Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Upembuzi yakinifu wa barabara ya kutoka Nyololo hadi Mtwango yenye urefu wa kilomita 40 umefanyika mwaka 2013/2014:- Je, ni lini barabara hiyo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, hii barabara ni ya muhimu sana na ni ya miaka mingi sana na bahati nzuri sana hata Naibu Waziri wa Ujenzi mwaka 2015 alifika kule Mufindi na alifanya mikutano miwili na aliwaambia wananchi kwamba, baada ya kumaliza uchaguzi hii barabara itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kufuatana na umuhimu wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapoongelea viwanda, viwanda kule tayari viko, kuna kiwanda cha Kibwele pale, kuna kiwanda cha Kilima Factory, kuna kiwanda cha Lugoda factory, hivi ni Viwanda vya Chai na vinategemea hii barabara. Mheshimiwa Waziri aniambie kwa sababu upembuzi yakinifu walishamaliza na Serikali iliahidi na Chama cha Mapinduzi kimeahidi kwamba kitaweka kiwango cha lami. Ni lini hizi fedha zitapatikana na wataanza kujenga kwa kiwango cha lami?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wananchi walishaambiwa tayari kuna nyumba zao zilishawekewa alama ya X na wanatarajia kuhama! Je, Serikali ni lini itaenda kutoa fidia kwa wale ambao walijenga nyumba jirani na barabara na Serikali ilisema itawalipa fidia kwa mfano, wananchi wa Kijiji cha Nzivi, Igowole, Kibao, Mtwango na pale Lufuna, kuna nyumba ziliwekewa X, Serikali itaenda kuwalipa lini ili waanze kuhama?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii. Tunapoongelea ujenzi ni pamoja na fedha za fidia pamoja na fedha za ujenzi wenyewe. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama ambavyo barabara hii ipo katika ahadi ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015/2020, namhakikishia ahadi hiyo itatekelezwa, asiwe na wasiwasi!

Name

Saumu Heri Sakala

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Upembuzi yakinifu wa barabara ya kutoka Nyololo hadi Mtwango yenye urefu wa kilomita 40 umefanyika mwaka 2013/2014:- Je, ni lini barabara hiyo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa tatizo la barabara lipo nchi nzima na katika Jimbo letu la Pangani pia tatizo hili la uharibifu wa barabara limekuwa ni sugu. Licha tu ya barabara inayounganisha Wilaya ya Pangani na mikoa mingine kuwa mbovu, lakini pia barabara zinazounganisha vijiji na vijiji zimekuwa mbovu kiasi ambacho kipindi cha mvua hazipitiki kabisa. Je, Serikali ina mpango gani sasa kuhakikisha barabara zile zinapitika kipindi chote cha mwaka?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu itahakikisha ubora wa hizi barabara unaongezwa na unaimarishwa na tutaweka mipango maalum kuhakikisha magari makubwa ambayo mara nyingi ndiyo yanayoharibu barabara hizi hayataruhusiwa kupita katika barabara ambazo haziruhusu kupita magari yenye kiwango fulani cha tonnage.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, barabara hii anayoiongelea iko katika Ilani yetu na tutaendelea kuiimarisha na nichukue fursa hii kuwaomba au kuwaelekeza TANROADS, Mkoa wa Tanga kuhakikisha kwamba, kama ambavyo tuliwapa maelekezo kufungua barabara zingine na hii wahakikishe inafunguliwa na maeneo hayo yote yaliyoharibika yatengenezwe.