Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Vifaa Tiba katika Hospitali ya Ilongero pamoja na Vituo vya Afya vya Msange na Mgori Wilayani Singida?

Supplementary Question 1

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu ya kutia matumaini ya Serikali awali ya yote kwanza nitoe pole kwa wananchi wa Jimbo la Singida Kaskazini kufatia ajali mbaya iliyotokea juzi na kuuwa wananchi wanne hapo hapo na majeruhi 20 lakini hawakuweza kupatiwa matibabu kwa wakati na ipasavyo kwa sababu ya kukosa vifaa tiba katika hospitali zetu. Lakini...

SPIKA: Mheshimiwa Mbunge ngoja tuelewane vizuri, kwanza ni kipindi cha maswali, pili unaongeza hoja hapo kwamba hawakupatiwa matibabu, hiyo ni hoja nzito sana, unao ushahidi ama huna? Kama huna hebu jielekeze kwenye maswali ondoa hiyo habari nyingine kabisa, kwa sababu tusije tukahama kwenye maswali tukaelekea kuanza kushughulika na hiyo hoja kwamba walifariki kwa sababu hawajapatiwa matibabu, hiyo ni hoja nzito sana kuletwa hapa Bungeni.

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, maswali yangu mawili madogo ya nyongeza. Kwanza, ni lini tutapatiwa ambulance katika hospitali hizi ili kurahisisha huduma kwa wananchi wetu wanaopata magonjwa mbalimbali na mengine ya ghafla kama ajali?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, ni lini sasa Serikali itapeleka watumishi wa kutosha katika vituo hivi vya afya pamoja na hospitali ya wilaya ili waweze kutoa huduma kwa wakati na ipasavyo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Abeid Ramadhani Ighondo, Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na suala la ambulance katika bajeti inayokwisha mwaka huu tarehe 30 Juni, Serikali imetenga magari ya wagojwa 195 na kila halmashauri itapata gari la wagonjwa ikiwepo halmashauri ya Singida ambayo tutapeleka kwenye hospitali hii. Kwa hiyo nimhakikishie kwamba suala hilo tayari linafanyiwa kazi na gari ya wagonjwa itapelekwa.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na watumishi ni kweli tuna upungufu wa utumishi, lakini Serikali imetoa kibali tayari hivi sasa vijana wanaendelea kuomba ajira ya watumishi wa kada mbalimbali za afya 7,612 na miongoni mwa watumishi hao watapelekwa katika Wilaya ya Singida.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Vifaa Tiba katika Hospitali ya Ilongero pamoja na Vituo vya Afya vya Msange na Mgori Wilayani Singida?

Supplementary Question 2

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa Serikali imeleta milioni 500 kumalizia ujenzi wa Hospitali za Halmashauri ya Kibiti, Kibaha Mjini, Kibaha Vijjini na bilioni moja Halmashauri ya Chalinze. Je, Serikali inatoa ahadi gani kwa wananchi wa maeneo hayo juu ya kuleta vifaa tiba kwa wakati ili iendane na jitihada hizi za uwekezaji?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Subira Mgalu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali kwa kutambua umuhimu wa huduma za afya kwa wananchi wa Kibiti na wananchi wa Chalinze imepelekwa jumla ya shilingi bilioni moja na milioni mia tano kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya na hospitali. Hata hivyo, nimhakikishie mara baada ya kukamilika kwa vituo hivi Serikali itapeleka vifaa tiba kwa sababu katika bajeti ya mwaka ujao shilingi bilioni 69.95 imetengwa kwa ajili hiyo.

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Vifaa Tiba katika Hospitali ya Ilongero pamoja na Vituo vya Afya vya Msange na Mgori Wilayani Singida?

Supplementary Question 3

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba na watumishi katika zahanati ya Mwashilalage katika Jimbo la Sumve ambayo ujenzi wake umeshakamilika kwa muda sasa na mahitaji ya watumishi na vifaa tiba ni ya hali ya juu kutokana na kwamba kata nzima ya Sumve haina zahanati yoyote?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kasalali Mageni, Mbunge wa Jimbo la Sumve, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na vifaa tiba na watumishi vyote viko kwenye mpango na viko tayari. Watumishi wanaendelea kuajiriwa hivi sasa na matarajio ya Serikali ifikapo Julai, watumishi watapelekwa kwenye vituo vyetu na tutahakikisha tunatoa kipaumbele kwenye zahanati ambayo Mheshimiwa Mageni Kasalali ameongelea.

Mheshimiwa Spika, pili, kuhusiana na vifaa tiba mwaka ujao wa fedha tumetenga 69.95 bilioni kwa ajili ya vifaa tiba na tutahakikisha pia vinapelekwa kwenye zahanati hiyo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja.

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Vifaa Tiba katika Hospitali ya Ilongero pamoja na Vituo vya Afya vya Msange na Mgori Wilayani Singida?

Supplementary Question 4

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Kituo cha Afya cha Chalangwa kimekamilika muda mrefu pamoja na jengo la Mochwari limekamilika, lakini mpaka sasa hivi hakuna majokofu wala vifaa tiba: Je, Serikali inatuahidi nini kupeleka vifaa tiba hivi pamoja na jokofu kwenye Kituo cha Afya cha Chalangwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Masache Kasaka Mbunge wa Jimbo la Lupa kama ifuatavyo: -

Ni kweli kwamba Kituo cha Afya cha Chalangwa kimekamilika na ni miongoni mwa vituo afya ambavyo vimetengewa fedha ya vifaa tiba mwaka ujao 2022/2023 ikiwemo jokofu kwa ajili ya chumba cha kuhifadhia maiti.