Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga daraja litakalounganisha Tanzania Bara na Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nimshukuru Waziri kwa majibu yake mazuri sana ambayo ameyatoa sasa hivi. Nilikuwa na kitu kwanza kidogo kabla sijampa maswali yangu ya nyongeza mawili niliyonayo.

Nashukuru kwamba mwezi wa Ramadhani wenzetu wa jamii, wenzetu humu Bungeni walituheshimisha sana, wote walikuwa wanavaa mashungi na wanaume walikuwa wakivaa kanzu pamoja na koti, hilo kwanza niwashukuru sana na Mwenyezi Mungu awajaalie wazidi kutufuata sisi wenzetu Waislam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maswali mawili ya nyongeza, zipo nchi zimefanikiwa kujenga daraja za umbali mrefu, kwa nini tusipate uzoefu kutoka kwao?

Swali langu la pili, je, kwa nini usitumike mpango wa ubia na sekta binafsi PPP kwa ajili ya ujenzi huo? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, upande wa Zanzibar na upande wa Tanzania Bara, wahusika tayari wameshakutana kwamba hili suala linazungumzika na lipo linachakatwa, bado yatokanayo na hilo hayajapatikana ikiwa ni pamoja na kulifanyia kazi lile alilosema Mheshimiwa Mbunge kupata uzoefu kutoka sehemu mbalimbali ambazo wenzetu wameshajenga madaraja mengine marefu kama haya, ndiyo maana tunasema yatokanayo na hayo bado lakini suala hilo lipo linafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la pili kuhusu PPP, ni kweli kabisa kwamba siyo mpango kwa maana ya Serikali ichukue fedha zake ijenge na hata hao walioonesha nia ni sekta binafsi. Kwa hiyo, tunaamini daraja hili kama litajengwa, litajengwa kwa mtindo wa PPP kama alivyoshauri Mheshimiwa Mbunge. Ahsante.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga daraja litakalounganisha Tanzania Bara na Zanzibar?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kuniona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Denmark kuna daraja linalounganisha Odense na Sealand na lilichukua muda mfupi sana kujengwa.

Je, Serikali inatueleza nini katika kupeleka mtu kama mwenye swali lake Mwantumu Dau Haji kwenda kulishuhudia ili tufupishe hayo maneno ya mazungumzo yalifanyika, yalifanyika kwa muda mrefu? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mazungumzo yalifanyika Mwezi Machi mwaka huu na huu ni mwezi Aprili. Kwa hiyo, kwa mradi mkubwa kama huu na daraja ambalo linaunganisha linategemewa liunganishe Bara na Zanzibar yako mambo mengi sana ambayo yatafanyika. Moja ya eneo ambalo tunafahamu ni Denmark lakini hata China wana madaraja mengi marefu. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kabla Serikali haijaanza kutekeleza lazima watajiridhisha kwa mambo mengi sana ikiwa ni pamoja na teknolojia mbalimbali ambazo zimetumika katika nchi nyingine ambazo wana madaraja marefu kama haya. Ahsante.