Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaongeza madarasa katika Shule ya Msingi Puma kutokana na kuzidiwa na idadi ya wanafunzi?

Supplementary Question 1

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya kaka yangu Naibu Waziri Deo Ndejembi nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa Shule ya Msingi ya Muhintiri inakabiliwa na changamoto hizo hizo ambazo Mheshimiwa Naibu Waziri ametoa majibu kwa Shule ya Puma.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kuambatana na mimi kwenda jimboni kujionea msongamano mkubwa wa wanafunzi katika shule hiyo na kuangalia namna ya kuweza kuwasaidia wanafunzi wa Shule Msingi ya Muhintiri?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niko tayari kuongozana na Mheshimiwa Kingu kuelekea katika shule hii ya Muhintiri ili kujionea msongamano huo na kuweza kuona ni hatua gani Serikali inaweza ikachukua kuweza kutoa msongamano huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaongeza madarasa katika Shule ya Msingi Puma kutokana na kuzidiwa na idadi ya wanafunzi?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru; je, ni lini sasa Serikali itaimarisha Shule za Msingi Salakwa, Salama A na Salama B, Salama na Nyarubundu; ni lini majengo ya shule hizi yamezeeka sana, ya muda mrefu, lini Serikali itatekeleza?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba baada ya session hii ya maswali nikae na Mheshimiwa Getere kuweza kuona ni hatua gani tunaweza tukazichukua za haraka kuweza kuzifanyia shule hizi matengenezo ambayo zinahitaji.