Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. FURAHA N. MATONDO K.n.y. MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: - Je, mpango wa kutumia majengo ya Sekondari ya Sengerema kuwa Chuo cha Madini na Uvuvi umefikia wapi?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri ametamka uhaba wa shule za A-Level na jambo hilo limejityokeza katika jimbo langu. Mpaka sasa hivi kuna A- Level mbili tu zinazofanya kazi wakati kuna kata 18 na tulishaomba kupandisha hadhi Shule ya Makong’onda kuwa A- Level; mchakato huu wa kupandisha hadhi utakamilika lini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, mchakato wa kupandisha hadhi shule kuwa na mkondo wa kidato cha tano na sita ni upo chini ya Wizara ya Elimu, maombi yale yanapelekwa Wizara ya Elimu. Nitakaa na Mheshimiwa Mchungahela kuona mchakato huu umefikia wapi na kuweza kumpa majibu hayo.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FURAHA N. MATONDO K.n.y. MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza: - Je, mpango wa kutumia majengo ya Sekondari ya Sengerema kuwa Chuo cha Madini na Uvuvi umefikia wapi?

Supplementary Question 2

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, nashukuru majibu mazuri ya Serikali lakini niombe tu kwa kuwa maeneo ya kanda ya ziwa yamezungukwa na madini ya kila aina.

Je, hamuoni haja ya kujenga chuo cha madini katika Wilaya ya Sengerema ili kuwapatia wananchi wetu wapate ujuzi lakini waweze kuchimba kitaalamu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kwa, kuwa sasa uvuvi umekuwa ni wa kisasa;

Je, hamuoni haja ya kujenga chuo cha uvuvi katika Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ili wavuvi wetu waweze kuvua kitaalam tuendane na kasi ya Uganda nan chi nyingine?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo umesema hapa haya masuala ambayo ni yako chini ya Wizara ya Madini. Sisi kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI tutakaa na wenzetu wa Wizara ya Madini. Swali lake la pili ni la Wizara ya Uvuvi, kuona mipango waliyonayo juu ya kuweka vyuo hivi katika kanda ya ziwa.