Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka fedha kumalizia ujenzi wa Vituo vya Afya Geterer na Masieda?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, Mbulu Vijijini tumeshaanzisha slogan ya kuhamasisha ujenzi wa vituo vya afya mimi na DC Kheri James. Tuna vituo vya afya vya Hayderer, Geterer, Masqaroda, Dinamu, Ladha, Endamilay na Maghang. Je, uko tayari sasa kupeleka fedha hizo ili kuzihamasisha juhudi za wananchi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa kuwa, Hospitali ya Halmashauri bado haijaisha na inahitaji Shilingi milioni 500 na Kituo cha Hydom hakina jengo la upasuaji: Je, ni lini utapeleka fedha hizo ambazo maombi yetu unayo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwenye swali lake la kwanza la nyongeza la lini Serikali itapeleka fedha kuunga mkono juhudi za wananchi za kujenga vituo vya afya; kwanza, nampongeza Mheshimiwa Mbunge na Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya, tumeona jitihada kubwa wanayoifanya katika kujenga vituo hivi vya afya. Serikali itajitahidi kadiri ya upatikanaji wa fedha kuweza kutenga bajeti kwa ajili ya kwenda kuongeza nguvu pale ambapo wananchi watakuwa wameishia.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili, tayari Hospitali ya Wilaya imeshawekwa kwenye bajeti hii tunayoenda kuitekeleza ya 2023/2024, shilingi milioni 500. Fedha hizi zitakwenda kwa ajili ya ukamilishaji wa hospitali hiyo. (Makofi)

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka fedha kumalizia ujenzi wa Vituo vya Afya Geterer na Masieda?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Ujenzi wa Kituo cha Afya Kitaya umeshakamilika: Ni lini dawa na vifaa tiba vitapelekwa ili kianze kutoa huduma kwa wananchi wa Kitaya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tayari Serikali imeanza kupeleka vifaa tiba kwenye vituo vya afya mbalimbali hapa nchini na Waheshimiwa Wabunge wengine watakuwa ni mashahidi, vifaa tiba vinavyoenda ni vile vya kisasa kabisa ambapo zamani vilikuwa vinapatikana kwenye Hospitali za Rufaa. Hii ni juhudi kubwa sana ya Mheshimiwa Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Katika kituo hiki cha afya ambacho amekitaja Mheshimiwa Mbunge, tutahakikisha vifaa tiba vya kisasa kabisa vinaenda pale kuweza kupeleka huduma karibu, kwa Watanzania.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka fedha kumalizia ujenzi wa Vituo vya Afya Geterer na Masieda?

Supplementary Question 3

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, Jimbo la Kibaha Vijijini kwenye Kata ya Kwala, tulipokea pesa kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya; je, ni lini Serikali itamalizia fedha zilizobaki kwa ajili ya kukamilisha na kuanza kazi? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali inafanya tathmini ya vituo vya afya vyote vilivyopelekewa pesa na ambavyo havikukamilika. Pale tathmini itakapokamilika, basi tutatenga fedha kwa ajili ya kuweza kumalizia vituo hivi vya afya.