Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA K.n.y. MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, Serikali haioni ni busara kuuza nyumba kwa Wapangaji wa kota za Ukonga kwa kuwa wameishi miaka mingi bila kufanyiwa ukarabati?

Supplementary Question 1

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mzauri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru Serikali kwa kuanza ukarabati wa majengo haya ila kwa kuwa yamekaa muda mrefu, nataka kufahamu kama mwaka huu wa fedha unaokuja fedha zimetengwa kwa ajili ya kumaliza ukarabati kwa ajili ya majengo yote yaliyobakia na ukarabati utategemea kumalizika kwa muda gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili ni kwamba Serikali haioni umuhimu wa kujenga mradi kama ule wa Magomeni, Ukonga ili wananchi waweze kupata nyumba na majengo mengine waweze kukodiwa watumishi ikiwemo watumishi wa Magereza? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge yote kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, majengo ya Ukonga kota ni majengo yale madogo na ya zamani na mpango wa Serikali kama ilivyoelekezwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi maeneo yote ambayo yalikuwa na majengo yale ya zamani yaboreshwe ama yabadilishwe na Ukonga ikiwa ni moja ya eneo ambalo mwezi huu wataalam wamekwenda ku–assess na kupata ukubwa wa eneo halisi ili paweze kubadilishwa na kujenga majengo makubwa ya ghorofa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi mpango mzima ni kujenga majengo yanayokwenda juu badala ya kuejenga haya majengo madogo. Kwa hiyo, Ukonga kota ni sehemu mojawapo kama Temeke, Ilala kota, Kinondoni, Ghana Mwanza na hata Arusha. Kwa hiyo, maeneo yote haya tunafanya mabadiliko ya kujenga ghorofa kama ambavyo tumejenga Magomeni kota na tunavyoendelea Temeke, ahsante.

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA K.n.y. MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, Serikali haioni ni busara kuuza nyumba kwa Wapangaji wa kota za Ukonga kwa kuwa wameishi miaka mingi bila kufanyiwa ukarabati?

Supplementary Question 2

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafsi ya kuuliza swali la nyongeza.

Manispaa ya Moshi tunazo Kata ambazo ziko katika maeneo ya Majengo Kiusa na kota hizo zimechoka sana na ni za miaka mingi sana. Wako wapangaji ambao wameishi pale mpaka sasa hivi wana wajukuu na vitukuu.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha kota hizo au hata kama kuna uwezekano wa kuweza kuwauzia? Aahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu ssali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye jibu la pili kwenye majibu yangu ya nyongeza kwa Mheshimiwa Kapinga, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, awamu hii ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan; moja, ameshatoa maelekezo kwamba, pale ambapo mnaweza mkafanya na sekta binafsi, basi kuna haja ya kufanya hivyo. TBA kwa jinsi muundo wake ulivyokuwa, sasa hivi iko kwenye kubadilishwa ili iweze kufanya na private sector ili maeneo yote yale ambayo yalikuwa na quarters zilizochoka tuangalie uwezekano wa kuongea na wenzetu wa sekta binafsi ili kuharakisha kujenga majengo kwa ajili ya kutoa huduma kwa watumishi na viongozi wa Tanzania hii, ahsante. (Makofi)

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA K.n.y. MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, Serikali haioni ni busara kuuza nyumba kwa Wapangaji wa kota za Ukonga kwa kuwa wameishi miaka mingi bila kufanyiwa ukarabati?

Supplementary Question 3

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi hii. Kwa kuwa Serikali imekubali maombi ya wananchi na wakazi wa Magomeni Quarter, familia 644 kuwauzia nyumba hizo na kuwapunguzia bei ya ununuzi na vilevile kuwaongezea muda wa kulipa kutoka miaka 15 hadi 30. Swali langu: Je, Serikali iko tayari kupokea shukrani zangu za dhati pamoja na wananchi wa Magomeni Quarter kwa uamuzi wa Serikali kuwauzia nyumba hizo na kuboresha familia zao, kitendo ambacho kinaonekana ni kuboresha maisha ya wananchi wa Tanzania? Shukrani hizi zimwendee Mheshimiwa Rais na Mtendaji Mkuu wa TBA Bwana Kondoro. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tarimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, shukrani alizotoa Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, naomba nizipokee shukrani hizo ambapo ni kazi kubwa imefanyika, na kweli amejali wananchi waliokuwa wanaishi hapo, ahsante. (Makofi)