Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nancy Hassan Nyalusi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme katika Vijiji Nane vya Wilaya ya Mufindi ambavyo havijapata umeme?

Supplementary Question 1

MHE. NANCY H. NYALUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Tunaishukuru Serikali kwa utekelezaji, hata hivyo, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je, ni lini Serikali itakamilisha kupeleka umeme katika Kijiji cha Idunda na Funuti, Kata ya Kimara katika Wilaya ya Kilolo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; je, ni lini Serikali itaanza kusambaza umeme katika Vitongoji Mkoani Iringa? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili nyongeza la Mheshimiwa Nancy Nyalusi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika jibu la msingi Vijiji vya Mufindi vitakamilika mwezi wa Sita mwaka huu kwa mujibu wa Mkataba, lakini vijiji vingine vyote nchini kama alivyovitaja yeye vya Kilolo kabla ya Desemba mwaka huu vitakuwa vimefikishiwa umeme kwa mujibu wa mkataba wetu tuliokuwa nao kwenye REA three, round two. Kwa hiyo nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Nyalusi pamoja na Waheshimiwa wengine, kwamba jambo hili tunalisimamia kwa karibu zaidi kuhakikisha kwamba umeme unafika katika Vijiji vyote kabla ya mwaka huu kuisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye eneo la pili, tunaendelea kutafuta pesa ambayo itatuwezesha kupeleka umeme katika vitongoji vyote karibu 36,000 tulivyokuwa navyo nchi nzima katika miaka minne, mitano inayokuja kwa gharama ya Sh.6,500,000,000,000. Taratibu za kutafuta fedha hizi zinaendelea na zitakapokuwa tayari, basi zitaletwa kwa umma hili kazi hii iweze kufanyika na kuhakikisha vitongoji vyote vinapata umeme. (Makofi)

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme katika Vijiji Nane vya Wilaya ya Mufindi ambavyo havijapata umeme?

Supplementary Question 2

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mwezi Desemba Meneja Mkoa wa Iringa ndugu yangu Jumbe aliniahidi kupeleka umeme katika Kijiji cha Usengerenidete, mpaka sasa nimeshapelekwa kwenye vyombo vya habari mara nne, je, ni lini sasa TANESCO watatoa angalau fedha za dharura kutoka Makao Makuu watupelekee hili hao wananchi wapate umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jackson Kiswaga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ameomba yeye mwenyewe fedha za dharura na jambo hili nilikuwa sijalipata naomba baada ya session hii ya maswali, niende kwake tukajadiliane, nijue tatizo ni nini na tuweze kulitatua tatizo hilo ili wananchi waendelee kupata huduma hiyo ya umeme. (Makofi)

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme katika Vijiji Nane vya Wilaya ya Mufindi ambavyo havijapata umeme?

Supplementary Question 3

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa fursa ya swali dogo la nyongeza. Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa REA ndani ya Mkoa wa Rukwa speed yake ni ya kusuasua sana, hususani ndani ya Jimbo langu la Kwela kufikia mwezi Machi katika vijiji 54 alikuwa amewasha vijiji tisa. Nataka kujua comittment ya Serikali leo ili wana Rukwa na Jimbo la Kwera wajue nini hatima yao kupata umeme? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deus Sangu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe comittment ya Serikali kwamba ile mikataba yote ambayo ilitakiwa kwisha Desemba mwaka huu kwa wale wakandarasi ambao wanaendelea na kazi hizi, tutaendelea kuwasimamia kwa karibu zaidi. Tumeshawekeana deadline na timeline za mambo mbalimbali na wale ambao wanaendelea kuzikiuka taratibu ambazo tunazichukua za kisheria watazipata muda si mrefu. Kwa hiyo niwahakikishie kwamba watapata umeme kabla ya muda wa mkataba kwisha na wale ambao watashindwa tutachukua hatua mapema ili tuweze ku– rescue situations kupata wakandarasi wengine ambao watakamilisha upelekaji wa umeme katika miradi ambayo tumekubaliana.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme katika Vijiji Nane vya Wilaya ya Mufindi ambavyo havijapata umeme?

Supplementary Question 4

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa, zoezi la upelekaji umeme kwenye Miji na maeneo yanayofanana na Vijiji bado haijakamilika kama inavyotakiwa.

Je, ni lini, Serikali itahakikisha maeneo yote yaliyoko Mijini hasa kwenye Kata za Buhongwa, Runhima na Kishili yanapata umeme uliokusudiwa kwa wakati na wananchi waweze kufaidi matunda hayo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Stanslaus Mabula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli zimekuwepo awamu mbili za kupeleka umeme kwenye maeneo ya Mijini yenye picha ya Vijiji ambayo tunaita miradi ya peri-urban, katika Jiji letu la Mwanza awamu ya kwanza ilifika ambayo iligusa pia, maeneo ya Dar es Salaam, Arusha na Mwanza. Ipo awamu ya pili ambayo ilikuja Dodoma na Mbeya na sasa iko awamu ya tatu ambayo kuna baadhi ya maeneo tayari imeshaanza kufanyika, Mkoa wa Kagera Jimbo la Bukoba Mjini likiwa ni mojawapo Geita, Mbeya tena Tanga na maeneo mengine ambayo yana uso wa Vijiji lakini yako Mjini yanaendelea kupelekewa umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamuahidi Mheshimiwa Mabula pamoja na Waheshimiwa Wabunge wengine ambao Majimbo yao yako Mjini kwamba miradi hii inaendelea kufanyika kadri ya upatikanaji wa fedha awamu kwa awamu. Pale ambapo tunapambana kuhakikisha kwamba REA III round II inakamiliishwa kwenye vijiji, vivyo hivyo ndivyo tunavyopambana kutafuta pesa kwa ajili ya kupeleka umeme katika maeneo ya Mijini lakini yenye uso wa Vijiji.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme katika Vijiji Nane vya Wilaya ya Mufindi ambavyo havijapata umeme?

Supplementary Question 5

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Serikali ina mkakati gani wa kuongeza Mkandarasi katika Wilaya ya Kahama yenye Halmashauri mbili Ushetu pamoja na Msalala kutokana na aliyepo kupeleka umeme kwa kusuasua sana?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cherehani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkandarasi anaepeleka umeme katika Wilaya ya Kahama ni Mkandarasi anayeitwa Tontan ambaye tunakiri ana mapungufu na hasa katika kazi yake anayoifanya Tanga na tumewekeana masharti ya kutimiza, akishindwa kuyatimiza mwezi huu wa Nne hautaisha ataondoka site zetu ili tuweze kupata Mkandarasi mwingine wa kupeleka umeme katika maeneo hayo. Kwa hiyo wananchi wa Kahama ninawaahidi kabisa kwamba umeme katika maeneo yao utapelekwa na utakamilika kwa wakati kwa sababu ni jambo linalotakiwa kukamilika kwa wakati.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha usambazaji wa umeme katika Vijiji Nane vya Wilaya ya Mufindi ambavyo havijapata umeme?

Supplementary Question 6

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali. Pamoja na Mkandarasi anayetekeleza kazi kwa Jimbo la Mbulu Vijijini kusuasua, sasa ameanza kuweka nguzo katika kila Kijiji, vingine nguzo 12, 13 na 15.

Je, ni kiasi gani cha nguzo kinatakiwa kiwekwe kila Kijiji ili sisi tusimamie?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatei, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, pesa iliyokuwa imepatikana katika awamu ya kwanza ya REA III round II ilikuwa unawezesha nguzo takribani 20 kupelekwa katika kila Kijiji, lakini tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alisikia kilio cha Watanzania na akatafuta pesa ya ziada na kuongeza, kwa hiyo kila Kijiji kitapata takribani kilomea Tatu ambazo ni 20 mara Tatu maana yake karibia nguzo 60 katika awamu hiyo inayokuja ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ninawaahidi Waheshimiwa Wabunge wote kwamba kutoka nguzo 20 sasa tutapata nguzo 60 katika kila Kijiji kwa ajili ya kuongeza wigo wa upelekaji wa umeme katika maeneo hayo. Tunakamilisha taratibu za kusaini mikataba kwa Wakandarasi ambao wanaonekana wanaweza wakaongezewa kazi katika maeneo yao ili waongezewe katika kilometa Mbili ambazo wanatakiwa kuzifanya katika vijiji vyote ambavyo tunavimalizia katika mradi huu wa mwisho wa REA III round II.