Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: - Je, kuruhusu Benki kuwa Wakala wa Bima Serikali haioni kuwa Mawakala wengine watafunga biashara kwa kukosa wateja?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Kiuhalisia, ongezeko la Mawakala wa Bima linatokana na vijana wengi waliomaliza elimu ya fani ya bima nchini kuamua kujiajiri wenyewe baada ya kukosa kazi Serikalini: -

Mheshimiwa Spika, je, ni utafiti gani wa kina ambao umefanyika na Serikali hadi kujua kwamba ongezeko hilo linatokana na mfumo wa biashara ya bima kukua?

Mheshimiwa Spika, je, ni utafiti gani ambao mmeufanya katika kujua mawakala vijana ambao wamefunga biashara baada ya kushindwa biashara kutokana na ushindani mkubwa wa biashara ya bima ambao umevamiwa na benki pamoja na kampuni za simu? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, namshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa maswali mazuri. Moja, hivi tunavyoongea mpaka sasa, upande wa masuala haya ya bima hapa nchini ziko takribani asilimia 16 tu, ndiyo tunapata ushiriki wa vijana ambao wako chini ya umri wa miaka 18 na utafiti huo uliofanywa na Finscope ulionesha hivyo. Sasa katika nchi ambazo zimeendelea na kule tunakoelekea tunatamani angalau tufike asilimia 84 au zaidi ya hapo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu utafiti wa mawakala, taarifa ambazo zilikusanywa kwa miaka kadhaa kama nilivyotoa pale mwanzo, zinaonesha kwa mwaka 2020 walikuwa zaidi ya 700, lakini kwa sasa tumeshazidi 930. Kama tumeshazidi 930 hii inaonesha kwamba bado pana fursa ambapo vijana wote wanaweza wakashiriki na bado mafanikio yakapatikana bila wao kuzuiliwa kwa sababu ya uwepo wa BenkiWakala.

Mheshimiwa Spika, hivyo hivyo, TIRA ilishatoa mwongozo ambao unaweka mipaka ambayo inaonesha ni namna gani italinda BenkiWakala zisilete athari kwa Mawakala hawa wa kawaida ambao wanaendesha shughuli hizo. Tunaamini kwamba biashara hiyo itaendelea kusambaa zaidi kwa wananchi walio wengi zaidi. (Makofi)