Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga shule ya Kidato cha Tano na Sita katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Kwa kuwa wananchi wako tayari kukamilisha majengo ya madarasa ambayo Serikali imetoa shilingi milioni 260 na uwezekano upo ndani ya miezi miwili majengo haya yakakamilika.

Je, anihakikishie Naibu Waziri mwezi Julai ujasili na uanzwaji wa kidato cha tano utakuwa tayari?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Shule ya Sekondari Mchoteka ina walimu watano tu wa sayansi.

Je, kukamilisha kidato cha tano na sita Serikali itapeleka walimu wa sayansi zaidi ili watoto wale wawe na ufaulu mzuri?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, shule hii kama nilivyokwishakusema kwenye majibu yangu ya msingi imeombewa usajili kutoka Wizara ya Elimu. Na kuona kama itakuwa tayari mwezi wa saba kuweza kupokea wanafunzi tutalifanyia kazi hili kwa haraka sisi Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu kuweza kupata usajili na kuona kama itaweza kupokea wanafunzi mwezi huu wa saba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili la ukosefu wa walimu wa sayansi. Bunge lako tukufu ni mashahidi kwamba Serikali imetoa ajira zaidi ya 21,000 ambapo katika hizo zipo za walimu na zipo za Idara ya Afya. Hivyo basi katika ajira hizi tutaiwekeza kipaumbele Shule hii ya Sekondari ya Mchoteka.

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga shule ya Kidato cha Tano na Sita katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 2

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi ya kuuliza swali moja. Shule ya Sekondari Kilindi Girls na Shule ya Sekondari Mlongwema zilizopo Wilaya ya Lushoto zina upungufu mkubwa wa mabweni lakini zinachukua watoto all over the country, ni form five na six.

Je, ni lini Serikali itapeleka mkakati maalum wa kuongeza mabweni katika shule hizi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wa Serikali upo wa kuendelea kutafuta fedha kuhakikisha kwamba shule zote zenye uhitaji wa mabweni yanaweza kujengwa. Nitoe rai kwa viongozi wa Halmashauri hii ya Lushoto na Kilindi kuanza kuhamasisha wananchi kuanza ujenzi wa mabweni na Serikali inaweza ikaja kuja kuyamalizia majengo hayo kama walivyofanya kule Mchoteka kwa Mheshimiwa Mpakate.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga shule ya Kidato cha Tano na Sita katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba niulize swali moja fupi. Kwa vile Kata ya Mamba Kaskazini na Mamba Kusini kuna shule nyingi za sekondari lakini hatuna shule hata moja ya kidato cha tano na sita.

Je, Serikali iko tayari kuipandisha hadhi Shule yaSekondari ya Mboni kwa kuijengea pia hosteli?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye shule hizi ambazo amezitaja Mbunge za Mamba Kaskazini na Mamba Kusini, utaratibu ni ule ule kuweza kujenga miundombinu ambayo inatakiwa ili kupandisha hadhi shule halafu kuiombea usajili kutoka Wizara ya Elimu. Tutakaa na Mheshimiwa Mbunge kuona shule hizi kama miundombinu inakidhi vigezo, na kama inakidhi vigezo basi tuone taratibu za kuombea usajili wa kuweza kupata mkondo wa kidato cha tano na sita.

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga shule ya Kidato cha Tano na Sita katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi. Shule ya Sekondari ya Kumkubwa ni shule ya kidato cha tano na sita inayotumia majengo chakavu yaliyokuwa kambi ya wakimbizi.

Je, ni lini Serikali itajengea miundombinu ya madarasa katika Shule hii ya Sekondari ya Kumkubwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lengo la Serikali kuboresha miundombinu ya shule zote, si tu za sekondari, kuanzia za msingi, sekondari na hizi za A-level. Hivyo basi tutaona ni namna gani ambavyo tunaweza tukaanza ukarabati wa shule hii ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja.

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga shule ya Kidato cha Tano na Sita katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 5

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, swali langu, nataka kujua ni lini Serikali itaanza ujenzi wa shule ya mkoa ya mfano ya wasichana katika Mkoa wa Mtwara kama ilivyojenga kwenye mikoa mingine?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan imedhamiria kujenga shule hizi katika kila mkoa na tayari bilioni 30 ilishatoka kwa ajili kujenga shule kumi kwenye mikoa kumi ambao kila mkoa ilipata bilioni tatu. Tunaenda sasa kwenye hatua ya pili ambapo mikoa mitano itapokea hizi bilioni tatu pia kujenga na awamu ya tatu pia tutamalizia hizo shule nyingine na tutahakikisha Mkoa wa Mtwara pia nao unapata shule hii kwa wakati.