Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwaongezea mkopo akina mama wajasiriamali wa Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 1

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwanza, naishukuru Serikali kwa majibu mazuri, lakini ripoti ya CAG mwaka 2020/2021 imeonesha kwamba fedha hizi zimekuwa nyingi zikipotea kutokana na kutorejeshwa ipasavyo: Je, Serikali inatoa tamko gani kuhakikisha fedha hizi zinarejeshwa ili ziweze kuwanufaisha wanufaika wengine?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Martha Festo Mariki, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli katika mwaka wa fedha 2020/2021 na miaka ya fedha ya nyuma ya mwaka wa fedha huo, kulikuwa na kasi ndogo ya urejeshaji wa fedha za mikopo ya asilimia 10, na Serikali ilitambua changamoto hiyo, tukachukua hatua; kwanza, kwa kuongeza usimamizi na uratibu wa mikopo pamoja na marejesho ya fedha hizo.

Mheshimiwa Spika, nilijulishe Bunge lako Tukufu sasa kwamba mwenendo wa marejesho wa fedha hizi kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 umeongezeka kwa takribani asilimia 84 sasa ikilinganishwa na miaka nyuma ambayo ilikuwa chini ya asilimia 50. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha tunaendelea kusimamia marejesho ya fedha hizi ili mfuko huu uendelee kuzunguka kunufaisha vikundi vingine.

Mheshimiwa Spika, nitoe tamko kwamba Wakurugenzi wa halmashauri zote kote nchini wahakikishe wanakopesha asilimia 10 kwa makundi yale kadri ya sheria, na wahakikishe wanarejesha fedha zile ili ziendelee kuwanufaisha wananchi wengine. Ahsante sana.

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwaongezea mkopo akina mama wajasiriamali wa Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 2

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa kuna kundi kubwa la watu ambao sio vijana, wenye umri wa miaka ya 35 hadi 45, wanaachwa sana na ni changamoto kwenye ajira, na bado wapo kwenye kundi la kuajiriwa na Serikali kwa maana hawajafikia ukomo.

Je, ni lini Serikali sasa itarekebisha hiyo sera au itatoa tamko kwamba sasa nao wale watu wapewe mikopo kupitia hiyo asilimia kumi, au kuongeza asilimia 10 ili kupunguza hili wimbi la ukosefu wa ajira? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Noah Lemburis Saputu, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba mikopo hii inatolewa kwa vijana ambao wana umri wa miaka 18 hadi 35 kwa mujibu wa definition ya vijana kwa utaratibu huu wa mikopo ya ten percent. Ni kweli kwamba kuna vijana ambao wana umri wa zaidi ya umri wa miaka 35 ambao pia wangeweza kunufaika na mikopo hii. Kwa hiyo, naomba niichukue hoja ya Mheshimiwa Mbunge tukaifanyie kazi na kuona uwezekano huo na pia kuona kama inaweza ikatekelezwa ama vinginevyo. Ahsante.

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwaongezea mkopo akina mama wajasiriamali wa Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 3

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa Halmashauri za SMT ndiyo zinasimamia mikopo kwa ajili ya vijana, akina mama na walemavu; na kwa upande wa Zanzibar vilevile Halmashauri za SMZ zinasimamia hivyo hivyo: -

Je, Mheshimiwa Waziri kwa sababu halmashauri za bara tayari zinafanya kazi hiyo, lakini halmashauri ya Zanzibar kisheria zinatakiwa nazo zifanye kazi hiyo; utazisaidia vipi ili halmashauri zile ziweze kuwasaidia akina mama nao waweze kujikwamua katika maisha?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Fakharia Khamis, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, usimamizi wa mikopo ya asilimia 10 kwa maana ya Tanzania Bara, unasimamiwa na halmashauri; na kama ambavyo amesema Mheshimiwa Mbunge kwamba Zanzibar pia inatakiwa isimamiwe na halmashauri lakini kuna changamoto.

Mheshimiwa Spika, naomba kama Serikali tuchukue hoja hiyo ili tuweze kukaa pamoja tuone namna gani tunaweza tukaboresha kwa upande wa Zanzibar pia ili huduma hiyo iweze kuimarika. Ahsante sana.