Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- (i) Je, ni lini ujenzi wa mradi wa katika Kata za Izimbya, Kyaitoke, Ruhunga, Mugajwale, Katoro na Kaibanja utaanza na kukamilika? (ii) Je, ni lini mradi wa maji wa Kata za Kemondo, Katerero na Bujugo utaanza na kukamilika? (iii) Je, ni lini mradi wa maji wa Kata za Karabagaine, Maruku na Kanyangereko utaanza na kukamilika?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi, majibu haya ni mazuri kuyasikia kwenye masikio na yanafurahisha, lakini siamini kama kuna ukweli wa kutosha kwasababu kwa mfano hili swali (c) kuhusu Mradi wa Maji Karabagaine nimewahi kuliuliza humu ndani majibu yakawa ni haya haya kwamba mradi huu utaanza, lakini mpaka leo haujaanza. Sasa leo nitaaminije kinachosemwa hapa ni kweli?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante nipende kujibu swali la Mheshimiwa Jasson Rweikiza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Wizara tupo katika mageuzi makubwa ya utekelezaji wa miradi mbalimbali na mradi kama huu wa Karabagaine ni mradi wa muda mrefu lakini ni katika ile miradi ambayo tayari tupo katika mpango wa kuona kwamba utekelezaji wake unafikia sasa mwisho.

Mheshimiwa Spika, hivyo nipende kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwa namna ambavyo ameshafuatilia kwa muda mrefu na jitihada kubwa namna ambavyo tumeweza kushirikiana pamoja nikuhakikishie mradi huu unakwenda kutekelezwa katika mwaka wa fedha huu 2021/ 2022 na itawezekana kwa sababu tumedhamiria kuleta mageuzi makubwa.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- (i) Je, ni lini ujenzi wa mradi wa katika Kata za Izimbya, Kyaitoke, Ruhunga, Mugajwale, Katoro na Kaibanja utaanza na kukamilika? (ii) Je, ni lini mradi wa maji wa Kata za Kemondo, Katerero na Bujugo utaanza na kukamilika? (iii) Je, ni lini mradi wa maji wa Kata za Karabagaine, Maruku na Kanyangereko utaanza na kukamilika?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa swali dogo la nyongeza; wewe ni shahidi mradi wa Bunda umechukua muda mrefu sana takribani miaka 13; lakini moja katika makubaliano kwenye mkataba wa mradi ule ni kujenga vitu kabla mradi haujafika Bunda Mjini kwenye eneo linalotoka kule Nyabeu.

Sasa nataka kuuliza maeneo yanayopita mradi kama Gushigwamara, Kinyambwiga, Tairo, Guta na Bunda Store kabla hayajafika centre; ni lini mtaweka vituo ili wale wananchi wa maeneo yale wasisikie tu mradi umetoka chanjo cha maji vijiji ambavyo vinapita havijapata maji? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ester Bulaya kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, sisi kama Wizara tayari tunaendelea na kuona kwamba maeneo ya miradi ambayo imekaa muda mrefu inakamilika, na sera ya maji inataka pale kwenye chanzo na kadri ambavyo mradi unakwenda tunaendelea kusambaza maji. Yule wa karibu ya chanzo ataendelea kupata maji kwa kwanza kulikoni aliyekuwepo kule mbali. Hivyo nikuhakikishie Mheshimiwa Ester Bulaya kwamba maeneo yote ambayo umeyataja yatazingatiwa katika kuona kwamba miundombinu ya usambazaji maji inawafikia. (Makofi)

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- (i) Je, ni lini ujenzi wa mradi wa katika Kata za Izimbya, Kyaitoke, Ruhunga, Mugajwale, Katoro na Kaibanja utaanza na kukamilika? (ii) Je, ni lini mradi wa maji wa Kata za Kemondo, Katerero na Bujugo utaanza na kukamilika? (iii) Je, ni lini mradi wa maji wa Kata za Karabagaine, Maruku na Kanyangereko utaanza na kukamilika?

Supplementary Question 3

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali.

Serikali imekamilisha mradi wa maji katika Mji wa Kateshi mradi wenye thamani ya shilingi bilioni 2.5 lakini mpaka sasa mradi huo haujaanza kufanya kazi.

Je, ni lini Serikali itaanza kusambaza maji ili wananchi wa mji wa Katesh lakini maeneo ya Mogito ambayo chanzo kimeanzia pamoja na maeneo mradi unapopita watanufaika na maji haya katika miji hii na kata hizi? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asia Halamga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mradi wowote ukishakamilika sisi kama Wizara tunapenda kuona maji yanawafikia wananchi kwenye vituo vya kuchotea maji, hivyo mara miundombinu yote itakapokamilika maji mara moja yataanza kutoka katika mradi huu wa Katesh. Tunafahamu tumeshatumia fedha nyingi za Serikali ambazo ni jasho la wananchi, hivyo hatuko tayari kuona fedha imeshatumika halafu kile tunachokitarajia kisipatikane. Pia niendelee kukupongeza Mheshimiwa Asia mwendo wako ni mzuri wewe unawakilisha vizuri vijana na sisi kama Wizara hatutakuwa kikwazo kuona kwamba unafika mbali. (Makofi)

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:- (i) Je, ni lini ujenzi wa mradi wa katika Kata za Izimbya, Kyaitoke, Ruhunga, Mugajwale, Katoro na Kaibanja utaanza na kukamilika? (ii) Je, ni lini mradi wa maji wa Kata za Kemondo, Katerero na Bujugo utaanza na kukamilika? (iii) Je, ni lini mradi wa maji wa Kata za Karabagaine, Maruku na Kanyangereko utaanza na kukamilika?

Supplementary Question 4

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kuniona kunipa swali la nyongeza.

Kwa kuwa katika miradi 28 ambayo inatakiwa ipelekewe maji na Mji wa Makambako ni miongoni katika miji hiyo 28; ni lini mradi huo utaanza katika mji wa Makambako?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sanga Mbunge wa Makambako kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, miradi yote ya miji 28 mpaka dakika hii taratibu zote zimeshakamilika hivyo wakati wowote ule miradi hii katika miji yote 28 tunakwenda kuanza kufanya kazi mara moja.