Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO K.n.y. MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Mahakama ya Wilaya ya Kibiti?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, kwanza nashukuru Serikali kwa majibu mazuri ya kuihakikishia Halmashauri au Wilaya ya Kibiti kupata Mahakama ya Wilaya. Nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Swali la kwanza; kwa kuwa sasa hivi Mahakama hiyo iko kwenye jengo la Mahakama ya Mwanzo ambalo limechakaa. Je, Serikali ina mpango gani kulitumia au kulifanya ukarabati jengo hilo ambalo litabaki kutumika kama Mahakama ya mwanzo?

Swali la pili; Mkoa wa Pwani una Mahakama za Mwanzo 21, kati ya hizo zipo ambazo zimechakaa na nyingine zimebomoka babisa ikiwemo ya Kibaha Vijijini pale Kata ya Ruvu na Kata ya Magindu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuzijenga hizi zilizobomoka na kuzifanyia ukarabati zile ambazo zimechakaa.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika,
ninakushukuru, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Michael Mbunge wa Kibaha Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nipende kufahamu endapo tutajenga Mahakama hii ya Kibiti hilo jengo ambalo sasa linatumika kama tutalikarabati. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba jengo hilo litaendelea kutumika na Mahakama ya Mwanzo kwa kuwa saa hizi wametuhifadhi Mahakama ya Wilaya, kwa hiyo tutalikarabati.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili anapenda kufahamu katika Mkoa wa Pwani Mahakama ya Mwanzo hizi mbili ambazo amezitaja. Mahakama yetu imeweka mpango kabambe wa kuhakikisha tunakarabati Mahakama zote ambazo zimechakaa, katika Mkoa wake wa Pwani tunakwenda kukarabati Mahakama 19 pamoja na hizi mbili ambazo amezitaja.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO K.n.y. MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Mahakama ya Wilaya ya Kibiti?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kuzijenga Mahakama za Mwanzo za West Meru Mkwaranga na Ngerenanyuki ambazo ziliachwa tu zikaharibika kabisa sasa hivi yamebaki magofu?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru, naomba nijibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Pallangyo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mpango wetu wa ujenzi na ikarabati wa mahakama katika mwaka huu wa fedha tunategemea kukarabati na kujenga Mahakama 60 za mwanzo. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika Mkoa wake pia Arumeru tumeweka Mahakama za kukarabati tutampatia list ataona Mahakama zake kama zinahitaji kukarabatiwa.