Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. SUSAN L. A. KIWANGA (K.n.y. MHE. OMARY T. MGUMBA) aliuliza:- Vijana ndio nguvu kazi kubwa katika Taifa letu na Serikali haina uwezo wa kutoa ajira kwa vijana wote kwa sasa:- (a) Je, Serikali itawawezesha kifedha vijana wa vijiji vyote 64 vya Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki katika makundi ili waweze kujiajiri wenyewe na kupunguza tatizo la ajira na umasikini wa vijana na akina mama? (b) Je, ni lini Serikali itaanzisha kituo maalum cha kuwawezesha vijana kupata sehemu ya kujifunzia kwa vitendo shughuli mbalimbali za ujasiriamali na kupata taarifa mbalimbali za maendeleo?

Supplementary Question 1

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini Wilaya ya Morogoro Kusini mpaka hivi sasa, hata hivyo vikundi alivyovizungumzia hapa; na kwa kuwa, Wilaya hiyo haina Makao Makuu ya Wilaya, wanaripoti Morogoro Mjini, kwa hiyo, inakuwa ngumu vijana hawa kufuatilia hizo fedha anazosema; na kutokana na idadi na umasikini wa wananchi wa Morogoro Vijijini, kwa kweli, kasi ya Serikali katika kuwawezesha vijana imekuwa ndogo sana kutokana na ukubwa wa Wilaya hiyo ambapo haina Ofisi ya Wilaya.
Je, Serikali ni lini sasa itaweka Ofisi ya Halmashauri ndani ya Wilaya ya Morogoro Vijijini ili vijana hao waache kuhangaika na kufuatilia masuala yao ndani ya Wilaya yao badala ya kukimbilia Morogoro Mjini ambako ni mbali na Wilaya yao? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kwa kuwa matatizo ya vijana Wilaya ya Morogoro Mjini na Wilaya ya kilombero, hususan Jimbo la Mlimba yanalingana; mara nyingi katika hii Mifuko ya Vijana ukitaka kuangalia ufuatiliaji wake, kwanza Halmashauri hazipeleki hizo hela. Mara nyingi Wabunge wengi ndani ya Bunge hili wamelalamika kwamba pesa hizo haziwafikii vijana.
Je, Serikali ina mpango gani sasa kwa kusudio la kuhakikisha hela zinazotengwa kwa ajili ya vijana ambapo hazitengwi na Wakurugenzi kuweka kipindi maalum kulipa madeni ya nyuma na kuendelea kutoa zile asilimia ili vijana wengi wapate kujiajiri wenyewe katika awamu hii?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, agenda ya kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro haina Ofisi ni kweli. Swali hili nadhani nimelijibu wiki iliyopita hapa na nimetoa ufafanuzi wa kina kuhusu swali hili; na tumesema mchakato hivi sasa unaendelea wa ujenzi kule. Lengo kubwa, ni kweli watu wanaotoka maeneo ya mbali kabisa; kwa mfano mimi mwenyewe nilienda Morogoro Vijijini yapata karibuni mwezi uliopita, ukitoka maeneo ya Mvuha mpaka kufika mjini changamoto kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeshatoa maelekezo kwamba mchakato ufanyike kwa haraka ilimradi wananchi wale wa Morogoro Vijijini kama Swali la Msingi alilouliza Mheshimiwa Tebweta, wiki iliyopita nilivyokuwa nikilifafanua.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala zima la uwezeshaji wa vijana, ni kweli, nanyi mnakumbuka hapa mwaka 2015 katika mchakato wetu tulipitisha mpaka Baraza la Vijana. Lengo kubwa ni kuona jinsi gani vijana waweze kufanyiwa kazi. Katika Bajeti ya mwaka huu wa fedha, ninyi Waheshimiwa Wabunge mnakumbuka, katika kikao chetu kilichopita cha Bajeti, tulitenga mafungu katika maeneo matatu tofauti.
Katika Wizara ya Habari na Vijana, kipindi kile tulitenga karibu shilingi bilioni moja katika bajeti, halikadhalika Waziri wa Utumishi alipokuja hapa eneo kubwa la concentration jinsi gani vijana wanaomaliza vyuo wanakosa ajira, Serikali ilitenga takribani bilioni 233, lengo likiwa ni kuajiri waajiriwa wapya wapatao 71,408.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hili nini kimefanyika hivi sasa? Siku mbili zilizopita hapa, Mheshimiwa Angellah Kairuki alizungumzia kwamba sekta ya afya peke yake itaajiri takriban wafanyakazi wapatao 10,870. Katika changamoto ya kuajiri walimu wapya, tunatarajia kuajiri walimu wapatao 40,000 ambao idadi katika bajeti ile ya shilingi bilioni 233, lengo kuwa ni kuwaajiri wafanyakazi wapya ambao ni vijana wapatao 71,408. Hii ni ajenda kubwa sana ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwaambie ndugu zangu, tatizo hasa la kukosa 5% kwa vijana na akinamama, changamoto hii inatukabili sisi Wabunge. Kwa sababu own source inajadiliwa katika vikao vya Mabaraza ya Madiwani na sisi ni miongoni mwa Wajumbe katika Mabaraza ya Madiwani. Own source haiji TAMISEMI wala haiji Wizara ya Fedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, kinachofanyika nini? Collection imefanyika ndani ya Halmashauri; Kamati ya Huduma za Jamii na Kamati ya Uchumi inakaa, baadaye Kamati ya Fedha; ninyi mnajua mwezi huu tumekusanya shilingi milioni 100 na wewe Mbunge upo na unafanya decision. Naomba niwaambie ndugu zangu, Taarifa ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali, katika report yake aliyo-submit mwezi wa nne imeonesha kwamba takriban shilingi bilioni 38.7 ambazo zinawagusa akina mama na vijana hazijapelekwa katika makundi hayo, lakini sisi ndio wa kufanya maamuzi hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwape changamoto ndugu zangu, hili jukumu ni la kwetu sisi sote. Kila Mbunge katika Kamati ya Fedha aende akasimame, own source zinazokusanywa ahakikishe 5% kwa vijana na akina mama inakwenda kwa ajili ya kuokoa uchumi wa vijana wetu. Katika hili tutawekeza ajira pana sana ya vijana wetu kwa sababu. Kwa sababu shilingi bilioni 38; sasa hivi tuna Halmashauri 181, takriban kila Halmashauri ikitoa shilingi milioni 100 ambayo collection ikiwasilishwa shilingi bilioni moja kwa mwaka, maana yake nini? Kwa Halmashauri 181 maana yake kuna shilingi bilioni 181 ilibidi ziende kwa vijana na akinamama.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwasihi Wabunge wenzangu, sasa tufanye mabadiliko ya kweli kuwakomboa Watanzania. Mabadiliko haya yataanza na sisi na Wenyeviti wetu wa Halmashauri na Madiwani wetu kuhakikisha own source ya 5% kwa vijana na akina mama inakwenda kwa ajili ya mustakabali wa nchi yetu. (Makofi)

Name

Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. SUSAN L. A. KIWANGA (K.n.y. MHE. OMARY T. MGUMBA) aliuliza:- Vijana ndio nguvu kazi kubwa katika Taifa letu na Serikali haina uwezo wa kutoa ajira kwa vijana wote kwa sasa:- (a) Je, Serikali itawawezesha kifedha vijana wa vijiji vyote 64 vya Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki katika makundi ili waweze kujiajiri wenyewe na kupunguza tatizo la ajira na umasikini wa vijana na akina mama? (b) Je, ni lini Serikali itaanzisha kituo maalum cha kuwawezesha vijana kupata sehemu ya kujifunzia kwa vitendo shughuli mbalimbali za ujasiriamali na kupata taarifa mbalimbali za maendeleo?

Supplementary Question 2

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la Morogoro Kusini Mashariki linafanana na tatizo la Mbinga Mjini, hasa maeneo ya Mbinga „A‟, Mbinga „B‟, Ruwiko, Bethlehemu na kadhalika; ile 5% inayotolewa kwa ajili ya vijana, pamoja na kwamba inaonekana inawasaidia vijana na maeneo mengine haiwafikii, bado inaonekana ni hela ndogo sana ukilinganisha na mahitaji ya vijana na hasa ukizingatia mabenki yetu hayajawa marafiki kwa vijana.
Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza, ukiondoa ile 5% inayotoka kwenye Halmashauri, Serikali Kuu kutengeneza fungu maalum kwa ajili ya kuwasaidia vijana, hususan vijana wa Mbinga? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Naibu Spika, swali la Mbinga kwa vijana, nadhani mnafahamu. Katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ambapo wananchi wote wameipa ridhaa Serikali ya Chama cha Mapinduzi, imeonesha kwamba kwa kila kijiji kitatengewa shilingi milioni 50. Lengo kubwa ni kwa ajili ya kuwawezesha vijana na akina mama katika vikundi waliojiunga katika SACCOS.
Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba ndugu yangu Mheshimiwa Sixtus Mapunda, najua ni mpiganaji sana wa Mbinga. Tushirikiane katika hili tuhakikishe hizi collection zinapatikana, lakini twende huko tukazisimamie, mwisho wa siku vijana wapate mahitaji yao kwa ajili ya kukuza uchumi wao.