Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufungua vituo vingi zaidi vya kuuza gesi asilia?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; Serikali sasa ina mpango gani wa kuendelea kujenga vituo hivyo vya kuuza gesi asilia katika mikoa ya mingi Tanzania hususani Mkoa wa Rukwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Serikali sasa imejipangaje kupunguza bei ya vifaa vinavyotumika kurekebishia mfumo wa magari kwenye mafuta na kwenye kit ya kujazia gesi? Ahsante. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bupe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kwenye jibu la msingi kama nilivyosema Serikali imejipanga vipi kuongeza Vituo vya Kujaza (CNG), tayari vibali kwa wakandarasi na wawekezaji 20 vimetolewa kwa ajili ya kwenda katika maeneo mbalimbali kuweza kuongeza wigo wa eneo hili. Tunaendelea kuvutia wawekezaji mbalimbali waje kuwekeza katika eneo hili la gesi asili ambalo litakuwa linatumika katika maeneo mbalimbali. Kwa hiyo michakato hiyo inaendelea na Serikali katika mwaka huu wa fedha itajenga hivyo vituo vyetu viwili ambao tunaamini kabla ya mwaka huu wa fedha kwisha vitaanza utekelezaji wake maeneo ya Mlimani City na maeneo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali la pili, Serikali inafanya nini kuhakikisha bei ya hizi zinazoitwa conversion kits zinapungua. Mojawapo ya kitu tunachokifanya tunahamasisha watu wengi wanaoweza kuja katika biashara hii ya kutengeneza conversion kits waje, biashara ikisha kuwa na watu wengi wanaoshiriki automatically ushawishi utakuwa ni mkubwa na gharama tunatarajia zitapungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile pia tumewaza namna ambayo tunaweza tukashirikiana na wenzetu wa Wizara

nyingine za Kisekta, Wizara ya Fedha na wengine kuona namna ya kuweka fedha au punguzo la kodi kwenye vifaa hivi kwa watalam watakavyoshauri ili tuone namna ambavyo tunaweza tukapunguza gharama za hizi conversion kits ili kuweza kuvutia watu wengi zaidi kuweza kuingia katika eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo la mwisho, tayari vituo vinavyouza gesi vimeweka utaratibu wa kukopesha wale wanaokuwa na haya magari wanaotaka kufanya conversion kit wanawakopesha na wanakuwa wanalipa kidogo kidogo kwa sharti la kwenda kuchukua gesi katika kituo chake hizo zote ni mbinu katika kuhakikisha kwamba gharama zinapungua na watumiaji wanaweza kupatikana kwa wingi.