Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali italeta Mwekezaji wa Kiwanda cha Saruji katika Wilaya ya Uvinza?

Supplementary Question 1

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishukuru Serikali kwa majibu yake mazuri, lakini pia ninalo swali moja la nyongeza; kwamba, Uvinza ndipo kunapopatikana malighafi ya kutengeneza saruji. Sasa nataka nijue Serikali imejipanga vipi kuhakikisha kwamba, kiwanda hicho kinajengwa ili wananchi waweze kupata ajira ya muda mfupi, lakini na muda mrefu na ili tuweze kukamata soko la DRC na Burundi? Ahsante.

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nashon William, Mbunge wa Kigoma Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mbunge kwa kufuatilia. Amekuwa anafuatilia sana kuhusiana na ujenzi wa kiwanda katika Wilaya ya Uvinza, lakini mkakati wa Serikali ni kuendelea kuboresha miundombinu wezeshi ili kuvutia wawekezaji zaidi katika ujenzi wa viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninyi ni mashahidi sasa hivi Kigoma itaenda kufunguka kwa sababu Mheshimiwa Rais wetu, Samia Suluhu Hassan, anaunganisha gridi ya Taifa ya umeme katika Mkoa huo. Maana yake hii ni miundombinu wezeshi ambayo ni muhimu sana kwa ajili ya ujenzi wa viwanda. Kwa hiyo, tunaamini kwa uboreshaji wa miundombinu hii wezeshi, pamoja na barabara tutavutia wawekezaji zaidi ambao watakuja kujenga pia katika Wilaya ya Uvinza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tunaendelea kufanya juhudi za makusudi ili kuvutia wawekezaji zaidi ambao watajenga viwanda katika ukanda huo wa ziwa ili kushika soko katika nchi za jirani, kama alivyosema. Nakushukuru sana.