Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Kituo cha Afya Chunya kilipandishwa hadhi kuwa hospitali ya Wilaya mwaka 2008 lakini kuna tatizo la ukosefu wa chumba cha kuhifadhia maiti:- Je, ni lini Serikali italitatua tatizo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza:
Mheshimiwa Naibu Spika, Naibu Waziri amesema mwaka huu Serikali imetenga shilingi milioni 50. Hizi hela ni hela za Halmashauri, own source ya Halmashauri na mimi Mbunge nitachangia katika hela hizo. Mimi ninalosema Serikali kutoka Makao Makuu iwe Wizara ya Afya au TAMISEMI watachangia kiasi gani kwenye hospitali hiyo ambayo ni ya wananchi wa Wilaya ya Chunya hilo la kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Bunge lililopita la Kumi Serikali ilianzisha mpango wa kukarabati hospitali za Wilaya kumi, kuziinua kiwango ziweze kutibu maradhi yote ili kupunguza congestion kwenye hospitali ya rufaa na Chunya ilikuwa mojawapo katika hospitali hizo kumi katika Tanzania.
Je, huo mpango umefia wapi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli safari hii imetengwa shilingi milioni 50 na tunapofanya mobilization of resources mara nyingi sana kuna vipaumbele, najua wazi kwamba pesa hizi ni own source. Lakini siyo kusema kwamba kwa vile ni own source basi Serikali maana yake haina jicho lake ndiyo maana mchakato wa bajeti kuna pesa nyingine zinatoka katika Serikali za Mitaa na nyingine zinatoka katika Serikali Kuu. Wakati mwingine kipaumbele cha baadhi ya vipengele inaenda katika miradi mingine. Kwa hiyo, lengo kubwa ni Serikali kupeleka mchakato huo mpana na mwisho wa siku ni kwamba wananchi kuweza kupata huduma.
Mheshimiwa Mwambalaswa naomba nikuhakikishie kwamba hela hii ni own source na ninajua kwamba na ninyi mmefanya harakati na wewe mwenyewe ulikuwa ukisimamia ile harakati ya harambee. Mimi naomba niwapongeze kwa sababu miongoni mwa watu ambao wamefanya wenyewe kuhakikisha kwamba wanafanya harambee tena ikiongezewa na Mbunge Mwambalaswa nikupongeze katika hilo. Naomba nikuhakikishie kwamba katika mchakato wetu najua hii itakapokuwa imekamilika lazima kutakuwa na mapungufu mengine yatakuwa yanajitokeza katika kuhakikisha hospitali ile inaweze kufanya kazi. Jukumu la Serikali mwisho wa siku ni kwamba hospitali ile ya Chunya iweze kuwa na hadhi sasa kama nyingine, naomba nikuhakikishie kwamba tutakuunga mkono kwa nguvu zote kwa vile umekuwa ukipigania katika hili tutashirikiana kwa jinsi zote.
Suala zima la ukarabati kama ulivyosema kulikuwa na mchakato wa ukarabati ni kweli, na maeneo mbalimbali ukarabati huu ulikuwa unaendelea. Lakini bado tukiri wazi tatizo hili bado ni kubwa sana ukiachia ukarabati; hata niliposema wiki iliyopita, kwamba ukiacha ukarabati halikadhalika kuna majengo mengine ambayo hayajakamilika. Ndiyo maana tumetoa maelekezo wiki iliyopita nimesema Halmashauri zote hata Mheshimiwa Mwambalaswa tulikuuliza kule Chunya kuwa Mkurugenzi atakuwa amepata waraka kutoka TAMISEMI, lengo letu ni nini, najua kuna mambo tumeyafanya lakini bado mapungufu yapo makubwa zaidi, tuweze kubainisha hizo changamoto tuzipangie mkakati wa pamoja sasa jinsi gani tutafanya kurekebisha matatizo haya hasa ya magofu ambayo hayajakamilika lakini kuhakikisha hadhi za hospitali zetu za zahanati ziwe sawa sawa. Nadhani mchakato huu utakuwa mpana sana ili kukidhi matakwa ya ilani ya Chama Cha Mapinduzi kama tulivyoahidi wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimuahidi Mheshimiwa Mwambalaswa kwamba tutakuunga mkono katika juhudi kubwa ulizozifanya katika Jimbo lako la Chunya na Halmashauri yako ya Chunya.

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Kituo cha Afya Chunya kilipandishwa hadhi kuwa hospitali ya Wilaya mwaka 2008 lakini kuna tatizo la ukosefu wa chumba cha kuhifadhia maiti:- Je, ni lini Serikali italitatua tatizo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Nkasi leo ina miaka 40 tangu ilipoanzishwa, lakini haina hospitali ya Wilaya, wala Serikali haina mpango wa kujenga hospitali ya Wilaya. Ni lini Serikali yetu itakuwa na azimio la kujenga hospitali ya Wilaya hasa katika Makao Makuu ya Wilaya katika Mji wetu wa Namanyere?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ninamfahamu Mheshimiwa Keissy kuhusu suala la tatizo la afya. Miongoni mwa mambo ambayo ninayakumbuka Mheshimiwa Keissy alipendekeza kituo kimoja kile cha afya kukipandisha grade kuwa hospitali ya Wilaya kama sikosei. Alizungumza hapa Bungeni kwamba kituo kile cha afya licha ya kuwahudumia wananchi wa Jimbo lake, wengine wanatoka katika nchi mpaka ya Congo. Hili nilisema siku ile kwamba Mheshimiwa Keissy jambo hili tumelichukua, katika mpango wa pili wa afya kila Halmashauri kuwa na hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Keissy naomba niseme tu kwamba tutaungana pamoja katika mipango kwa sababu tunajua Wilaya yako ipo pembezoni na ina changamoto nyingi. Tutajitahidi kwanza kuhakikisha kile kituo cha afya tunakiangalia na mimi nimekiri wazi kwamba nikija kwako lazima nikitembelee kituo cha afya, tutashawishi wenzetu wa Wizara ya Afya wakiangalie kama kimefikia vigezo kipandishwe kuwa hospitali ya Wilaya, tutakuunga mkono ili wananchi wa eneo lako lazima wapate afya. Jambo hili umelipigia kelele sana toka Waziri Mkuu wa mwanzo Mheshimiwa Peter Pinda nilikusikia ukilizungumza, nasema kwamba tupo pamoja katika hili.

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Kituo cha Afya Chunya kilipandishwa hadhi kuwa hospitali ya Wilaya mwaka 2008 lakini kuna tatizo la ukosefu wa chumba cha kuhifadhia maiti:- Je, ni lini Serikali italitatua tatizo hilo?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru kwa kuniona na mimi naomba niulize swali moja tu dogo la nyongeza;
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Wilaya hii ya Chunya ni mojawapo ya Wilaya kongwe sana Tanzania, lakini hospitali hii haina vifaa tiba wala matibabu ni kweli. Pia akina mama kwenye wodi ya wazazi wanapata shida mpaka wanajifungulia chini, naomba kujua Serikali ina mkakati gani kuiangalia jicho la ziada Wilaya hii kongwe nchini

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto ya vifaa tiba na siyo vifaa tiba tu maana yake kuna changamoto nyingi, ukienda kwenye vifaa tiba utakuta changamoto ya madawa, ndiyo maana katika mpango wetu wa sasa ninawashukuru sana wenzetu wa Wizara ya Afya ukiangalia mpango mkubwa tunaondoka nao, suala zima la vifaa tiba, madawa katika bajeti ya mwaka huu imeji-reflect kabisa ni jinsi gani tutafanya hasa hospitali zetu za Wilaya ziweze kuwezeshwa. Maelekezo makubwa tumeona hospitali nyingi sana mara nyingi zinasuasua katika suala la madawa na vifaa tiba na ndiyo maana mpango wetu mkakati sasa hivi ni kuhakikisha kwamba tunafanya collection ya kutosha, mara nyingi pesa zilikuwa zinakusanywa lakini siyo zile zinakusanywa zinaingia katika Halmashauri na hospitali, nyingi zilikuwa zinapotea.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana tumeasisi hii mifumo ya ki-electronic, hata mwanzo pesa zikikusanywa zilikuwa hazitumiki zote kwa matumizi ya hospitali, mengine watu walikuwa wanatumia kwa ajili ya kulipana per diem mwisho wa siku ni kwamba hata dawa na vifaa tiba vinakosekana. Kwa hiyo kutokana na mwongozo tumesema kwamba pesa zote zinazokusanywa katika hospitali za Wilaya ukiachia na mafungu mengine, lengo letu kubwa kwamba hii mifumo ya electronic tutakusanya fedha lakini lazima mwongozo ufuatwe. Je, asilimia ngapi inaenda katika vifaa tiba na asilimia ngapi inaenda katika dawa, mwisho wa siku tuweze kutatua tatizo la dawa na vifaa tiba katika hospitali zetu.
Hili Mheshimiwa Mwanjelwa tutaenda kulisimamia katika mwaka huu wa fedha ili kuongeze ufanisi katika hospitali zetu za Wilaya na hospitali zetu mbalimbali wananchi waweze kupata huduma.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Kituo cha Afya Chunya kilipandishwa hadhi kuwa hospitali ya Wilaya mwaka 2008 lakini kuna tatizo la ukosefu wa chumba cha kuhifadhia maiti:- Je, ni lini Serikali italitatua tatizo hilo?

Supplementary Question 4

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi nina swali dogo la nyongeza;
Kwa kuwa, wananchi wa Kijiji cha Majami, Kibolianana, Mlembule na Mgoma tayari wameshaonesha juhudi ya kujenga majengo ya zahanati, kilichobaki ni Serikali kusadia. Lakini Igodi Kusini, Isalanza jengo lipo tayari limekamilika pamoja na Igodi Kaskazini.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri utakuwa tayari kuwapelekea watu wa Igoji Kaskazini na Kusini huduma ya madawa na kusaidia hawa ambao tayari wameonesha nguvu za kujenga zahanati?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesikia kilio hiki na bahati nzuri Mheshimiwa Lubeleje kama ukifanya reference mwenyewe hili ni miongoni mwa maswali mengi sana aliyouliza katika sekta ya afya, Mheshimiwa Lubeleje nikuhakikishie kwamba katika eneo hilo kwanza ahadi zetu zile za kwanza ni lazima tutazitembelea zahanati hizi kuziangalia kama kuna changamoto tuweze kuzitatua; hali kadhalika tutafanya utaratibu jinsi ya upatikanaji wa dawa, kwa sababu nikijia Jimbo lako ni kubwa, maeneo yako ni makubwa. Nimefika katika sehemu wanaita Makutupa, kutoka Makutupa mpaka mtu anaenda kufuata huduma ya afya ni mbali sana. Kwa hiyo Mheshimiwa Lubeleje juhudi unayoenda kufanya endelea kuifanya, tutaunga mkono lakini lazima tu-visit tuangalie kama kuna changamoto nyingine tuweze kurekebisha, tuwaambie wataalamu wetu tuweze kufanya hata allocation ya wataalamu wa ndani na madawa tutafanya ili vituo hivi viweze kufanya kazi na wananchi waweze kupata huduma.