Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE Aliuliza:- Je, lini utekelezaji wa mradi wa maji kwa vijiji 57 vya Wilaya ya Kyerwa utaanza kwa kuwa usanifu wa kina wa mradi huo umeshakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza naipongeza Serikali kwa juhudi za kuwapatia wananchi wa Kyerwa maji safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijauliza maswali, kwenye majibu aliyotujibu, kuna sehemu ambayo haiko sahihi. Vijiji vya Kibale, Nyamiaga na Magoma hakuna kisima ambacho kimechimbwa. Kwa hiyo, hiyo taarifa aliyonipa siyo sahihi.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, huu mradi ni muhimu sana kwa ajili ya wananchi wa Jimbo la Kyerwa. Mheshimiwa Waziri ananihakikishia kwenye bajeti ya mwaka 2021/2022 atatenga fedha kwa ajili ya mradi huu ili uweze kutekelezwa? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Ziko Kata ambazo haziko kwenye huu mradi, Kata za Bugomora, Kibale, Murongo pamoja na Businde. Serikali ina mpango gani wa kuzipatia maji Kata hizi ili nao watoke kwenye adha wanayoipata? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Bilakwate, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza kuhusu kutengwa fedha kwa mwaka wa fedha ujao kwa mradi huu mkubwa, azma ya Serikali ni kuhakikisha miradi hii yote tunaitekeleza kwa wakati. Hivyo, katika mwaka wa fedha ujao 2021/2022 mradi huu utapatiwa fedha kwa awamu na utekelezaji wake utaanza mara moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Kata ambazo amezitaja Mheshimiwa Mbunge, napenda tu kusema kwamba tutahakikisha maeneo yote yenye matatizo ya maji, maji yanapatikana. Kwa mradi huu mkubwa ambapo bomba kubwa litapita, michepuo ya maji pia itazingatiwa; na kwa maeneo ambayo michepuo haitafika kwa urahisi, basi uchimbaji na ujenzi wa visima utazingatiwa katika mwaka wa fedha ujao.