Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatafuta soko la uhakika la zao la vanilla?

Supplementary Question 1

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali madogo mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Mkoani Kagera kilimo cha vanila kilianza kwenye miaka ya tisini lakini hadi leo hakuna mfumo unaoeleweka wa kilimo cha vanila nchini. Je, ni lini Serikali sasa italeta mwongozo juu ya namna ya kulima, wakatoa huduma za ugani na wakaelekeza juu ya masoko?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa huko ulimwenguni katika nchi nyingine kilo ya vanilla inanunuliwa kati ya 800,000 mpaka 1,000,000 wakati mkulima wa Kagera anauza vanilla kwa 20,000, 15,000 mpaka 30,000 tu. Je, ni lini sasa Serikali kwa kutumia balozi zetu za nje wataweza kututafutia masoko yanayoeleweka ili kuweza kumnufaisha huyu mkulima kupata bei nzuri ya vanilla?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Benardeta Kasabago Mushashu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, wiki mbili zilizopita Wizara ya Kilimo pamoja na wadau wa zao la vanilla tulikutana tukafanya mkutano wa pamoja hapa Dodoma kwa lengo la kuandaa na kutengeneza mwongozo.

Mheshimiwa Spika, nilihakikishie Bunge lako kwamba tuko katika hatua za kuanza kuandaa mwongozo huo ambao utajumuisha masuala ya utafiti, kalenda ya mazao, mfumo wa bei, masoko na uzalishaji bora wa vanilla ambao unakidhi mahitaji ya soko la dunia, hasa ile ambayo ina vanillin na moisture content ambayo inahitajika kimataifa.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu masoko; baada ya mkutano huo wa wadau, sisi kama Wizara ya Kilimo tumeshawaandikia Ubalozi wa Tanzania Nchini China ikiwa ni moja ya sehemu ya masoko makubwa ya vanilla kuanza mazungumzo na ufunguzi wa soko hilo na tutafanya katika maeneo mengine ili kumsaidia mkulima wa vanilla aweze kupata soko la uhakika.