Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: - Je, ni lini Hospitali ya Kanda ya Kusini itaanza kutoa Huduma kwa Wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Ni kweli Hospitali hiyo ya kanda imeanza kutoa huduma, lakini lengo la Hospitali ya Kanda ni kutoa huduma za rufaa. Huduma hizo hazijaanza kwa sababu hakuna vifaa na hakuna madaktari bingwa. Sasa swali langu: Ni lini vifaa na madaktari bingwa wataletwa katika hospitali hiyo kwa sababu hiyo ndiyo shida yetu sisi watu wa kusini hususan Mkoa wa Mtwara? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili. Ukiangalia mazingira ya nje ya hospitali ile, bado yapo shaghalabaghala, ni lini yatawekwa katika mandhari ambayo inaendana na mandhari ya hospitali? Nakushukuru. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO (MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL): Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake zuri sana; na kweli mawazo mazuri aliyoyatoa ndiyo mwelekeo wa Serikali.

Mheshimiwa Spika, kwanza hospitali hiyo imeanza na ni kweli bado watumishi hawajafikia idadi aliyoisema. Tumegawa uanziswaji wa hiyo hospitali. Ukiangalia hospitali yenyewe sasa ina umri wa mwezi mmoja na siku nane, lakini tumegawa uanzishwaji wake kwa phase tatu, maana yake tumeanza phase ya pili ambayo sasa wanaenda kuwekwa watumishi.

Mheshimiwa Spika, tayari Serikali imetenga shilingi bilioni saba kwa ajili ya hospotali hiyo na tayari shilingi bilioni tatu zimeingia kwa ajili ya kununua CT-Scan na MRA. Kuna specialist mmoja na mwezi ujao wanapelekwa 4 ili wafikie 5. Mpaka mwezi wa Pili ambapo tutaenda kwenye Phase ya tatu ya uanzishwaji wa hospitali, tutakuwa na watumishi 217. Kwa hiyo, Mheshimiwa ukitembelea mwazi wa tatu utakuta imeanza kama ulivyotaka wewe.

Mheshimiwa Spika, swali la pili ni kuhusu mazingira ya Hospitali. Kweli nimeyaona na mimi wakati jiwe la msingi linawekwa, bado mazingira yaliyozunguka siyo safi. Wakati tunaendela kwenye phase hizi, tunaendelea kuhakikisha vile vile na usafi unafanywa.

Mheshimiwa Spika, OC imetengewa shilingi milioni 600. Kwa hiyo, watatumia kwa ajili ya kuhakikisha mambo mengine yanakuwa sawa na kufikia lengo ambalo Wana- Mtwara wangetegemea kuona.

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: - Je, ni lini Hospitali ya Kanda ya Kusini itaanza kutoa Huduma kwa Wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Spika nashukuru. Nami napenda kuiuliza Serikali: Ni lini itaimarisha utoaji wa huduma kwa magonjwa yale ambayo yalikuwa hayapewi kipaombele; magonjwa ya kitropiki, kwa maana ya neglected tropic diseases kwenye hospitali hii ya Kanda ya Kusini? Ahsante.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO (MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL): Mheshimiwa Spika, kwanza ukisikia tunaanzisha specialists mbalimbali, tunazungumzia magonjwa yote hayo. Ukisikia tunasema tunaongeza watumishi, ni kwa kuzingatia hayo. Ndiyo maanda unaona sasa kuzunguka nchi nzima, utaona kila Mkoa sasa unafanya wahamasa kuhusu magonjwa ambayo ameyazungumzia. Juzi Arusha nilimwakilisha Waziri wa Afya kwenye kuzindua swala hilo kitaifa. Ahsante. (Makofi)