Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUM M. ZODO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati wa miundombinu chakavu katika Vyuo Vikuu?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuwa kwenye majibu ya Waziri katika ukarabati wa awali nimesikia baadhi ya Vyuo Vikuu ambavyo vimekarabatiwa, lakini sikusikia Chuo Kikuu cha UDOM na kwa kuwa Chuo Kikuu cha UDOM kina changamoto sugu ya uhaba wa maji kwa miaka kumi na sita sasa toka 2007, ambayo inapelekea uchakavu wa majengo yale. Swali la kwanza; je, ni lini Serikali inakwenda kuondoa changamoto ya miundombinu ya maji katika Chuo Kikuu cha UDOM? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; kwa kuwa Chuo Kikuu cha UDOM kilikuwa kinajengwa kwa phase na kwa kuwa ujenzi wake bado haujakamilika, kuna uhaba wa madarasa na hakuna kabisa nyumba za watumishi. Je, Serikali imejipangaje sasa kwenda kumaliza phase za ujenzi wa Chuo Kikuu cha UDOM?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nilitaja baadhi ya Vyuo ambavyo tayari Serikali imeshapeleka fedha kwa ajili ya ukarabati na ku–improve miundombinu chakavu lakini sikutaja vyuo vyote ambavyo vimenufaika na fedha za Mradi wa HEET. Chuo Kikuu cha UDOM ni kati ya vyuo ambavyo vimenufaika na fedha za mradi huu wa HEET na tayari fedha zimeshapelekwa kwa ajili ya ujenzi. Suala la maji UDOM kwa ujumla wake tunaendelea kulishughulikia kwa kushirikiana na Wizara husika kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunapata utatuzi wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ujumla wake tunaongeza jitihada kuhakikisha kwamba vyuo vyote ikiwa ni pamoja na UDOM tunamaliza ujenzi na ukarabati katika maeneo ambayo yalikuwa hayajakamilika ili wanafunzi wetu waweze kupata huduma nzuri ya elimu ya juu.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. MWANTUM M. ZODO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati wa miundombinu chakavu katika Vyuo Vikuu?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Naomba kuuliza Swali dogo la nyongeza. Wakati ambapo wenzetu wanazungumzia kuboresha Vyuo Vikuu chakavu, Mkoa wa Njombe hauna Chuo Kikuu hata kimoja, mara kwa mara tumekuwa tukiomba na kwa kuwa Wilaya ya Makete tuko tayari kutoa eneo kwa ajili ya ujenzi wa Chuo Kikuu chochote kile ambacho unaweza kuona kinafaa;

Je, ni lini Serikali na ipi ahadi ya Serikali kwa wananchi wa Jimbo la Makete na Mkoa wa Njombe kwamba mtajenga Chuo Kikuu?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Festo Sanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza hakuna Mkoa hapa nchini ambao hauna Tawi la Chuo Kikuu Huria, ni kweli kama alivyosema Mheshimiwa Sanga kwamba Njombe siyo kati ya Mikoa ambayo inayo au itanufaika sasa hivi kwa mradi wa HEET kwa kuwa na kampasi ya Chuo Kikuu kwa jitihada ambayo Serikali imefanya kwa maelekezo ya Mheshimiwa Rais, tumesambaza kampasi katika Mikoa kadhaa. Mipango iko mbioni ya mazungumzo na Mkoa wa Njombe kuhakikisha kwamba tunapeleka kampasi kule. Ningeomba details tuzitoe baada ya kukamilisha mikakati hii, lakini tunatambua umuhimu huo na tunajua kwamba kulikuwa na ahadi ilitolewa pale Njombe kwamba Njombe na yenyewe itapata kampasi ya Chuo Kikuu.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. MWANTUM M. ZODO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati wa miundombinu chakavu katika Vyuo Vikuu?

Supplementary Question 3

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona. Je, Serikali ina mpango gani kujenga au kuboresha vituo atamizi katika vyuo vyetu vikuu au taasisi za elimu ya juu, kwani hivi vituo ndio chachu ya kutengeneza viwanda hapa nchini?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Profesa Ndakidemi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba vituo atamizi ni muhimu sana kwa ajili hasa ya kuunganisha juhudi za taaluma na maendeleo ya viwanda na maendeleo ya nyanja nyingine mbalimbali hapa nchini, nguvu kubwa tunazielekeza huko. Naamini hata baadhi ya Wabunge watakuwa wamepata fursa ya kuangalia wiki ya ubunifu ambayo inaendelea kwenye viwanja vya Jamhuri leo na juhudi ambazo tumezifanya na baadhi ya matokeo ambayo tayari tumeshazifanya. Kwa hiyo, tunalichukulia suala hili kwa umuhimu mkubwa na tutajitahidi sana kuongeza juhudi ya kuwa na vituo vyakutosha atamizi katika vyuo vikuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua kesho tunazindua Industrial Advisory Council ya Sokoine ambayo vilevile ni kwa ajili ya kuunganisha juhudi za maendeleo ya viwanda na Chuo Kikuu cha Sokoine na vyuo vingine vyote hapa nchini.