Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas Van Zeeland

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuiliza: - Je, ni kesi ngapi za Wakulima kulishiwa mazao yao zimeripotiwa na ngapi zimepelekwa Mahakamani?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS V. ZEELAND: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante. Naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Swali la kwanza; kwa kuwa yapo malalamiko kwa baadhi ya askari wako kutotenda haki ikiwemo kuchukua rushwa na kuziharibu hizi kesi za migogoro ya wakulima na wafugaji, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kuongozana nami baada ya Bunge hili la Bajeti kwenda kuwasikiliza wananchi wa Mvomero? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kutokana na jiografia yetu ya Mvomero, tuna uhaba mkubwa wa vituo vya polisi. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kutuongezea Vituo vya Polisi lakini pia kuvimalizia Vituo vya Polisi vilivyoanza kujengwa kwa nguvu za wananchi kikiwemo Kituo cha Polisi Turiani na Kituo cha Polisi Mvomero? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uwepo wa madai ya rushwa na kwamba Mheshimiwa amependekeza niende Mvomero pamoja naye kuwasilikiliza wananchi, hilo halina shida Mheshimiwa tutaongozana. Hata hivyo pale zinapokuwepo tuhuma za rushwa ushauri wangu wananchi waelekezwe kwenda kwenye vyombo vinavyosimamia sekta hiyo. Tunayo TAKUKURU kila Wilaya, kila Mkoa na Taifa, lakini kama inashindikana kuna Kamati ya Usalama inayoongozwa na Mkuu wa Mkuu wa Wilaya wanaweza wakapeleka manung’uniko huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia wapo Wakuu wa Mapolisi hawa wadogo wanaokuwa kwenye site kama OCD wanaweza pia kuwasikiliza, lakini nipo tayari kuungana naye kwenda kuwasikiliza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, juu ya swali la pili la kuongeza Vituo vya Polisi kwa sababu Wilaya ni pana, nitakapokwenda kwenye kikao hicho tutaweza kuviangalia vituo viwili vinavyoendelea kujengwa na kupata mapendekezo yako ni wapi kwingine wanapenda viongezwe ili viweze kuingizwa kwenye mipango yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuiliza: - Je, ni kesi ngapi za Wakulima kulishiwa mazao yao zimeripotiwa na ngapi zimepelekwa Mahakamani?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi ya swali la nyongeza katika Jimbo la Kilwa Kusini, Kata za Nanjilinji, Kikole na Kiranjeranje bado migogoro ya wakulima na wafugaji inaendelea. Je, ni nini jukumu la Jeshi la Polisi kuzuia na kukomesha kabisa migogoro hii badala ya kuendelea na kesi ambazo hatima yake inakuwa si nzuri sana? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uwepo wa migogoro katika eneo la Kilwa alilotaja Mheshimiwa Mbunge ni kweli tunafahamu na kuna maelekezo yalitolewa na Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa Wakuu wote wa Mikoa ambao ni Wenyeviti wa Kamati za Usalama na wadogo zao kwa maana ya Wakuu wa Wilaya, Wenyeviti wa Kamati za Usalama ngazi ya Wilaya kuwa na mipango ya usimamizi wa matumizi bora ya ardhi pamoja na kuwapanga wakulima na wafugaji kuepuka mwingiliano unaosababisha migogoro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa Jimbo la Kilwa na hizo kata tatu alizozitaja Mheshimiwa Mbunge nishauri tutumie infrastructure kwa maana ya miundombinu iliyopo ya upatanisho, Jeshi la Polisi kupitia Kitengo cha Polisi Jamii wanaendelea kuelimisha wananchi juu ya kupunguza migogoro isiyokuwa ya lazima kama hii. Hata hivyo, tuwaombe wataalam wetu wa ngazi za Serikali za Mitaa ambao hufanya uthamini wa uharibifu wa mazao kabla Polisi hawajachukua hatua za kurejesta kesi Mahakamani ili watimize wajibu wao ipasavyo, kwa sababu wakati mwingine wanaona inachelewa kumbe ni kutokana na kuchelewa kwa zile tathmini za wenzetu. Vinginevyo tuendelee kuwaelimisha wakulima na wafugaji, wote ni Watanzania, waishi kwa maelewano kila mmoja akitimiza wajibu wake, ahsante sana.