Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuupitia tena Muundo wa Utumishi wa Madaktari Bingwa wa mwaka 2022?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante. Namshukuru Waziri kwa majibu mazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa sababu swali langu ni swali la kiutumishi, je, Serikali inafahamu tofauti ya kati ya Vyama vya Wafanyakazi ambavyo vinatetea maslahi ya Utumishi na Vyama vya Kitaaluma kwenye kada husika? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; linakuja suala zima la uhuishwaji wa maslahi ya kiutumishi je, Serikali haioni kwamba kuna umuhimu wa kuwa unashirikisha Vyama vya Wafanyakazi ambavyo vimesajiliwa kisheria kutimiza maslahi ya wafanyakazi ili kuepusha sintofahamu ambayo imetokea kwa uhuishwaji wa mwaka jana 2022 kutangazwa kwamba Daktari Bingwa? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge Alice siyo tu kwa kufuatilia masuala ya Watumishi na Madaktari Bingwa, lakini kwa kazi kubwa ambayo anaifanya kusaidia wenzetu wa Mkoa wa Pwani haswa kwenye maeneo ya afya na masuala ya akinamama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, amesema katika swali lake la kwanza, je, tunafahamu tofauti ya vyama na vile vya kitaaluma. Ndiyo tunafahamu kuna Vyama vya Wafanyakazi lakini kuna vya Kitaluuma kama ambayo mimi na yeye tupo cha Madaktari cha Tanganyika tunafahamu tofauti ya hivyo viwili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile swali lake la pili kwamba je, wakati wa kuamua haya tunawashirikisha. Ndiyo maana imechelewa ni kwamba baada ya kutengeneza ile draft na kuona matatizo ambayo na wewe umeyaona hasa tunapofika kuna Madaktari super specialist ambao sasa kwenye muundo hawatambuliki, kuna watu walioongeza elimu kama manesi wengine wameongeza elimu lakini haifiki kwenye muundo, tulivyoyaona hayo tumemaliza sisi kama Wizara. Sasa tunataka tushirikishe hivyo vyama vyote, tukishashirikisha sasa, wakishakubali wote tunapeleka utumishi sasa kitu ambacho ni shirikishi na kimekubalika na pande zote.