Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE Aliuliza:- Mradi wa REA III(1) unatekelezwa katika Jimbo la Tabora Kaskazini kwa kasi ndogo na mpaka sasa ni vijiji vitatu tu kati ya vijiji 82 ndiyo vimewashwa umeme. (a) Je, Serikali inachukua hatua gani kumfanya mkandarasi akamilishe kuwasha umeme katika vijiji vyote 18 vya REA III(1)? (b) Kwa vile kwa makosa Mradi wa REA III(1) unarudiwa kupelekwa katika Kijiji cha Upuge, Kata ya Upuge ambako umeme ulishapelekwa na REA III. Je, ni lini sasa umeme utapelekwa katika Kata ya Ikongolo ambako ni Kata jirani na Kata ya Upuge?

Supplementary Question 1

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri na juhudi kubwa inayofanywa na Waziri wa Nishati ninayo maswali mawili ya nyongeza.

(i) Kwa vile katika mradi huu wa REA III uliokuwa na vijiji 18 katika Jimbo langu ni vijiji vinne tu ndiyo vimepata umeme mpaka sasa. Je, ni lini vijiji vyote 18 vitapata umeme?

(ii) Kwa kuwa Jimbo langu lote la Tabora Kaskazini lenye vijiji 82 ni vijiji saba tu ndiyo vimepata umeme. Napata wasiwasi kama kweli umeme utaenea karibu vijiji vyite 82. Je, Serikali inawahakikishia wananchi wa Jimbo la Tabora Kaskazini kwamba vijiji vyite 82 vitapata umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote napenda nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya swali la msingi la Mheshimiwa Almas Maige, lakini zaidi nimpongeze sana Mheshimiwa Maige anavyofuatilia masuala ya umeme katika Jimbo lake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya mwaka 2015 Jimbo zima la Tabora Kaskazini halikuwa na kijiji chochote chenye umeme lakini kwa juhudi kubwa alizofanya Mheshimiwa Maige kufuatilia upatikanaji wa umeme hadi sasa tuna zaidi ya vijiji saba vina umeme. Kwa hiyo, nipende kumpongeza Mheshimiwa Maige lakini niwaombe wananchi wa Jimbo la Tabora Kaskazini wawe na imani na Serikali kwa sababu vijiji vyote 82 vitapelekewa umeme ifikapo mwezi Juni, 2021.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maswali yake mawili ya nyongeza kuhusiana na vijiji 18 ni lini vitapate umeme?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa mkandarasi anaendelea na vijiji vingine pamoja na kwamba ameshawasha vijiji saba alivyotaja Mheshimiwa Mbunge lakini tarehe 25 mwezi huu, mkandarasi atawasha vijiji vingine vine ikiwemo Kijiji cha Ibushi, Kagera ya Nsimbo, Majengo ambako Mheshimiwa Mbunge unatoka kwenye Kata ya Ikongolo pamoja na Mputi navyo vitawashwa umeme tarehe 25 mwezi huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 15 mwezi ujao vijiji vingine vitawashwa umeme ikiwemo Kijiji cha Mkalya, Mpenge pamoja na Ngokoro. Kwa hiyo niwape taarifa wananchi ambavyo Mheshimiwa Mbunge anavyofanya kazi vijiji vyote vya Tabora Kaskazini vitapelekewa umeme ifikapo Juni mwaka 2020/2021.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE Aliuliza:- Mradi wa REA III(1) unatekelezwa katika Jimbo la Tabora Kaskazini kwa kasi ndogo na mpaka sasa ni vijiji vitatu tu kati ya vijiji 82 ndiyo vimewashwa umeme. (a) Je, Serikali inachukua hatua gani kumfanya mkandarasi akamilishe kuwasha umeme katika vijiji vyote 18 vya REA III(1)? (b) Kwa vile kwa makosa Mradi wa REA III(1) unarudiwa kupelekwa katika Kijiji cha Upuge, Kata ya Upuge ambako umeme ulishapelekwa na REA III. Je, ni lini sasa umeme utapelekwa katika Kata ya Ikongolo ambako ni Kata jirani na Kata ya Upuge?

Supplementary Question 2

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, awali ya yote napenda niipongeze Wizara ya Nishati hasa Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya kuifanya Tanzania inayomeremeta. Umeme ni maendeleo, umeme ni uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini kwenye Kata ya Kitumbikwela ambapo kuna Kijiji cha Sinde na Mnali itapatiwa umeme wa REA na maeneo mengine yote yaliyosalia hapa nchini?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa mama yangu Salma Kikwete, Mbunge wa Kuteuliwa na Mheshimiwa Rais.

Kwanza nimpongeze kwa kazi nzuri anayoifanya kutokana na heshima aliyopewa na Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkoa wa Lindi na Mkoa wa Pwani, lakini swali lake limejielekeza kuulizia Kata ya Kitumbikwela, Vijiji vya Sinde na Mnali ni lini vitapata mradi wa REA. Nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mama Salma, natambua hii ni changamoto ambayo aliwasilishiwa alipofanya ziara lakini tumefanya mawasiliano na TANESCO kwa kuwa tuliwapa maelekezo ya kubaini maeneo ambayo yanaweza yakapelekewa miundombinu ya umeme kupitia kwao TANESCO na wamebaini maeneo 754. Moja ya maeneo ambayo wamebaini ni eneo la Kitumbikwela na kwa bajeti ya TANESCO ya mwaka 2019/2020 eneo hilo na vijiji ambavyo amevitaja ikiwemo Mnali vitapatiwa umeme katika kipindi hiki.

Kwa hiyo, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge na maeneo ambayo Lindi yamesalia kati ya vijiji 150, Mkandarasi State Grid anaendelea na kazi na tutaratajia ifikapo Disemba, 2019 kazi itakamilika. Kwa hiyo niwape moyo Wananchi wa Mkoa wa Lindi na Waheshimiwa Wabunge wote akiwemo Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mbunge wa Jimbo la Ruangwa kwamba kazi ya mkandarasi inaendelea na tutamsimamia vizuri ili akamilishe. Ahsante sana.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE Aliuliza:- Mradi wa REA III(1) unatekelezwa katika Jimbo la Tabora Kaskazini kwa kasi ndogo na mpaka sasa ni vijiji vitatu tu kati ya vijiji 82 ndiyo vimewashwa umeme. (a) Je, Serikali inachukua hatua gani kumfanya mkandarasi akamilishe kuwasha umeme katika vijiji vyote 18 vya REA III(1)? (b) Kwa vile kwa makosa Mradi wa REA III(1) unarudiwa kupelekwa katika Kijiji cha Upuge, Kata ya Upuge ambako umeme ulishapelekwa na REA III. Je, ni lini sasa umeme utapelekwa katika Kata ya Ikongolo ambako ni Kata jirani na Kata ya Upuge?

Supplementary Question 3

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na ninakiri kutambua kazi kubwa inayofanywa na Wizara hii kuhakikisha kwamba maeneo mengi yanapata umeme na kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni dogo tu, kumekuwa na changamoto kubwa sana ya upatikanaji wa nguzo kwa wateja wapya hasa kwenye Jimbo la Nyamagana, lakini pia ni lini sasa Serikali itahakikisha Nyamagana ambayo inajengeka kwa kasi kubwa sana kwenye maeneo yote kuanzia Kishiri, Fumagira, Rwanima, Bwigoma na Maina watapata umeme wa uhakika kabla hatujafika kwenye mwisho wa mwaka tuliokusudia? Nakushukuru sana.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nijibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Stanslaus Mabula, Mbunge wa Nyamagana kama ifuatavyo:-

Ni kweli, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Nyamagana mwaka jana tulifanyakazi kubwa sana kuhakikisha wananchi wa mitaa yote ya Nyamagana wanapata umeme na hivi sasa tunavyoendelea kuzungumza vijiji na maeneo ya Kishiri, Fumagira, Buhongwa pamoja na Nyamagana yote kuna wakandarasi wanne wanaofanyakazi na nguzo zaidi ya 2000 zitaondoka tarehe 18 mwezi huu kwenda kufanyakazi Nyamagana. Niwaondoe wasiwasi wananchi na wakandarasi nguzo zipo za kutosha hapa Nchini kuliko hata mahitaji yetu. Kwa hiyo kazi zitafanyika na Nyamagana nzima itapata umeme. Ahsante sana.