Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Chikola na Makanda katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, ninayo maswali mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Maweni, wananchi walijenga boma la kituo cha afya, miaka ya 2012, lakini mpaka sasaivi halijakamilishwa; je, nini kauli ya Serikali kuhakikisha kwamba boma hilo linaenda kukamilishwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Serikali ilitoa shilingi milioni 50 kwa ajili ya kukamilisha Zahanati ya Mhalala, Sasajila, Igose, Magasai na Mahaka; bahati mbaya zile fedha hazijatosha: Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba zile zahanati zinakamilishwa ili ziweze kuanza kutoa huduma? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, la kwanza; kwenye Kata ya Maweni, ujenzi wa kituo cha afya ambapo boma limekamilika toka mwaka 2012, Serikali itaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma haya ambayo yamejengwa na wananchi kwenye vituo vya afya na zahanati.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge, ameleta orodha hii ya zahanati ambazo anazitaja, na alinikabidhi mimi mwenyewe juzi hapa. Tutaendelea kutafuta fedha kwa ajili ta umaliziaji wa zahanati hizi, lakini kwa sasa kuna tathmini ambayo inafanyika kwa ajili ya ramani zile ambazo zilipelekwa mwanzoni kwenye majimbo mbalimbali hapa nchini kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ili kuweza kujua ni kiasi gani sasa kinahitajika kwa ajili ya kumalizia.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Chikola na Makanda katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 2

MHE. ALMASI A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniruhusu nami niulize swali la nyongeza kwa swali hili 226. Lini Serikali itaendeleza na kumalizia vituo viwili katika Kata za Usagali na Shitage? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kumalizia vituo vya afya hivi ambavyo amevitaja Mheshimiwa Mbunge na kadiri pale bajeti itakavyoruhusu, basi tutakwenda kuvimalizia.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Chikola na Makanda katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika,
ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Napenda kuuliza, ni lini Kituo cha Afya Mwaya, kilichopo Tarafa ya Mwaya, Wilayani Ulanga, kitafanyiwa ukarabati? Ahsante sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, ni kipaumbele cha Serikali kufanya ukarabati kwenye vituo vya afya ambavyo ni vya muda mrefu na tutaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuweza kufanyiwa ukarabati kituo cha afya ambacho amekitaja Mheshimiwa Dkt. Ishengoma.

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Chikola na Makanda katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 4

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Ni lini sasa Serikali itatekelea mapendekezo ya Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba ya ujenzi wa vituo vya afya katika Kata za Mwabomba na Bugando?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali imeshatafuta fedha ya kuweza kuangalia ujenzi au kuanza ujenzi wa vituo vya afya katika maeneo ya kimkakati hapa nchini. Tutaangalia vilevile Kwimba imetengewa kiasi gani kwa ajili ya kuanza ujenzi wa vituo vya afya hivi ambavyo Mheshimiwa Mbunge amevitaja.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Chikola na Makanda katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 5

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kata ya Idodyandole, Kata ya Gondi na Kata ya Ipande ni kata kubwa sana, na tulileta mapendekezo: Je, lini Serikali itatoa pesa kwa ajili ya kituo hiki cha afya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwa bahati nzuri, ni hivi karibuni tu Mheshimiwa Massare ameleta orodha hii ya kuomba vituo hivi vya afya na Serikali itaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kwenda kujenga kituo cha afya kipya katika maeneo ambayo ameyataja.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Chikola na Makanda katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 6

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Wananchi wa Kata ya Busangwa, Kijiji cha Mwanima, wameshaandaa eneo la ekari 15 kwa ajili ya ujenzi wa health center na tayari wameshaanza ufyatuaji: Nini mpango wa Serikali wa kuhakikisha kwamba wana-support kwa ajili ya kukamilisha mradi huu? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, ni mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba tunajenga vituo vya afya kwenye maeneo ya kimkakati. Tayari kuna fedha ambayo imeshatengwa kwa ajili ya ujenzi wa vituo hivi vya afya kwenye maeneo kama anavyotaja Mheshimiwa Mbunge hapa. Kwa Busangwa, tutaangalia kama eneo hili pia limetengewa kwenye mwaka wa fedha huu ambao tunaenda kuuanza.

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Chikola na Makanda katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 7

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Jengo la Tunduru Kusini, Kata ya Marumba, ni moja ya kata ya kimkakati kwa ajili ya kujenga kituo cha afya, ambayo ina umbali wa kilometa 80 kutoka Makao Makuu ya Halmashauri: Je, ni lini Serikali itapeleka pesa kwa ajili ya kujenga kituo cha afya katika Kata ya Marumba?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nilisema hapo awali, tayari Serikali imetafuta fedha kwa ajili ya kujenga vituo vya afya vya kimkakati katika maeneo mbalimbali nchini. Tutaangalia pia Kata ya Marumba kama ipo imetengewa bajeti kwenye mwaka wa fedha unaokuja, kama haijatengewa, basi tutaitengea fedha kwenye ule mwaka mwingine wa fedha wa 2024/2025.