Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE K.n.y. MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara ya Km 10 kwa kiwango cha lami Mjini Tunduma?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali ambayo yanatia moyo, kuna barabara nyingine ndani ya Mkoa wetu wa Songwe ambazo zimekwama, kwa mfano barabara ya kutoka Mlowo – Itaka – Kamsamba na Barabara ya Mbalizi – Utengule mpaka Mkwajuni kule kwa Mheshimiwa Mulugo, zote hizo zina ahadi nyingi na ninaomba Serikali itilie mkazo zipate kutekelezwa.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa George Ranwell Mwenisongole, Mbunge wa Mbozi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kujenga barabara hizi, hasa hizi alizozitaja Mheshimiwa Mbunge kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha. Katika mwaka huu wa fedha tunaokwenda wa 2023/2024, Bunge lako tukufu limeiidhinishia TARURA zaidi ya shilingi bilioni 772 kwa ajili ya kutengeneza barabara mbalimbali hapa nchini, na ninaamini katika hizi barabara za Mlowo ambazo amezitaja Mheshimiwa Mbunge nazo zitawekwa katika kipaumbele cha mwaka huu wa fedha tunaokwenda kuutekeleza.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE K.n.y. MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara ya Km 10 kwa kiwango cha lami Mjini Tunduma?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati barabara ambazo zimeathirika na mvua katika Jimbo la Mbagala?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abdallah Jafari Chaurembo, Mbunge wa Mbagala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni mkakati wa Serikali kutengeneza barabara hizi na ndiyo maana TARURA walikuwa na emergency fund ya shilingi bilioni 11 na sasa wameomba tena nyongeza iweze kufika shilingi bilioni 46 kwa ajili ya kutengeneza barabara hizi za Mbagala na za maeneo mengine ya Waheshimiwa Wabunge ambayo yameathiriwa na mvua ambazo zimeendelea kunyesha hapa nchini.