Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO Aliuliza: - (a) Je, ni Watumishi wangapi wamerejeshwa kazini baada ya kuondolewa kimakosa wakati wa zoezi la uhakiki wa vyeti feki na Wafanyakazi hewa? (b) Je, ni Watumishi wangapi waliorejeshwa kazini wamelipwa stahiki zao kama mishahara ambayo hawakupata kutokana na kuondolewa kazini?

Supplementary Question 1

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa msamaha ulitolewa kwa wale wote ambao waliondolewa kazini kwa kukosa sifa ya kidato cha nne na baadaye wakajiendeleza kupata sifa hizo; na kuna maeneo ambayo watu hawana mawasiliano ya simu kama Ulingombe, Vidunda, Malolo na Kisanga.

Je, Serikali inatoa tamko gani kwa waajiri kuhakikisha kwamba watu wote ambao wame-qualify kurudishwa na hawana taarifa wanapata taarifa hizi kwa wakati na wanarudishwa kazini bila masharti ya ziada?

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa watumishi hawa ambao walishindwa kujiendeleza kidato cha nne lakini walikuwa na sifa stahiki wakati wanaajiriwa waliondolewa kazini walitumikia hii nchi kwa uadilifu na uzalendo lakini hawakuwa na kosa mahali zaidi ya maelekezo ya Serikali.

Je, ni lini Serikali inaenda kuhakikisha kwamba malipo yao na stahiki zao zinalipwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dennis Lazaro Londo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, msamaha uliotolewa kwa watumishi hawa ambao waliajiriwa baada ya tarehe 20 Mei, 2004 ambapo tangazo la Serikali lilitoka mpaka ifikapo Mei, 2004 watumishi wote wanaoajiriwa Serikalini ni lazima wawe na sifa ya kidato cha nne. Hata hivyo kuna waajiri ambao waliajiri watumishi baada ya tangazo lile la Serikali. Tunatambua kwamba haikuwa kosa la wale watumishi walioajiriwa.

Mheshimiwa Spika, sasa Serikali ilitoa maelekezo kupitia Katibu Mkuu Kiongozi kwamba hawa watumishi wote walioajiriwa baada ya tarehe hiyo wawe wamejiendeleza na kupata sifa ya kuajiriwa Serikalini, yaani cheti cha kidato cha nne mpaka ifikapo Desemba, 2020. Na waliorejeshwa kazini mpaka kufikia Desemba 2020 ni zaidi ya watumishi 4,335 ambao walirudi kwa sababu walikuwa wamejiendeleza.

Mheshimiwa Spika, sasa kwa wale ambao kama Mheshimiwa Mbunge alivyosema, kwamba hawakupata taarifa popote ya kwamba wajiendeleza na walijiendeleza kabla ya ile deadline iliyowekwa basi niwaelekeze waajiri wote nchini kuweza kuliangalia hili kuwachukua watumishi hawa kama walijiendeleza tu kabla ya kufikia Desemba, 2020 lakini hawakupata tangazo la kurejea kazini basi waajiri waweze kuliangalia hilo.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali lake la pili aliulizia wale ambao hawakujiendeleza lakini waliajiriwa baada ya Mei 2004. Hawa siku ya Mei Mosi Mheshimiwa Rais wetu mama yetu Samia Suluhu Hassan alitoa maelekezo, kwamba watumishi wote waliokuwa na sifa ya elimu ya darasa la saba walipwe stahiki zao kwa sababu hawa hawakughushi wao waliajiriwa siyo makosa yao basi stahiki zao kama hawakurejeshwa kazini na kama hawakujiendeleza walipwe. Tayari ofisi yetu ilishatoa waraka kupitia Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Utumishi kwa waajiri wote nchini kuanza kushughulikia hawa wenye elimu ya darasa la saba ambao hawakurejeshwa kazini, na tayari linafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO Aliuliza: - (a) Je, ni Watumishi wangapi wamerejeshwa kazini baada ya kuondolewa kimakosa wakati wa zoezi la uhakiki wa vyeti feki na Wafanyakazi hewa? (b) Je, ni Watumishi wangapi waliorejeshwa kazini wamelipwa stahiki zao kama mishahara ambayo hawakupata kutokana na kuondolewa kazini?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza, na nimpongeze pia Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kutupandisha daraja kutuita kidato cha saba.

Mheshimiwa Spika, watumishi wa darasa la saba ambao waliondolewa kazini walifanya kazi zao kwa uaminifu, wengine walikuwa watendaji na watu wengine; lakini tamko hili lilitoka na waraka ukatoka mpaka leo asilimia 95 hawajawahi kulipwa wala kuitwa wala kupokelewa tu na waajiri. Sasa ningemwomba Mheshimiwa Waziri kama anaweza kutoa commitment angalau akatupa kopi ya zile nyaraka sisi Waheshimiwa Wabunge ili tuweze kwenda kutetea wale waliondolewa na hawajapata stahiki zao?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Musukuma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, watumishi ambao hawakujiendeleza mpaka kufika Desemba, 2020 walikuwa kama 1,491, ambao hawakujiendeleza, na hivyo walikosa sifa ya kurejeshwa katika utumishi wa Umma.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema awali wakati najibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Londo, kwamba Mheshimiwa Rais wetu, mama yetu Samia Suluhu Hassan alitoa agizo lake siku ya Mei Mosi pale Mwanza. Kwamba hawa 1491 stahiki zao zilipwe; na tayari ofisi yetu ya Utumishi ilishatoa waraka tarehe 21 Mei, 2021 kwa waajiri wote kuanza kuhakiki madeni haya na kuangalia stahiki walizotakiwa kulipwa hawa wa darasa la saba. Naamini baada ya muda mfupi hawa 1491 wataanza kulipwa, kwa sababu ilikuwa ni maelekezo ya Mheshimiwa Rais na hivyo tutalitekeleza kama aliyoelekeza yeye Mheshiwa Rais. Ahsante sana.