Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Paulina Daniel Nahato

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mabweni kwenye shule za wasichana wanaosoma masomo ya sayansi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza. Ni nini mkakati wa Serikali wa kujenga mabweni ya wasichana katika shule za sekondari za kata nchini? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Je, katika shule hizo kumi ambazo mnajenga, ni nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha shule hizo zinafunguliwa ifikapo Julai, mwaka 2023? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI
ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimesema kwenye majibu yangu ya msingi, kwa sasa kipaumbele cha Serikali ni kujenga shule maalum hizi za bweni za wasichana katika kila mkoa katika nchi yetu hii. Hii itaenda kusaidia kupunguza dropout na mimba za utotoni, kwa sababu watoto wote katika mkoa ule wataenda kwenye shule hizi maalum.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili, baadhi ya shule hizi ambazo zimejengwa, shilingi bilioni 30 imekwenda katika mikoa kumi kwa maana ya shilingi bilioni tatu kila Mkoa. Tayari baadhi ya shule hizi zimesajiliwa na ifikapo Julai mwaka huu 2023 shule hizi zote kumi zitaanza kupokea wanafunzi wa kike ili kuanza masomo yao ya sayansi katika maeneo hayo ambayo fedha imeshaenda.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mabweni kwenye shule za wasichana wanaosoma masomo ya sayansi?

Supplementary Question 2

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Bweni la Sekondari ya Mlongwema ni dogo sana na halikidhi mahitaji kwa wanafunzi wale; je, Serikali ina mpango gani wa kujenga bweni kubwa ambalo linaweza kukidhi mahitaji ya wanafunzi wa Mlongwema? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, ni kipaumbele cha Serikali kujenga mabweni katika shule zote za A-Level. Tutakaa na Mheshimiwa Mbunge kuweza kuona shule hii ambayo ameitaja mahitaji hasa ni yapi ili tuweze kutafuta fedha ya kwenda kumalizia au kujenga mabweni mapya katika shule hiyo.

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mabweni kwenye shule za wasichana wanaosoma masomo ya sayansi?

Supplementary Question 3

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Wananchi wa Jimbo la Kwela wamejitahidi kuanza kujenga mabweni katika Sekondari za Mpui, Mzindakaya, Milenia na Vuma. Je, ni lini Serikali mtaunga mkono jitihada hizi kwa kuwapelekea fedha?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Kwela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali itapeleka fedha kuunga mkono juhudi za wananchi wa Kwela kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha. Ni kipaumbele kuhakikisha kwamba tunajenga mabweni katika shule hizi ambazo hasa ni za A- Level katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mabweni kwenye shule za wasichana wanaosoma masomo ya sayansi?

Supplementary Question 4

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Wananchi wa Kata ya Lumuli ambayo iko Jimbo la Kalenga, Mkoa wa Iringa, walijenga maboma kwa ajili ya mabweni ya watoto wa kike, kwa miaka 13 sasa hayajamaliziwa. Ni lini Serikali itamalizia mabweni haya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokuwa nimeshasema hapo awali, Serikali itamalizia mabweni haya, hata hili la Lumuli kule Kalenga, kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha. Na tutaangalia katika mwaka huu wa fedha ambao tunakwenda kuuanza wa 2023/24 kama shule hii imetengewa fedha ili mabweni haya yaweze kukamilishwa na Serikali kuunga mkono juhudi za wananchi katika eneo hili.