kubwa ambalo ninachotaka kusema utekelezaji wa mradi wa maji unategemea na fedha nataka nimhakikishie mkandarasi anayetekeleza mradi ule shilingi bilioni 6.1 sisi kama Wizara ya maji hatutakuwa kikwanzo na Mheshimiwa Mbunge na kuhakikishia certificate ile na mradi uweze kuendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili ni kuhusu utekelezaji wa mradi pale Misungwi tuna mradi takribani shilingi bilioni 12 kutokana na kilio cha Mheshimiwa Mbunge Mzee wangu Kitwanga. Wiki ijayo tunakwenda kukabidhi mradi ule ili wananchi waweze kupata maji, na ninataka kumtia moyo Mheshimiwa Kangoye na Mheshimiwa Kitwanga unapotembea na kuzuru wengine naomba usinipite mwokozi, sitowapita nitakuja mwenye Misungwi kushuhudia namna gani wananchi wanaenda kupata maji wiki ijayo. Ahsante sana Mheshimiwa.

Name

Charles Muhangwa Kitwanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE Aliuliza:- Kumekuwa na mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kuelekea Mikoa ya Shinyanga na Tabora vyenye mitambo yake chanzo cha maji kule Ihelele Wilayani Misungwi, aidha maeneo yanayozunguka mitambo hiyo na yanayopitiwa na mabomba ya mradi huo hayana maji safi na salama. Je, nini mpango wa Serikali kusambaza maji safi na salama kutoka Ziwa Victoria kwa wananchi wa vijiji vya Mkoa wa Mwanza hususan maeneo yanayopitiwa na bomba hilo?

Supplementary Question 2

MHE. CHARLES M. KITWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya matumaini ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kuna mradi mwingine ambao umekuwepo kwa muda mrefu sana; mradi wa kutoa maji katika Ziwa Victoria sehemu ya Butimba kupeleka Wilaya ya Ilemela, vilevile kuleta Usagara Wilaya ya Misungwi pamoja na Kisesa Wilaya ya Magu. Kumekuwa na muda mrefu sana tunaambiwa watasaini mkataba. Naomba basi nifahamu leo hii ni lini mkataba utasainiwa na mradi huo uanze haraka iwezekanavyo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji napenda kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kiukweli Mheshimiwa Kitwanga ni miongoni mwa Wabunge ambao ni wafuatiliaji ususani mambo yanayohusu wananchi wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kusema ukimuona mtu mzima analia ujue kuna jambo. Mheshimiwa Kitwanga sio mara moja analizunguzia hili jambo, nataka nimhakikishie serikali ya awamu ya tano ni serikali ya matokeo sio serikali ya mchakato. Na kwa kuwa sisi tupo karibu sana na Wizara Fedha nikuombe Mheshimiwa Mbunge nikuombe hebu tukutane leo ili tukae na wenzetu wa Wizara ya Fedha hili jambo tuweze kukalisha na wananchi wako waweze kupata huduma hii muhimu sana safi na salama.

Name

Kiza Hussein Mayeye

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE Aliuliza:- Kumekuwa na mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kuelekea Mikoa ya Shinyanga na Tabora vyenye mitambo yake chanzo cha maji kule Ihelele Wilayani Misungwi, aidha maeneo yanayozunguka mitambo hiyo na yanayopitiwa na mabomba ya mradi huo hayana maji safi na salama. Je, nini mpango wa Serikali kusambaza maji safi na salama kutoka Ziwa Victoria kwa wananchi wa vijiji vya Mkoa wa Mwanza hususan maeneo yanayopitiwa na bomba hilo?

Supplementary Question 3

MHE. KIZA H. MAYEYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona naomba kuliza swali kama ifuatavyo:-

Halmashauri ya Kigoma Vijiji ina vijiji cha Mwandiga, Kiganza, Bitale, Mkongoro na Msimba ambavyo mpaka sasa wananchi wanateseka kwa kukosa maji, kipundupindu ni cha kwao, lakini kina mama hata ndoa zao zinakwenda kuhatarika.

Ni lini sasa mradi wa Ziwa Tanganyika na ule wa Kigoma Manispaa utafika katika vijiji hivi? Ahsante sana.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji kwanza napenda nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba kubwa tunapozungumzia maji, maji ni uhai na sisi kama viongozi wa Wizara ya Maji hatupo tayari kupoteza uhai wa wana Mwandiga. Mheshimiwa Mbunge nilivyokuja ziara katika yetu Peter Serukamba alipiga kelele sana kuhusu suala la kupelekewa fedha ili tutekeleze maji na Mheshimiwa Waziri ametuma fedha tayari na ile kazi itatekelezwa na watalaamu wetu wa ndani katika kuhakikisha wana Mwandiga wananufaika na mradi wa uwepo wa Ziwa Tanganyika kati eneo hilo. Ahsante sana.

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE Aliuliza:- Kumekuwa na mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kuelekea Mikoa ya Shinyanga na Tabora vyenye mitambo yake chanzo cha maji kule Ihelele Wilayani Misungwi, aidha maeneo yanayozunguka mitambo hiyo na yanayopitiwa na mabomba ya mradi huo hayana maji safi na salama. Je, nini mpango wa Serikali kusambaza maji safi na salama kutoka Ziwa Victoria kwa wananchi wa vijiji vya Mkoa wa Mwanza hususan maeneo yanayopitiwa na bomba hilo?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri yanatia matumaini mazuri. Napenda kufahamu mradi wa maji wa kutoka Bukabile katika Wilaya ya Busega kwenda katika Wilaya za Bariadi Itilima, Meatu na Maswa ni lini mradi huu utaanza kutelezwa, licha kwamba fedha zilishapatikana na mpaka sasa hivi tuliambiwa mwezi wa tisa tutasaini mkataba lakini mpaka sasa hivi hatujasaini mkataba wowote. Nataka kujua ni lini mradi huu sasa utaanza kutekelezwa?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji napenda kwanza kumpongeza Mheshimiwa Mbunge anafanya kazi kubwa sana. Lakini pia napenda nimfahamishe kwamba mkataba tumekwisha kusaini mradi ule na nikuombe Mheshimiwa Mbunge kutokana na kazi kubwa ambayo Mheshimiwa Waziri ambayo ameitupia jicho katika Mkoa ule wa Simiyu ni kuombe tuweze kukutana tuweze kupeana update lini tutaweza kuutekeleza ili wananchi wako waweze kupata huduma ya maji. Ahsante sana.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIA N. KANGOYE Aliuliza:- Kumekuwa na mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kuelekea Mikoa ya Shinyanga na Tabora vyenye mitambo yake chanzo cha maji kule Ihelele Wilayani Misungwi, aidha maeneo yanayozunguka mitambo hiyo na yanayopitiwa na mabomba ya mradi huo hayana maji safi na salama. Je, nini mpango wa Serikali kusambaza maji safi na salama kutoka Ziwa Victoria kwa wananchi wa vijiji vya Mkoa wa Mwanza hususan maeneo yanayopitiwa na bomba hilo?

Supplementary Question 5

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza. Shida iliyopo Mwanza ni sawa na shida iliyopo Mkoani Rukwa, Wilaya Sumbawanga Vijijini Kata ya Kaengesa katika vijiji vya Mkunda, Kaengesa B, Kaengesa A na Italima na vijiji vyote vya wilaya Sumbawanga vijiji.

Ni lini sasa Wizara itapeleka maji katika vijiji hivyo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji napenda nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wake, lakini kubwa ambacho ninachotaka kusema jukumu la wananchi kupata maji ni jukumu letu sisi Wizara ya Maji na nilishasema si mara moja si mara mbili, sisi ni Wizara maji si Wizara ya ukame tumepata fedha ambazo tumetengewa zaidi ya shilingi bilioni 301 na uwanzaishaji huu wa wakala wa maji vijiji kwa maana ya RUWASA tumejipanga miradi mingi katika kuhakikisha tunaitekeleza kutumia wataalamu wetu wandani, nimhakikishie Mheshimiwa Bupe sisi kama Wizara ya maji vijiji ambavyo ameainisha tunajipanga kuhakikisha tunavitatua ili wananchi wake waweze kupata huduma maji. Ahsante sana.