Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatenga fedha za ujenzi wa kiwango cha lami kwa barabara ya Mziha – Kibindu – Mbwewe?

Supplementary Question 1

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Spika, nashukuru pamoja na majibu ya Serikali ambayo pamoja na kwamba hayatoi matumaini ya karibuni, lakini napenda nitumie fursa hii kuishukuru sana Serikali kwamba barabara hii iko chini ya TANROADS kwa matengenezo ambayo yanaendelea inawezesha walau kupitika na barabara hii ni shortcut kwa ajili ya kutoka Magila – Turiani – Mziha - Handeni - Mziha, Kibindu -Mbwewe kwenda Mikoa ya Kaskazini.

Mheshimiwa Spika, sasa naomba niulize maswali yangu kama yafuatavyo; je, Serikali ipo tayari kuielekeza TANROADS katika matengenezo yanayoendelea kutenga pesa kwa ajili ya matengenezo ya mifereji, kwa sababu eneo hili lina mvua nyingi ili barabara hii iendelee kupitika na kwa kuwa kuna vyakula vingi katika eneo hilo ili uweze kufika sokoni?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; kwa kuwa Serikali imepanga mpango mzuri wa kuendelea na upanuzi wa ujenzi wa njia sita kutoka Kibaha mpaka Chalinze na ilishafanya tathmini; je, Serikali inasemaje ina mpango gani juu ya fidia kwa maeneo ambayo barabara hiyo itapita? Ahsante sana.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Subira Khamis Mgalu, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii kwanza ina umuhimu mkubwa sana kwa mikoa hii yote miwili ya Morogoro pamoja na Pwani, na katika mwaka huu wa fedha ili iweze kupitika tumetenga fedha takribani kiasi cha shilingi milioni 346.981 na wakandarasi wawili wapo site.

Kwa hiyo, nimhakikishie Mbunge kwamba suala la ujenzi wa mifereji pia tutajenga kwa kuwa tayari wakandarasi wako site ni sehemu ya scope ya kazi tuliyompatia mkandarasi.

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa ajili ya barabara kutoka Kibaha – Chalinze kuja Morogoro kwa ajili ya fidia, tayari barabara hii wizara imekusudia tutafanya kwa mfumo wa EPC+Finance, lakini sasa tumebadilisha kwa tutafanya kwa njia ya Public Private Partnership (PPP). Tayari mtaalam mwelekezi Kampuni kutoka Korea ya Kusini yupo site na tunategemea tutakabidhi kazi hii kati ya mwezi wa tatu ama wa nne na kupitia ripoti atakayoleta kwa ajili ya fidia na gharama zote, Serikali itatumia hiyo ripoti kwa ajili ya kulipa wale wote watakaokuwa wameathirika na barabara hii, ahsante.