Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Mji wa Mangaka?

Supplementary Question 1

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Jimbo la Nanyumbu liko mpakani mwa Tanzania na nchi ya Msumbiji. Sisi sote ni mashahidi kwamba hali ya usalama sisi na ndugu zetu wa Msumbiji siyo nzuri kwa wakati huu. Majibu ya Serikali nayashukuru sana. Sasa swali kwa Mheshimiwa Waziri: -

Je, ni commitment gani ambayo unaitoa kwa wananchi wa Jimbo la Nanyumbu kuwahakikishia kwamba katika mwaka huo ujao wa fedha 2023/2024 watapata Kituo cha Polisi ili kuwa na uhakika na usalama wao na mali zao? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, commitment ni kiwango cha asilimia mia moja. Kama bajeti yetu itapitishwa mwezi Juni, uhakika ni kwamba Kituo cha Mangaka ni moja ya vituo vilivyopangwa kujengwa katika mwaka wa 2023/2024. Kwa hiyo, huo ni uhakika, naomba Mheshimiwa Mbunge asiwe na wasiwasi, ahsante sana. (Makofi)

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Mji wa Mangaka?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. naomba kuuliza swali dogo la nyongeza: -

Je, ni lini Serikali itaongeza majengo na kukarabati Kituo Polisi Masasi ambacho kilijengwa wakati wa ukoloni 1959?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongea la Mheshimiwa Hokororo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua vituo vilivyojengwa kabla ya uhuru kama hiki cha Masasi ni vya muda mrefu, vimechakaa, vinahitaji ukarabati. Kupitia Bunge hili namwomba IGP kupitia wasaidizi wake walioko mikoani waweze kufanya tathmini ya kiwango cha uchakavu wa Kituo cha Polisi ngazi ya Wilaya pale Masasi ili baada ya kubaini kiwango cha uchakavu kiweze kutengewa bajeti kwa ajili ya matengezo kulingana na mpango wetu wa matengezo na ujenzi wa vituo vyetu vya Polisi, nashukuru.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Mji wa Mangaka?

Supplementary Question 3

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, Tarafa ya Nyijundu tuna ujenzi wa Kituo cha Polisi, nami kama Mbunge nimeweza kushirikiana na wananchi hao kwa kuchangia matofali zaidi ya 2,000: Je, Serikali iko tayari kuchangia nguvu za wananchi ili tuweze kukamilisha kituo hicho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Nyanghwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo spirit ya Wizara kwamba pale ambapo wananchi na wadau wao wamejitokeza kuanza ujenzi wa vituo hivi vya Polisi kwa ajili ya usalama wetu, sisi tutawaunga mkono. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge kama ametoa matofali 2,000 na wadau wengine wametoa na ujenzi umeanza, basi katika ukamilishaji tutawanga mkono. Wakati wowote mtakapokuwa mmefikia hatua ya ukamilishaji, tafadhali tuwasiliane ili tuweze kukuunga mkono kituo hicho kikamilike na kuanza kazi, ahsante.